
https://zeno.fm/radio/radio-fortune-africa
Na Cantona Joseph Imechapishwa : March 31, 2026 13:00 (EAT)

Jarida la Wall Street linaripoti kuwa Trump anafikiria kukomesha mapigano ya sasa, baada ya kile anachodai kudhoofisha jeshi la wanamaji la Iran na hifadhi ya makombora ya taifa hilo.

Jarida la Wall Street Journal linaripoti kuwa Rais wa Marekano Donald Trump amewaambia wasaidizi wake kuwa yuko tayari kusitisha operesheni ya kijeshi dhidi ya Iran hata kama Mlango wa bahari wa Hormuz utaendelea kufungwa.
Likiwanukuu maafisa wa utawala, jarida hilo linaripoti kuwa Trump na wasaidizi wake walihofia kwamba wazo la kutumia nguvu kufungua njia kuu ya baharini litarefusha mzozo huo zaidi ya muda wake wa wiki nne hadi sita.
Badala yake, anaripotiwa kufikiria kukomesha mapigano ya sasa, akiwa ameharibu pakubwa jeshi la wanamaji la Iran na hifadhi ya makombora, na ataendelea kuishinikiza Iran kidiplomasia kufungua tena mkondo huo wa biashara.
Israel yapitisha sheria inayotoa adhabu ya kifo kwa Wapalestina watakaofanya mauaji dhidi ya Waisraeli

Bunge la Israel limepitisha sheria mpya inayotoa adhabu ya kifo kwa Wapalestina watakaopatikana na hatia ya mashambulizi ya mauaji dhidi ya Waisrael.
Sheria hiyo ilipitishwa kwa kura 62 dhidi ya 48, huku mbunge mmoja akijizuia kupiga kura na wengine kutohudhuria kikao hicho. Waziri Mkuu Benjamin Netanyahu alihudhuria binafsi kupiga kura kuunga mkono muswada huo bungeni.
Muswada huo wa sheria uliwasilishwa na Waziri wa Usalama wa Taifa Itamar Ben Gvir, ambaye ni mmoja wa wanasiasa wenye msimamo mkali nchini humo.
Hatua hiyo imeibua mjadala mkubwa kimataifa, huku mataifa ya Umoja wa Ulaya na mashirika ya haki za binadamu yakielezea wasiwasi mkubwa.
Muda mfupi baada ya kupitishwa, kundi la haki za binadamu la Israel lilisema limewasilisha malalamiko katika Mahakama Kuu ya nchi hiyo.
Mamlaka ya Palestina ilitaja muswada huo “uhalifu wa kivita dhidi ya watu wa Palestina”, ikisema kuwa unakiuka Mkataba wa Geneva, Hata hivyo marekani imesema kwamba Israel in haki ya kutungu sheria zake huku nchi zikiwemo Ujerumani, Ufaransa, Italia na Uingereza zikielezea wasiwasi mkubwa kuhusu muswada huo.
Siku ya 32 bila mtandao Iran, mawasiliano yashuka hadi 1%

Iran imeingia siku ya 32 tangu kukatika kwa mtandao, huku watumiaji wengi wakikosa mawasiliano nje ya mtandao kwa zaidi ya saa 744, kwa mujibu wa taasisi ya ufuatiliaji wa mtandao, NetBlocks.
Inaelezwa kuwa kiwango cha mawasiliano ya intaneti na mataifa ya nje kimesalia kwenye asilimia 1 tu ya hali ya kawaida.
Hata hivyo, baadhi ya maafisa wa serikali, watumiaji wanaoiunga mkono serikali pamoja na baadhi ya waandishi wa habari bado wana uwezo wa kutumia mtandao bila vikwazo, wakati wengine wakilazimika kulipa fedha nyingi ili kuweza kupata huduma hiyo.
Watu wachache wamefanikiwa kuunganisha mtandao kwa kutumia huduma za intaneti ya satelaiti kama Starlink na njia nyingine, lakini gharama zake ni kubwa.
Nchini Iran, kutumia au kumiliki huduma ya Starlink kunaweza kusababisha kifungo cha hadi miaka miwili gerezani, huku mamlaka zikiongeza juhudi za kukabiliana na matumizi yake.
Wanajeshi wanne wa Israel wauawa kusini mwa Lebanon

