Na Cantona Joseph Julai 03, 2026 08:40 (EAT

f

Spika wa Bunge la Iran na mpatanishi mkuu wa nchi hiyo, Mohammad Baqer Qalibaf, ametoa wito kwa Wairani kushiriki kwa wingi katika mazishi ya Kiongozi Mkuu wa zamani wa Iran, Ayatollah Ali Khamenei, akisema ushiriki huo utakuwa sehemu ya kulipiza kisasi kwa kifo chake.

Katika taarifa yake Alhamisi, Qalibaf alisema, “Ninawaomba wananchi wote wa Iran kuandika ukurasa wa kihistoria wa Iran ya Kiislamu kwa kushiriki katika mazishi ya Khamenei.”

Aliongeza kuwa, “Wito wa taifa wa kulipiza kisasi lazima usikike duniani kote.”

Baraza Kuu la Usalama wa Taifa la Iran limesema litachukua hatua za kulipiza kisasi kwa kifo cha Kiongozi Mkuu wa zamani wa nchi hiyo, Ayatollah Ali Khamenei.

Katika taarifa iliyotiwa saini na Katibu wa Baraza hilo, Mohammad Baqer Zolqadr, Iran imesema “kisasi kwa damu ya Ayatollah Ali Khamenei kitachukuliwa dhidi ya waliomuua.”

Khamenei aliuawa Februari 28 wakati wa siku ya kwanza ya mashambulizi ya Marekani na Israel dhidi ya Iran.

Wakati huo huo, msemaji wa Wizara ya Mambo ya Nje ya Pakistan ametangaza kuwa Waziri Mkuu wa Pakistan, Shehbaz Sharif, atashiriki katika shughuli za mazishi ya Khamenei zitakazoanza Jumamosi mjini Tehran.

Kwa mujibu wa BBC Persian, shughuli za mazishi ya Khamenei zitafanyika kati ya Julai 4 na 8 katika miji ya Tehran, Qom na Mashhad, huku mikutano ya maombolezo pia ikipangwa kufanyika katika miji ya Baghdad, Kazmin, Karbala na Najaf nchini Iraq.

LIVE |MATANGAZO YA ASUBUI | 03 07 2026 | *AWAMU YA TATU| 2026™* | RADIO FORTUNE AFRICA

https://www.youtube.com/live/cKMl9oUW7Eo?si=sEDAZu1nitW8qGrA

Jeneza la Khamenei lapelekwa katika msikiti wa Tehran

f

Jeneza la Kiongozi Mkuu wa zamani wa Iran, Ayatollah Ali Khamenei, pamoja na miili ya baadhi ya wanafamilia wake waliouawa katika shambulio la pamoja la Israel na Marekani la Machi 29, limepelekwa katika msikiti mmoja mjini Tehran.

Shirika la habari la ISNA limesema baadhi ya wageni wa kigeni waliowasili nchini Iran wametoa heshima zao kwa kuhudhuria ibada ya maombolezo mjini Tehran. Shughuli hizo zinatarajiwa kuendelea siku nzima.

Miongoni mwa viongozi waliowasili Tehran kuhudhuria shughuli hizo ni Waziri wa Mambo ya Ndani wa Pakistan, Mohsin Naqvi, na Waziri wa Mambo ya Nje wa Afghanistan chini ya utawala wa Taliban, Amir Khan Muttaqi.

Imeelezwa pia kuwa maafisa kutoka Tajikistan, China na India wanatarajiwa kushiriki katika shughuli hizo.

Baadhi ya wanafamilia wa Khamenei, akiwemo mkwe wake, mjukuu wake, mmoja wa mabinti zake na mke wa mwanawe Mojtaba Khamenei, waliuawa pamoja naye katika shambulio hilo.

Kwa mujibu wa ratiba iliyotangazwa na mamlaka za Iran, shughuli za kuaga na mazishi ya Khamenei zitafanyika kwa hatua kadhaa katika siku mfululizo.

