Mgogoro wa Gaza waangaziwa kwenye Mkutano wa G7

Na Cantona Joseph June 17, 2026 06:00 (EAT)

Serikali ya Guinea ya Ikweta imejiuzulu baada ya kushindwa kutimiza malengo yake, Makamu wa Rais Teodoro Nguema Obiang Mangue amesema.
Obiang, ambaye pia ni mtoto wa Rais Teodoro Obiang Nguema Mbasogo, alisema waziri mkuu aliwasilisha tangazo la kujiuzulu kwa wanachama wote wa serikali kwa sababu ilikuwa imefikia 10% ya malengo yake.
Hakutaja malengo lakini taarifa ya chama tawala ilisema rais ameona kuwa serikali inakuza ufisadi na imeshindwa kuleta mseto wa uchumi.
Rais Obiang ndiye kiongozi aliyekaa madarakani kwa muda mrefu zaidi duniani na kuitawala nchi hiyo yenye utajiri wa mafuta ya Afrika Magharibi tangu mwaka 1979 kwa mkono wa chuma, huku akiwateua jamaa zake kushikilia nyadhifa muhimu serikalini.
Rais aliteua serikali inayoondoka mwaka 2024, huku Manuel Osa Nsue Nsua akiwa waziri mkuu.
Siku ya Jumanne, makamu wa rais alisema hatua hiyo inaambatana na “kanuni kwamba wajibu katika usimamizi wa umma lazima uambatane na matokeo”.
“Kiwango cha utekelezaji kilichopatikana hakitoshi kuhusiana na matarajio na ahadi zilizofanywa,” aliandika kwenye mtandao wake wa X.
Katika taarifa kwenye Facebook, chama tawala nchini Guinea ya Ikweta (PDGE) kilisema rais hakuridhishwa na usimamizi wa serikali inayoondoka.
Meli za mafuta za Iran zavuka kizuizi cha majini cha Marekani

Meli za mafuta za Iran zimepita eneo lililowekwa kizuizi cha Marekani katika bandari za Iran kwa karibu miezi miwili, tovuti ya ufuatiliaji wa meli TankerTrackers ilionyesha Jumatano, siku mbili kabla ya Tehran na Washington kusaini makubaliano ya kumaliza vita na kuanza mazungumzo juu ya makubaliano ya mwisho.
TankerTrackers.com, ambayo hufuatilia usafirishaji wa mafuta na orodha ya bidhaa kwenye mtandao wa X, ilionyesha “mauzo ya kwanza ya mafuta ghafi ya Iran katika miezi miwili,” kulingana na data ya ufuatiliaji wa kidijitali kuwa kutumia picha za satelaiti.
Mazungumzo kuhusu suluhisho la mwisho kuhusu mpango wa nyuklia wa Iran na kuondolewa kwa vikwazo yanatarajiwa kuanza Ijumaa katika eneo la Bürgenstock nchini Uswizi, huku taarifa za kufunguliwa tena kwa Mlango wa Bahari wa Hormuz zikichangia kushuka kwa bei ya mafuta duniani.
Israel yashambulia maeneo kadhaa kusini mwa Lebanon

Israel imeanzisha mashambulizi katika maeneo kadhaa kusini mwa Lebanon, huku makao makuu ya Khatam al Anbiya yakionya kuwa iwapo mashambulizi hayo hayatasitishwa, Israel inapaswa kujiandaa kwa “jibu kali”.
Iran imesisitiza kuwa usitishaji wa mapigano nchini Lebanon ni sehemu muhimu ya maelewano yaliyofikiwa kati yake na Marekani.
Jana,pembezoni mwa mkutano wa viongozi wa G7, Rais wa Marekani Donald Trump alimkosoa vikali Waziri Mkuu wa Israel Benjamin Netanyahu kutokana na mashambulizi ya Israel dhidi ya Lebanon.
Wakati huo huo, Makamu wa Rais wa Marekani amesema kuwa iwapo Tehran itazingatia kikamilifu masharti yote ya maelewano hayo.
Israel na Hezbollah zimekabiliana mara kadhaa tangu makubaliano ya Marekani na Iran yatangazwe Jumapili usiku.
Mapema siku hiyo, Israel ilishambulia mji wa Beirut kujibu mashambulizi ya roketi ya Hezbollah.
Trump aliiambia G7 kuwa alikuwa na “uhusiano wa karibu” na Netanyahu lakini “hakuridhishwa na shambulio… hilo lilikuwa kubwa mno”.
Waathiriwa wa Ebola Afrika wanapendelea waganga wa kienyeji kuliko hospitali

