Na Cantona Joseph Julai 01, 2026 08:40 (EAT)

Mpatanishi mkuu wa upande wa Iran, Mohammad Bagher Ghalibaf, ameeleza katika mahojiano na televisheni ya taifa ya nchi hiyo kuwa Tehran haitaacha kujilinda iwapo mazungumzo na Marekani hayatatoa matokeo.

Iran yatangaza likizo ya umma ili kujiandaa kwa mazishi ya Khamenei

f

Serikali ya Iran imetangaza Jumanne, Julai 6, kuwa siku ya mapumziko ya umma mjini Tehran.

Msemaji wa serikali ya Iran, Fatima Mohajerani, amesema hatua hiyo inalenga kuwezesha waombolezaji wa kiongozi wa zamani wa Iran kurejea kutoka mji mkuu.

Pia amesema siku ya maombolezo ya kitaifa itaadhimishwa nchini Iran siku ya Alhamisi, huku mazishi ya Ali Khamenei yakitarajiwa kufanyika mjini Mashhad Julai 8.

Kwa mujibu wa ratiba rasmi, sala za mazishi na shughuli za kuaga mwili wa Khamenei zitafanyika kati ya Julai 4 na 8 katika miji ya Tehran, Qom na Mashhad. Hafla za kutoa pole pia zitafanyika katika miji ya Baghdad, Kazmin, Karbala na Najaf nchini Iraq.

Inakumbukwa kuwa Ali Khamenei aliuawa katika mashambulizi ya anga ya Marekani na Israel dhidi ya Iran yaliyolenga makazi na ofisi yake, maarufu kama Nyumba ya Uongozi, lakini hadi sasa bado hajazikwa.

Mvulana wa miaka mitatu aokolewa akiwa hai siku sita baada ya tetemeko la ardhi Venezuela

Mvulana mwenye umri wa miaka mitatu ameokolewa akiwa hai kutoka chini ya vifusi siku sita baada ya matetemeko makubwa ya ardhi yaliyolikumba Venezuela, timu ya uokoaji kutoka Jordan imesema.

Mtoto huyo, aliyetambuliwa kwa jina la Klieber Morán, aliokolewa kutoka kwenye vifusi katika jimbo la La Guaira, kwa mujibu wa Rais wa mpito wa Venezuela, Delcy Rodríguez, ambaye alieleza uokoaji huo kuwa “chanzo cha matumaini kwa watu wetu.”

Tukio hilo limejiri huku Umoja wa Mataifa ukionya kwamba makumi ya maelfu ya watu wanahitaji kwa dharura chakula na makazi.

Idadi ya vifo kutokana na matetemeko ya ardhi ya wiki iliyopita, yaliyokuwa na ukubwa wa 7.2 na 7.5, imefikia watu 1,943, huku zaidi ya watu 10,000 wakijeruhiwa na makumi ya maelfu wengine wakiwa hawajulikani waliko.

Kwa mujibu wa tathmini ya awali ya data za satelaiti za NASA, matetemeko hayo huenda yaliharibu au kubomoa majengo 58,870.

Idara ya Ulinzi wa Raia ya Jordan ilisema Klieber alipatiwa huduma ya kwanza, akapelekwa hospitalini na hali yake ilikuwa nzuri. Anaendelea kupatiwa matibabu katika mji mkuu, Caracas.

Shirika la Umoja wa Mataifa la Kuhudumia Wakimbizi (UNHCR) lilisema upungufu wa chakula umeenea, huduma za msingi zimevurugika na mawasiliano mengi yamekatika katika jimbo la La Guaira.

“Mvutano ndani ya jamii unaongezeka huku upatikanaji wa misaada ukiendelea kuwa mgumu,” UNHCR ilisema katika taarifa yake.

Bilionea wa China ahukumiwa miaka 30 jela Marekani kwa ulaghai wa dola bilioni moja

Guo Wengui, ambaye wakati mmoja aliaminika kuwa miongoni mwa watu matajiri zaidi nchini China, amehukumiwa kifungo cha miaka 30 jela nchini Marekani kwa kuendesha ulaghai wa zaidi ya dola bilioni moja.

Bilionea huyo wa zamani wa sekta ya mali isiyohamishika alikimbilia Marekani mwaka 2017, ambako alijijenga upya kama mkosoaji wa Chama cha Kikomunisti cha China na kupata wafuasi wengi mtandaoni.