Wanajeshi wanne wa Israel waliuawa na wawili kujeruhiwa siku ya Jumatatu, katika taarifa mpya iliyochapishwa katika mtandao wa Telegram.
Kulingana na taarifa hiyo, Kapteni Noam Madmoni, 22, sajenti Ben Cohen, 21, sajenti Maxsim Entis, 22, waliuawa wakati wa mapigano kusini mwa Lebanon.
Maafisa wawili pia wamepelekwa hospitalini – askari mmoja alitajwa kama “aliyejeruhiwa vibaya”, na mwengine kwa kiasi”.
IDF inaongeza kuwa askari wa nne aliuawa katika tukio hilo hilo, lakini jina lake bado halijatumbuliwa ili kuchapishwa.
All Rights Reserved © The Cantona Group PLC||2026
afghanistan, africa, albania, algeria, America, american-samoa, andorra, angola, anguilla, antarctica, antigua-and-barbuda, argentina, armenia, aruba, arusha, australia, austria, azerbaijan, bahamas, bahrain, bangladesh, barbados, belarus, Belgium, belize, benin, bermuda, bhutan, bolivia, bosnia-and-herzegovina, botswana, Boukinafaso, brazil, brunei-darussalam, bulgaria, burkina-faso, burma, burundi, california, cambodia, cameroon, canada, cape-verde, cayman-islands, central-african-republic, Chad, chicago, chile, china, christmas-island, cocos-keeling-islands, colombia, comoros, congo, cook-islands, costa-rica, cote-divoire-ivory-coast, Croatia, cuba, cyprus, czech-republic, darsalaam, democratic-peoples-rep-north-korea, democratic-republic-of-the-congo-kinshasa, denmark, djibouti, dodoma, dominica, dominican-republic, dr-congo, dubai, east-timor-timor-leste, ecuador, egypt, egypty, el-salvador, england, equatorial-guinea, equitorial-guinea, eritrea, estonia, eswatini, ethiopia, falkland-islands, faroe-islands, federal-states-of-moldova, fiji, finland, Florida, france, french-guiana, french-polynesia, french-southern-territories, gabon, gaza, georgia, germany, ghana, gibraltar, goma, Greece, greenland, grenada, guadeloupe, guam, guatemala, guinea, guinea-bissau, guyana, habari, haiti, holy-see, honduras, hong-kong, houston, hungary, iceland, india, indonesia, Iowa, iran, iran-islamic-republic-of, iraq, ireland, israel, italia, italy, ivory-coast, jamaica, japan, jordan, karatu, kazakhstan, kilimanjaro, kinshasa, kiribati, kiswahili, korea, kosovo, kuwait, kyrgyzstan, lao, latvia-lebanon-lesotho-liberia-libya-liechtenstein-lithuania-luxembourg, Lebanon, liberia, macau, madagascar, malawi, malaysia-maldives, Mali, malta, marshall-islands-martinique-mauritania-mauritius, massechutes, mayotte, mazingira, mbeya, meru, mexico, miami, micronesia, monaco-mongolia-montenegro, montserrat, morocco, mozambique-myanmar, mtwara, mwanza, namibia, nauru, nepal, netherlands, netherlands-antilles, nevada, new-caledonia, new-zealand, newyork, nicaragua, niger, nigeria, niue, north-macedonia, northern-mariana-islands, norway, oman, pakistan, palau, palestine, palestinian-territories, panama, papua-new-guinea, paraguay, peoples-democratic-republic, peru, philadhephia, philipians, Philippines, pitcairn-island, poland, politics, Portugal, puerto-rico, qatar, republic-of, republic-of-brazzaville, republic-of-south-korea, reunion-island, romania, Russia, russian-federation, rwanda, sahara-occidental, saint-kitts-and-nevis, saint-lucia, saint-vincent-and-the-grenadines, samoa, san-marino, sao-tome-and-principe, saudi-arabia, saudiarabia, scotland, Senegal, serbia, seychelles, sierra-leone, Singapore, singida, slovakia-slovak-republic, slovenia, solomon-islands, somalia, southafrica, spain, sri-lanka, sudan, suriname, swaziland-eswatini, sweden, switzerland, syria, syrian-arab-republic, tabora, taiwan-republic-of-china, tajikistan, tanzania, texas, thailand, the-gambia, tibet, timor-leste-east-timor, togo, tokelau, tonga, toronto, trinidad-and-tobago, tunisia, turkey, turkmenistan, turks-and-caicos-islands, tuvalu, uganda, united-arabs-emirates, united-kingdom, united-states, uruguay, uzbekistan, vancover, vanuatu, vatican-city-state-holy-see, venezuela, vietnam, virgin-islands-british, virgin-islands-u-s, wallis-and-futuna-islands, wallis-and-futuna-islands, wallis-et-futuna, washington-dc, western-sahara, yemen, zambia, zambie, zimbabwe
Discover more from cantonadigital
Subscribe to get the latest posts sent to your email.