DRC yachaguliwa katika Baraza la Haki za Kibinadamu la Umoja wa Mataifa licha ya mabishano

Radio Fortune Africa -Na Cantona Joseph

https://zeno.fm/radio/radio-fortune-africa

Jamhuri ya Kidemokrasia ya Kongo imechaguliwa rasmi hivi punde siku ya Jumatano kwenye Baraza la Haki za Kibinadamu mjini Geneva, pamoja na Benin, Gambia, Kenya na Ethiopia kwa kundi la Afrika, licha ya kuwepo kwa utata kuhusu ukiukaji wa haki za binadamu nchini humo. Nchi hizo tano zitaketi kwa miaka mitatu, kuanzia Januari 1.

Rais wa Jamhuri ya Kongo Denis Sassou Nguesso akizungumza wakati wa Mkutano Mkuu wa Umoja wa Mataifa kwenye Makao Makuu ya Umoja wa Mataifa Septemba 21, 2023 huko New York.
Rais wa Jamhuri ya Kongo Denis Sassou Nguesso akizungumza wakati wa Mkutano Mkuu wa Umoja wa Mataifa kwenye Makao Makuu ya Umoja wa Mataifa Septemba 21, 2023 huko New York. © Kena Betancur / Getty Images via AFP

Ikiwa na kura 172 kati ya wapiga kura 190, Jamhuri ya Kidemokrasia ya Kongo (DRC) imechaguliwa kwa kiasi kikubwa katika Baraza la Haki za Kibinadamu, ambalo makao yake makuu yanapatikana Geneva – kwani kulikuwa na wagombea watano tu kwa viti vitano upande wa kundi la Afrika kwa viti 18 vilivyosambazwa alasiri huko New York.

Mzozo uliokuwa umepamba moto mjini Kinshasa, ambapo wapinzani waliitaka serikali kuheshimu haki za binadamu zaidi kabla ya kugombea kwenye Baraza la Haki za Binadamu la Umoja wa Mataifa, ulifanikiwa kwa kiasi fulani huko New York. Baadhi ya mashirika yasiyo ya kiserikali yakinyooshea kidole kukamatwa kiholela kwa mgombea wa upinzani Seth Kikuni, wanaharakati Jacques Sinzahera, Gloire Saasita, Gloria Senga, Robert Bunda na Chadrack Tshadio kwa mfano.

Shirika lisilo la kiserikali la Human Rights Watch hivyo limelaani ukandamizaji mkali wa mamlaka kwa wanachama wa vyama vya upinzani, wanaharakati wa mashirika ya kiraia, wakosoaji wa serikali na waandishi wa habari katika kipindi chote cha uchaguzi wa urais wa mwaka 2023. “Tuna wasiwasi kwa upande wa Human Right Watch kwa raia wa Congo, wanachama wa mashirika ya kiraia na waandishi wa habari kuhusu kuongezeka kwa ukandamizaji wa haki za kiraia na kisiasa,” anasema Carine Kaneza Nantulya, naibu mkurugenzi wa shiŕika la Human Rights Watch kanda ya Afrika.

Pia anabainisha kuwa, mbali na hatia chache, maafisa wa usalama katika vikosi vya usalama vya Kongo waliohusika na mauaji ya watu wasiopungua 57 huko Goma mnamo Agosti 2023 hawajawajibishwa kikweli. HRW imezitaja Ethiopia na Kenya kwa ukiukwaji mkubwa wa haki za binadamu.

Kwa upande wao, baadhi ya wanadiplomasia wa Geneva wanaeleza kuwa kukaa katika Baraza la Haki za Kibinadamu kunahitaji wanachama wake kurekebisha utendaji wao katika eneo hili kwa muda mrefu. Carine Kaneza Nantulya angependelea kuona maendeleo kabla ya uchaguzi: “Ni muhimu kwamba serikali zichukue kwa uzito kwamba uchaguzi kama huo usiwe wa kutia moyo haswa, lakini tuzo inayopatikana baada ya kazi ngumu na kazi ambayo tunapaswa kutathmini vyema. “

“Ulimwengu wote utatutegemea kutazama na kuangalia ikiwa tunastahili mahali hapa”

Kufuatia kutangazwa kwa uchaguzi huu, mtetezi wa haki za binadamu na mkurugenzi mtendaji wa shirika lisilo la kiserikali la Afya Mama, Annie Modi hakuficha hisia zake na kuzialika mamlaka kupima wigo wa nafasi hii ndani ya mfumo wa Umoja wa Mataifa. “Unapokaa katika taasisi hizi, sio kwako tu, ni kwa nchi zingine. Ni kwa kuwa kielelezo ndipo tunaweza kudai kutathmini mataifa mengine juu ya ulinzi na dhamana ya haki za binadamu dhidi ya raia wetu. “

Pia anasisitiza juu ya jukumu la kuwa na mfano wa kuigwa: “Ulimwengu wote utatugeukia kutazama na kuangalia ikiwa tunastahili mahali hapa. Mamlaka za Kongo zina wajibu na fursa ya kuonyesha maendeleo kuhusu haki za binadamu kwa wote. “

Kwa upande wake, Jonas Tshiombela, mkuu wa shirika mpya la Kiraia, anaorodhesha kesi za ukiukaji wa haki za binadamu zilizorekodiwa wiki hii ambazo pia zinahusisha vyombo vya usalama. “Jambo la kushangaza zaidi ni ukatili ambao uliambatana na matakwa ya wanafunzi katika mkoa wa Kongo ya Kati, huko Matadi. Pia kuna ghasia kuhusu kukamatwa kwa mwanahabari Patrick Lokala na mazingira ya kuwekwa kizuizini. DRC lazima isifiche, kwa uchaguzi huu, kesi hizi zote za ukiukwaji wa haki za binadamu katika nchi yetu. “

Kwa upande wao, mamlaka ya Kongo imefurahishwa na uchaguzi huu, kuhakikisha wanatekeleza wajibu huu.

All Rights Reserved © Cantona Group PLC||2024


Discover more from cantonadigital

Subscribe to get the latest posts sent to your email.

Leave a Reply