Hata hivyo, baadaye alipatikana na hatia ya makosa ya uhalifu wa kupangwa, ulaghai na utakatishaji fedha.

Jaji wa New York, Analisa Torres, alisema Guo aliwalaghai watu waliokuwa wakitafuta kuleta demokrasia nchini China na kutumia fedha zao kugharimia maisha yake ya anasa.

Wakili wake, Melinda Sarafa, alisema hukumu hiyo ni kali kupita kiasi na haikuzingatia maelfu ya wawekezaji wake ambao wanasema hawakulaghaiwa.

Guo amesisitiza kuwa hana hatia na atakata rufaa dhidi ya hukumu na adhabu hiyo.

Mwanasheria wa serikali ya Marekani, Sean Buckley, amesema:

“Hukumu ya leo inaonyesha kuwa umaarufu na utajiri haviweki mtu juu ya sheria, na walaghai wanaowaathiri wengine ili kujinufaisha watakabiliwa na madhara makubwa.”

Kabla ya kuondoka China, Guo alijijengea utajiri mkubwa kupitia biashara za mali isiyohamishika na alikuwa na uhusiano mzuri na serikali ya China.

Hata hivyo, aliomba hifadhi nchini Marekani baada ya kutuhumiwa na maafisa waandamizi wa China kwa ufisadi.

Iran yasema inapendelea mazungumzo, lakini iko tayari kwa vita pia



Mazungumzo ya kidiplomasia kati ya Iran na Marekani yanaendelea huku Iran ikisisitiza kuwa, pamoja na kuipa kipaumbele njia ya mazungumzo, bado iko tayari kurejea vitani ikiwa juhudi hizo zitashindwa.

Hayo yameelezwa na mpatanishi mkuu wa upande wa Iran, Mohammad Bagher Ghalibaf, ambaye alisema katika mahojiano na televisheni ya taifa kuwa Tehran haitaacha kujilinda iwapo mazungumzo hayatatoa matokeo.

“Tunafuata njia ya mazungumzo, lakini ikiwa mazungumzo hayatatekelezwa, pia tuko tayari kwa vita na tutajibu ipasavyo,” alisema Ghalibaf.

Kauli hiyo ilitolewa wakati wajumbe wa Iran na Marekani walipokuwa wakitarajiwa kufanya mazungumzo mengine mjini Doha, yakilenga kupunguza mvutano na kutafuta suluhu ya kudumu ya mgogoro uliodumu kwa miezi kadhaa.

Mvutano huo uliongezeka mwezi Juni 2026, baada ya mashambulizi ya kijeshi kati ya Iran na Israel, yaliyohusisha pia mashambulizi ya Marekani dhidi ya baadhi ya maeneo ya nyuklia ya Iran. Baada ya siku kadhaa za mapigano, pande husika zilikubaliana kusitisha mapigano kwa muda ili kutoa nafasi kwa juhudi za kidiplomasia.

Ingawa mapigano yamesitishwa kwa sasa, bado hakuna makubaliano ya kudumu yaliyofikiwa.

Amnesty International yasema RSF ilitenda uhalifu dhidi ya ubinadamu nchini Sudan

"Zaidi ya watu 6,000 waliuawa mjini El Fasher mwaka jana, kwa mujibu wa Umoja wa Mataifa."

Kundi la kutetea haki za binadamu limesema kuwa wanamgambo wa Sudan walifanya uhalifu dhidi ya ubinadamu na utakasaji wa kikabila wakati wa kampeni yao ya kuuteka mji wa El-Fasher mwaka jana.

Kuzingirwa na kutekwa kwa mji huo ulioko katika eneo la magharibi la Darfur kulikuwa miongoni mwa matukio mabaya zaidi ya umwagaji damu katika vita vya wenyewe kwa wenyewe nchini Sudan, vinavyopiganwa kati ya jeshi la Sudan na kikosi cha Rapid Support Forces (RSF).

Katika ripoti ya uchunguzi iliyotolewa Jumatano, Amnesty International ilisema:

“Uhalifu uliofanywa na RSF ulijumuisha mauaji, kuwahamisha watu kwa nguvu, kuwafunga bila sababu za kisheria, mateso, ubakaji, utumwa wa kingono, aina nyingine za ukatili wa kingono, utumwa, mauaji ya halaiki, na mateso kwa misingi ya utambulisho.”

