Radio Fortune Africa -Ukweli na Burudani
https://zeno.fm/radio/radio-fortune-africa

Na: Cantona Joseph|RFA

Picha: UNICEF/Xinhua/picture alliance
Kundi la uangalizi wa njaa duniani IPC limesema kuwa maeneo mawili ya Sudan yanakabiliwa na njaa ambayo iko kwenye hatari ya kuenea katika maeneo mengine ya nchi hiyo.
IPC inasema kuna njaa katika eneo la El-Fasher huko magharibi mwa Darfur na katika mji wa Kadugli ulioko katika mkoa wa South Kordofan.
Hayo yakiarifiwa watu saba wameuwawa katika shambulizi la droni lililofanywa katika hospitali ya watoto nchini Sudan.
Haya ni kwa mujibu wa madaktari katika taifa hilo lililozongwa na mapigano. Wanawake na watoto ni miongoni mwa waliouwawa kwenye shambulizi hilo lililofanywa eneo la Kernoi karibu kilomita 270 kutoka mji wa El-Fasher katika eneo la Darfur.
Wakati huo huo, mahakama ya Kimataifa ya Jinai, ICC, imeonya kuwa ukatili unaofanywa huko El-Fasher, unaweza kuwa uhalifu dhidi ya binadamu na uhalifu wa kivita.
ICC imeyasema haya baada ya Umoja wa Mataifa kudai kuwa maelfu ya watu wamelikimbia eneo jirani na El-Fasher ambalo limetekwa na wanamgambo wa RSF kwa sasa.
All Rights Reserved © The Cantona Group PLC||2025
Discover more from cantonadigital
Subscribe to get the latest posts sent to your email.