Waathirika wa vita Sudan watafuta haki Kenya

https://zeno.fm/radio/radio-fortune-africa

Na Cantona Joseph 10, 2026 06:00 (EAT)

Vocalize Pre-Player Loader

Wanamgambo wa RSF wakiwa katika operesheni zake, El-Fasher Sudan.Picha: Rapid Support Forces (RSF)/AFP

Waathirika wa ukatili wa RSF Sudan wamewasilisha malalamiko Kenya, wakidai mateso makali na ukatili wa kingono.

Waathirika 12  wa ukatili unaodaiwa kufanywa katika vita vya Sudan wamefikisha malalamiko nchini Kenya wakitaka uchunguzi dhidi ya wanamgambo wa RSF.

Malalamiko hayo, yaliyowasilishwa na shirika la kimataifa Legal Action Worldwide, yanadai mateso na ukatili wa kingono uliofanywa na RSF katika maeneo ya Khartoum kati ya Aprili 2023 na Machi 2025, kipindi ambacho mji mkuu ulikuwa chini ya wanamgambo hao.

Waathiriwa wanamtaka Mkurugenzi wa Mashtaka Kenya kuidhinisha mashitaka dhidi ya wanachama 10 wa RSF, baadhi yao wakiaminika kuishi Kenya.

Aidha wanadai kwamba walishikiliwa katika mazingira ya kinyama, wakipigwa, kuchomwa, kunyimwa chakula na maji, kuteswa kwa umeme na kubakwa. Baadhi walilazimishwa kubeba miili ya waliouawa.

Shirika hilo linataka Kenya kutumia Sheria ya Uhalifu wa Kimataifa ya 2008, likisema Sudan haiwezi kutoa haki kwa sasa. RSF, iliyoibuka kutoka wanamgambo wa Janjaweed, imekuwa ikituhumiwa na mashirika ya haki za binadamu na Umoja wa Mataifa kwa uhalifu wa kivita, hasa Darfur.

CantonaDigital
CantonaDigital

Listen Live Radio Fortune Africa
Ukweli Na Burudani.

-Be ready to be Impacted, Inspired & Empowered.

-Keep watching our Channels

Cantona Cast Television,

Fortune Television Network (FTN)

Donation
Paypal https://www.paypal.com/donate/?hosted_button_id=6EKXMLNW8W6A2&fbclid=IwY2xjawQxeChleHRuA2FlbQIxMABicmlkETFRdkNBRndpclRDQTB5bXZZc3J0YwZhcHBfaWQQMjIyMDM5MTc4ODIwMDg5MgABHq960uGsyU3ABRIBc2h-iXGhHATvuEqe55gFsQ-rDb0fT-Z7SIQ3TV8LnkpD_aem_ybU2SvBlvyqrVsS9NAczRw

An attitude determines an altitude.

All Rights Reserved © The Cantona Group PLC||2025

5,411 posts
0 followers

Fediverse Followers


Discover more from cantonadigital

Subscribe to get the latest posts sent to your email.

Leave a Reply