RSF haijasema chochote kuhusu ripoti hiyo ya Amnesty, lakini hapo awali ilikanusha tuhuma kama hizo.

Sudan bado imo katika mapambano ya madaraka yaliyodumu kwa miaka mitatu kati ya jeshi la kawaida la nchi hiyo na wanamgambo wa RSF. Vita hivyo vimeua mamia ya maelfu ya watu na kuwalazimisha zaidi ya watu milioni 14 kuyakimbia makazi yao.

Kwa mujibu wa Umoja wa Mataifa, ukatili wa kingono dhidi ya wanaume, wanawake na watoto unatumiwa kama silaha ya vita.

Pande zote mbili, RSF na Sudanese Armed Forces (SAF) zimeshutumiwa kwa kufanya uhalifu wa kivita, ingawa zote zimekanusha tuhuma hizo.

Baada ya kufukuzwa kutoka mji mkuu, Khartoum, mwezi Machi mwaka jana, RSF ilielekeza nguvu zake katika kuimarisha udhibiti wake wa eneo la magharibi la Darfur kwa kuuteka mji wa El Fasher, pamoja na kupanua ushawishi wake katika majimbo ya Kordofan yaliyoko kusini mwa nchi.

Chris Brown aamriwa kumlipa mfanyakazi wake wa nyumbani dola milioni 13 baada ya kushambuliwa na mbwa

Brown

Mwimbaji wa Marekani Chris Brown amepatikana na hatia na kutakiwa kuwajibika kisheria kwa shambulio la mbwa lililomjeruhi vibaya na kumwacha mfanyakazi wake wa nyumbani akiwa na ulemavu wa kudumu nyumbani kwake mwaka 2020.

Baada ya kesi iliyodumu kwa wiki mbili mjini Los Angeles, jopo la majaji lilitoa uamuzi kwa manufaa ya Maria Avila, ambaye alishambuliwa na mbwa aina ya Caucasian Shepherd mwenye uzito wa takriban kilo 90, anayemilikiwa na Brown, alipokuwa akimwaga taka nyumbani kwake eneo la Tarzana.

Brown pamoja na kampuni yake, Black Pyramid LLC, sasa wanatakiwa kumlipa Avila fidia ya dola za Marekani milioni 12.9 kutokana na uzembe, kwa mujibu wa chapisho la Marekani Billboard.

BBC News imewasiliana na wawakilishi wa Brown ili kupata maoni yao kuhusu uamuzi huo.

Avila alisema mbwa huyo, anayeitwa Hades, alimnyofoa vipande vikubwa vya ngozi yake, jambo lililosababisha uharibifu wa kudumu wa uso, makovu, kupoteza uwezo wa kuona kwa kiwango fulani na kuharibika kwa mishipa ya fahamu.

Brown alidai kuwa mbwa huyo alikuwa akifugwa kwa madhumuni ya ulinzi wa nyumba na hakuwa mnyama wake wa kufugwa binafsi.

Wakati wa kesi hiyo, mahakama ilisikia ushahidi ulioonesha kuwa badala ya kupiga simu kwa huduma za dharura au kumsaidia Avila mwenyewe baada ya shambulio, Brown aliondoka eneo la tukio, kwa mujibu wa Rolling Stone.

Majaji pia walielezwa kuwa Brown aliwaacha wafanyakazi wake wamuhudumie Avila, akisema aliogopa kuwapo kwake au sauti yake kusikika kwenye simu ya dharura ya 911 kungesababisha “msisimko mkubwa wa vyombo vya habari” polisi walipowasili.

Chris Brown alisema alikuwa anajiandaa kuoga alipomsikia mbwa akinguruma, ndipo akashuka chini na kumkuta Maria Avila akiwa amelala bila kutikisika na akiwa ametapakaa damu nyingi.

“Kuona damu nyingi kulinishtua sana,” alisema, akiongeza kuwa alikuwa katika hali ya mshtuko alipoamua kufuata ushauri wa meneja wake wa kuondoka eneo la tukio kabla ya wahudumu wa dharura kufika.

