
https://zeno.fm/radio/radio-fortune-africa
Na Cantona Joseph June 12, 2026 06:28 (EAT)


Raul Jimenez akifunga bao la pili kwa timu yake ya MexicoPicha: Raquel Cunha/REUTERS
Mexico imefanikiwa kufikisha mwisho laana ya mechi za ufunguzi wa kombe la dunia kwa kuishinda Afrika Kusini mabao 2-0 katika mechi ya ufunguzi ,

Mexico imefanikiwa kufikisha mwisho laana ya mechi za ufunguzi wa kombe la dunia kwa kuishinda Afrika Kusini mabao 2-0 katika mechi iliyojaa matukio ya ufunguzi wa Kombe la Dunia 2026 katika uwanja wa Estadio Azteca Alhamisi, na kuanza toleo kubwa zaidi kuwahi kutokea la tamasha la soka duniani.

Kocha wa Mexico Javier Aguirre amefichua kwamba timu yake ilikuwa imeshinda hofu ya jukwaani kabla ya kupata ushindi wao wa kwanza katika mchezo wa ufunguzi wa Kombe la Dunia.
Mexico ilikuwa haijawahi kushinda mchezo wao wa ufunguzi wa Kombe la Dunia katika majaribio saba, ikipoteza michezo mitano na kupata sare mbili wakati wa mechi zao za awali kwenye mashindano. Mchezo mwingine wa kundi wa A kati ya Korea Kusini na Jamhuri ya Czech unaendelea.
Baadaye mwenyeji mwenza Canada ina miadi na Bosnia Herzegovina katika pambano la kundi B ambalo beki wa klabu ya Bayern Alfonso Davies atalikosa. Kocha wa Kanada Jesse Marsch amsema Davies bado hajapona kikamilifu kutokana na jeraha la paja.

Discover more from cantonadigital
Subscribe to get the latest posts sent to your email.