Radio Fortune Africa -Ukweli na Burudani
https://zeno.fm/radio/radio-fortune-africa


Sudan yakanusha kutumia silaha za kemikali Picha: John Thys/AFP
Na:Cantona Joseph|RFA
Ripoti za vyombo vya habari zilizotolewa leo, zinaonyesha kuwa jeshi la Sudan lilitumia gesi ya klorini katika mashambulizi mawili mwaka 2024, kaskazini mwa mji mkuu, Khartoum.
Mwezi Juni, Marekani iliweka vikwazo kwa serikali ya Sudan inayoshirikiana na jeshi kutokana na matumizi ya silaha za kemikali, lakini haikufafanua wapi na lini walizitumia.
Uchunguzi uliofanywa na Shirika la habari la France24, umeonyesha kuwa jeshi linaonekana kudondosha mapipa mawili yenye klorini Septemba 2024 karibu na kiwanda cha mafuta cha Al-Jaili kaskazini mwa Khartoum.
Shirika la kimataifa la kutetea haki za binaadamu la Human Rights Watch limesema matumizi ya kemikali ya viwandani kama silaha, yanasababisha hali ya wasiwasi.
Sudan imerudia kukanusha madai ya Marekani, ikiyaita ”yasiyo na msingi” na ”kitisho cha kisiasa”.
All Rights Reserved © The Cantona Group PLC||2025
Discover more from cantonadigital
Subscribe to get the latest posts sent to your email.