Brown alikiri kuwa alikuwa na sehemu ya kuwajibika kabla ya kesi kuanza, lakini alipinga kiwango cha majeraha aliyopata Avila na kudai kuwa Avila pia alikuwa na mchango katika kutokea kwa tukio hilo.

Mwimbaji huyo alisema alikuwa amewaonya dada hao wawili waliokuwa wafanyakazi wa nyumbani kuwa mbwa hao “hawakuwa kabisa wa kirafiki”, na aliwaambia watoke nje ya nyumba tu pale walinzi walipokuwa wamefika.

Hata hivyo, wafanyakazi hao wawili walikanusha kuwa kuliwahi kufanyika mazungumzo kati yao na Brown, wakisema pia kuwa tofauti ya lugha ilifanya mazungumzo ya aina hiyo kuwa kutofanyika kwa urahisi.

Amnesty International yasema RSF ilitenda uhalifu dhidi ya ubinadamu nchini Sudan

"Zaidi ya watu 6,000 waliuawa mjini El Fasher mwaka jana, kwa mujibu wa Umoja wa Mataifa."

Kundi la kutetea haki za binadamu limesema kuwa wanamgambo wa Sudan walifanya uhalifu dhidi ya ubinadamu na utakasaji wa kikabila wakati wa kampeni yao ya kuuteka mji wa El-Fasher mwaka jana.

Kuzingirwa na kutekwa kwa mji huo ulioko katika eneo la magharibi la Darfur kulikuwa miongoni mwa matukio mabaya zaidi ya umwagaji damu katika vita vya wenyewe kwa wenyewe nchini Sudan, vinavyopiganwa kati ya jeshi la Sudan na kikosi cha Rapid Support Forces (RSF).

Katika ripoti ya uchunguzi iliyotolewa Jumatano, Amnesty International ilisema:

“Uhalifu uliofanywa na RSF ulijumuisha mauaji, kuwahamisha watu kwa nguvu, kuwafunga bila sababu za kisheria, mateso, ubakaji, utumwa wa kingono, aina nyingine za ukatili wa kingono, utumwa, mauaji ya halaiki, na mateso kwa misingi ya utambulisho.”

RSF haijasema chochote kuhusu ripoti hiyo ya Amnesty, lakini hapo awali ilikanusha tuhuma kama hizo.

Sudan bado imo katika mapambano ya madaraka yaliyodumu kwa miaka mitatu kati ya jeshi la kawaida la nchi hiyo na wanamgambo wa RSF. Vita hivyo vimeua mamia ya maelfu ya watu na kuwalazimisha zaidi ya watu milioni 14 kuyakimbia makazi yao.

Kwa mujibu wa Umoja wa Mataifa, ukatili wa kingono dhidi ya wanaume, wanawake na watoto unatumiwa kama silaha ya vita.

Pande zote mbili, RSF na Sudanese Armed Forces (SAF) zimeshutumiwa kwa kufanya uhalifu wa kivita, ingawa zote zimekanusha tuhuma hizo.

Baada ya kufukuzwa kutoka mji mkuu, Khartoum, mwezi Machi mwaka jana, RSF ilielekeza nguvu zake katika kuimarisha udhibiti wake wa eneo la magharibi la Darfur kwa kuuteka mji wa El Fasher, pamoja na kupanua ushawishi wake katika majimbo ya Kordofan yaliyoko kusini mwa nchi.