Kila mara kunapokuwa na mlipuko wa Ebola, baadhi ya walioathiriwa huchagua njia ya kwenda hospitali iliyo karibu. Wengine hufuata njia ya kuelekea kwenye madhabahu ya mganga wa kienyeji, na thari zake huwa mbaya zaidi.
Wengi wanaona mwanzo wa homa ya kutokwa na damu kama ugonjwa wa kiroho na hutafuta dawa za mitishamba na maombi badala ya kwenda hospitalini.
Hivi ndivyo ilivyo sasa nchini Kongo, ambayo inakabiliwa na mlipuko wake wa kumi na saba wa Ebola tangu 1976, wakati virusi hivyo kugunduliwa kwa mara ya kwanza katika mfumo ikolojia tajiri wa Bonde la Congo.
Miongo mitano baadaye, virusi hivyo vinaendelea kuwachanganya wagonjwa wengi barani Afrika ambapo wengine wanageukia viongozi wa kidini kuwa wahudumu.
Waathiriwa wa mlipuko wa sasa ni pamoja na wafanyakazi wa afya bila vifaa vya kujikinga pamoja na wachungaji na waumini waliokusanyika wakati Ebola ikienea, kulingana na wafanyakazi wa kibinadamu na wengine waliozungumza na The Associated Press.
Ebola huenea kupitia kugusana kwa karibu na majimaji ya mwili ya wagonjwa au waliofariki.
Mlipuko wa sasa unatia wasiwasi hasa katika eneo ambalo wengi hawaamini wafanyakazi wa afya na wanakataa kutafuta huduma ya matibabu.
Upinzani Congo walaani muswada mpya unatoa fursa kwa Tshisekedi kugombea muhula wa tatu

Upinzani wa Congo siku ya Jumanne umelaani kupitishwa kwa muswada ambao unaweza kutoa fursa kwa Rais Félix Tshisekedi kugombea muhula wa tatu, ukishutumu kile wanachosema ni unyakuzi wa madaraka.
Muswada huo, uliopitishwa na Seneti Jumatatu, utawezesha kura ya maoni kuhusu katiba mpya ambayo mihula ya awali ya Tshisekedi haitahesabiwa. Tayari umepitishwa na Bunge la Kitaifa na sasa unasubiri saini ya rais.
Tshisekedi, mwenye umri wa miaka 62, amekuwa madarakani tangu mwak 2019. Amesema kwamba atagombea muhula wa tatu, ikiwa wapiga kura wataukubali kupitia kura ya maoni. Lakini hakuna tarehe iliyowekwa.
Katiba ya Congo inakataza waziwazi marekebisho yoyote ya mipaka ya mihula ya urais. Muswada huo unaruhusu rais kurekebisha katiba iwapo kutatokea “hitilafu kubwa” inayoathiri taasisi za serikali.
Taiwan yaishutumu Kenya kwa kuzuia wajumbe wake