afghanistanafricaalbaniaalgeriaAmericaamerican-samoaandorraangolaanguillaantarcticaantigua-and-barbudaargentinaarmeniaarubaarushaaustraliaaustriaazerbaijanbahamasbahrainbangladeshbarbadosbelarusBelgiumbelizebeninbermudabhutanboliviabosnia-and-herzegovinabotswanaBoukinafasobrazilbrunei-darussalambulgariaburkina-fasoburmaburundicaliforniacambodiacamerooncanadacape-verdecayman-islandscentral-african-republicChadchicagochilechinachristmas-islandcocos-keeling-islandscolombiacomoroscongocook-islandscosta-ricacote-divoire-ivory-coastCroatiacubacyprusczech-republicdarsalaamdemocratic-peoples-rep-north-koreademocratic-republic-of-the-congo-kinshasadenmarkdjiboutidodomadominicadominican-republicdr-congodubaieast-timor-timor-lesteecuadoregyptegyptyel-salvadorenglandequatorial-guineaequitorial-guineaeritreaestoniaeswatiniethiopiafalkland-islandsfaroe-islandsfederal-states-of-moldovafijifinlandFloridafrancefrench-guianafrench-polynesiafrench-southern-territoriesgabongazageorgiagermanyghanagibraltargomaGreecegreenlandgrenadaguadeloupeguamguatemalaguineaguinea-bissauguyanahabarihaitiholy-seehondurashong-konghoustonhungaryicelandindiaindonesiaIowairaniran-islamic-republic-ofiraqirelandisraelitaliaitalyivory-coastjamaicajapanjordankaratukazakhstankilimanjarokinshasakiribatikiswahilikoreakosovokuwaitkyrgyzstanlaolatvia-lebanon-lesotho-liberia-libya-liechtenstein-lithuania-luxembourgLebanonliberiamacaumadagascarmalawimalaysia-maldivesMalimaltamarshall-islands-martinique-mauritania-mauritiusmassechutesmayottemazingirambeyamerumexicomiamimicronesiamonaco-mongolia-montenegromontserratmoroccomozambique-myanmarmtwaramwanzanamibianaurunepalnetherlandsnetherlands-antillesnevadanew-caledonianew-zealandnewyorknicaraguanigernigerianiuenorth-macedonianorthern-mariana-islandsnorwayomanpakistanpalaupalestinepalestinian-territoriespanamapapua-new-guineaparaguaypeoples-democratic-republicperuphiladhephiaphilipiansPhilippinespitcairn-islandpolandpoliticsPortugalpuerto-ricoqatarrepublic-ofrepublic-of-brazzavillerepublic-of-south-koreareunion-islandromaniaRussiarussian-federationrwandasahara-occidentalsaint-kitts-and-nevissaint-luciasaint-vincent-and-the-grenadinessamoasan-marinosao-tome-and-principesaudi-arabiasaudiarabiascotlandSenegalserbiaseychellessierra-leoneSingaporesingidaslovakia-slovak-republicsloveniasolomon-islandssomaliasouthafricaspainsri-lankasudansurinameswaziland-eswatiniswedenswitzerlandsyriasyrian-arab-republictaborataiwan-republic-of-chinatajikistantanzaniatexasthailandthe-gambiatibettimor-leste-east-timortogotokelautongatorontotrinidad-and-tobagotunisiaturkeyturkmenistanturks-and-caicos-islandstuvaluugandaunited-arabs-emiratesunited-kingdomunited-statesuruguayuzbekistanvancovervanuatuvatican-city-state-holy-seevenezuelavietnamvirgin-islands-britishvirgin-islands-u-swallis-and-futuna-islandswallis-and-futuna-islandswallis-et-futunawashington-dcwestern-saharayemenzambiazambiezimbabwe

CantonaDigital
CantonaDigital

Listen Live Radio Fortune Africa
Ukweli Na Burudani.

-Be ready to be Impacted, Inspired & Empowered.

-Keep watching our Channels

Cantona Cast Television,

Fortune Television Network (FTN)

Donation
Paypal https://www.paypal.com/donate/?hosted_button_id=6EKXMLNW8W6A2&fbclid=IwY2xjawQxeChleHRuA2FlbQIxMABicmlkETFRdkNBRndpclRDQTB5bXZZc3J0YwZhcHBfaWQQMjIyMDM5MTc4ODIwMDg5MgABHq960uGsyU3ABRIBc2h-iXGhHATvuEqe55gFsQ-rDb0fT-Z7SIQ3TV8LnkpD_aem_ybU2SvBlvyqrVsS9NAczRw

An attitude determines an altitude.

All Rights Reserved © Cantona Group PLC||2025

5,557 posts
0 followers

Fediverse Followers


Discover more from Cantona. Digital

Subscribe to get the latest posts sent to your email.

Leave a Reply

About us

Welcome to Cantona Group PLC-Where media meets moments.

Cantona Group PLC is a Premier Multi Media Group, where we connect live Broadcasting with world-class Production. We break the latest news in real-time, shape public perception, and produce captivating audio-visual content all under one roof.

Discover more from Cantona. Digital

Subscribe now to keep reading and get access to the full archive.

Continue reading

Discover more from Cantona. Digital

Subscribe now to keep reading and get access to the full archive.

Continue reading