Serikali ya Taiwan siku ya Jumanne imesema kuwa inajiondoa katika Kongamano la masuala ya Bahari Yetu (OAC) linalofanyika huko Mombasa baada ya wajumbe wawili kuzuiwa kuingia na kukamatwa na mamlaka ya uhamiaji ya Kenya kutokana na shinikizo la China.
Kulingana na Wizara ya Mambo ya Nje (MOFA) na Baraza la Masuala ya Bahari waandaaji wa tukio la kabla ya mkutano walikataa kutoa idhini kwa wajumbe kwa sababu hawakutambua pasipoti ya Taiwan.
Baadaye, wajumbe wawili walikamatwa kwa nguvu na mamlaka ya uhamiaji ya Kenya kwa saa 20, ambapo pasipoti na simu zao za mkononi zilichukuliwa, na kurejeshewa kwao baada ya mamlaka kuwaruhusu kupanda ndege karibu siku moja baadaye.
Kwa mujibu wa gazeti la Taipei Times, mamlaka za Kenya zilikataa kutambua pasi zao za kusafiria za Jamhuri ya China (Taiwan) na kwamba juhudi za serikali ya Taiwan kushughulikia suala hilo hazikufaulu.
All Rights Reserved © Cantona Group PLC||2026
afghanistan, africa, albania, algeria, America, american-samoa, andorra, angola, anguilla, antarctica, antigua-and-barbuda, argentina, armenia, aruba, arusha, australia, austria, azerbaijan, bahamas, bahrain, bangladesh, barbados, belarus, Belgium, belize, benin, bermuda, bhutan, bolivia, bosnia-and-herzegovina, botswana, Boukinafaso, brazil, brunei-darussalam, bulgaria, burkina-faso, burma, burundi, california, cambodia, cameroon, canada, cape-verde, cayman-islands, central-african-republic, Chad, chicago, chile, china, christmas-island, cocos-keeling-islands, colombia, comoros, congo, cook-islands, costa-rica, cote-divoire-ivory-coast, Croatia, cuba, cyprus, czech-republic, darsalaam, democratic-peoples-rep-north-korea, democratic-republic-of-the-congo-kinshasa, denmark, djibouti, dodoma, dominica, dominican-republic, dr-congo, dubai, east-timor-timor-leste, ecuador, egypt, egypty, el-salvador, england, equatorial-guinea, equitorial-guinea, eritrea, estonia, eswatini, ethiopia, falkland-islands, faroe-islands, federal-states-of-moldova, fiji, finland, Florida, france, french-guiana, french-polynesia, french-southern-territories, gabon, gaza, georgia, germany, ghana, gibraltar, goma, Greece, greenland, grenada, guadeloupe, guam, guatemala, guinea, guinea-bissau, guyana, habari, haiti, holy-see, honduras, hong-kong, houston, hungary, iceland, india, indonesia, Iowa, iran, iran-islamic-republic-of, iraq, ireland, israel, italia, italy, ivory-coast, jamaica, japan, jordan, karatu, kazakhstan, kilimanjaro, kinshasa, kiribati, kiswahili, korea, kosovo, kuwait, kyrgyzstan, lao, latvia-lebanon-lesotho-liberia-libya-liechtenstein-lithuania-luxembourg, Lebanon, liberia, macau, madagascar, malawi, malaysia-maldives, Mali, malta, marshall-islands-martinique-mauritania-mauritius, massechutes, mayotte, mazingira, mbeya, meru, mexico, miami, micronesia, monaco-mongolia-montenegro, montserrat, morocco, mozambique-myanmar, mtwara, mwanza, namibia, nauru, nepal, netherlands, netherlands-antilles, nevada, new-caledonia, new-zealand, newyork, nicaragua, niger, nigeria, niue, north-macedonia, northern-mariana-islands, norway, oman, pakistan, palau, palestine, palestinian-territories, panama, papua-new-guinea, paraguay, peoples-democratic-republic, peru, philadhephia, philipians, Philippines, pitcairn-island, poland, politics, Portugal, puerto-rico, qatar, republic-of, republic-of-brazzaville, republic-of-south-korea, reunion-island, romania, Russia, russian-federation, rwanda, sahara-occidental, saint-kitts-and-nevis, saint-lucia, saint-vincent-and-the-grenadines, samoa, san-marino, sao-tome-and-principe, saudi-arabia, saudiarabia, scotland, Senegal, serbia, seychelles, sierra-leone, Singapore, singida, slovakia-slovak-republic, slovenia, solomon-islands, somalia, southafrica, spain, sri-lanka, sudan, suriname, swaziland-eswatini, sweden, switzerland, syria, syrian-arab-republic, tabora, taiwan-republic-of-china, tajikistan, tanzania, texas, thailand, the-gambia, tibet, timor-leste-east-timor, togo, tokelau, tonga, toronto, trinidad-and-tobago, tunisia, turkey, turkmenistan, turks-and-caicos-islands, tuvalu, uganda, united-arabs-emirates, united-kingdom, united-states, uruguay, uzbekistan, vancover, vanuatu, vatican-city-state-holy-see, venezuela, vietnam, virgin-islands-british, virgin-islands-u-s, wallis-and-futuna-islands, wallis-and-futuna-islands, wallis-et-futuna, washington-dc, western-sahara, yemen, zambia, zambie, zimbabwe
Discover more from cantonadigital
Subscribe to get the latest posts sent to your email.