Baada ya shughuli za maombolezo mjini Tehran na baadaye Qom, mazishi yake yanatarajiwa kufanyika mjini Mashhad Alhamisi ijayo. Kabla ya hapo, mwili wake pia unatarajiwa kupelekwa katika miji ya Najaf na Karbala nchini Iraq.

Moto wa nyika wazidi kusambaa kusini mwa Ufaransa, watu 3,000 wahamishwa

h

Moto mkubwa wa nyika unaoendelea kusambaa kusini mwa Ufaransa umesababisha karibu watu 3,000 kuhamishwa kutoka makazi yao, huku mamlaka zikionya kuhusu kuanza mapema kwa msimu wa moto kufuatia wimbi la joto kali lililovunja rekodi.

Kwa mujibu wa vituo vya habari nchini humo, watalii na wakazi wa maeneo ya Sainte Marie la Mer na Canet en Roussillon walilazimika kuondoka baada ya moto kuzuka katika eneo la kambi na kusambaa kwa kasi.

Moto huo umeharibu nyumba kadhaa za muda kabla ya kufika eneo la bandari, ambapo moshi mzito wenye sumu ulitanda juu ya boti na majengo ya karibu.

Kwa mujibu wa mamlaka za eneo hilo, moto mkubwa zaidi umeshuhudiwa katika maeneo ya Aude na Herault, ambapo zaidi ya ekari 900 za ardhi tayari zimeteketea.

Takriban wazima moto 800 na magari 150 ya zimamoto wametumwa kupambana na moto huo, huku juhudi za kuudhibiti zikiendelea.

Minyoo 38 yapatikana kwenye ubongo wa mwanamke baada ya kula nyama ya nguruwe India

h

Laurie Denman aligundua kwa mara ya kwanza kuwa kuna jambo lisilo la kawaida mwilini mwake baada ya kuona minyoo mrefu wa takriban mita moja alipoenda chooni.

“Ilikuwa ya kutisha sana. Ilifanana na utepe wenye mistari midogo midogo,” alisema Laurie, mwenye umri wa miaka 42 kutoka Wales.

Hilo lilikuwa ishara ya kwanza ya ugonjwa wa neurocysticercosis, hali iliyosababisha minyoo 38 kupatikana kwenye ubongo wake na kusababisha maumivu makali ya kichwa, degedege na matatizo ya kisaikolojia.

Laurie ni miongoni mwa watu wachache nchini Uingereza waliowahi kugundulika kuwa na maambukizi hayo ya ubongo, yanayosababishwa na mabuu ya minyoo ya nguruwe.

“Daktari aliniambia, tumeangalia picha za uchunguzi wako na tumegundua kuna minyoo 38 kwenye ubongo wako,” alisema Laurie.

“Mimi na mama yangu tulitazamana kwa mshangao, tukijiuliza ni kitu gani hiki.”

Mwanzoni, madaktari walidhani alikuwa na toxoplasmosis, maambukizi yanayoenezwa kupitia kugusana na kinyesi cha paka aliyeambukizwa.

Hata hivyo, mama yake aliwauliza madaktari kama hali hiyo inaweza kuwa inahusiana na minyoo aliyokuwa ameipata mwaka mmoja uliopita.

Baada ya uchunguzi zaidi, hatimaye aligundulika kuwa na ugonjwa wa neurocysticercosis.

Kwa mujibu wa Shirika la Afya Duniani (WHO), watu wanaweza kupata maambukizi hayo kwa kula nyama ya nguruwe mbichi au isiyopikwa vizuri, kunywa maji yaliyochafuliwa na mayai ya minyoo, au kutokana na tabia duni za usafi.

Ugonjwa huo ni nadra sana nchini Uingereza na visa vingi huonekana kwa watu waliotoka katika maeneo ambako ugonjwa huo ni wa kawaida.

Daktari Healy, ambaye alikuwa akimhudumia Laurie, alisema kuwa hiyo ndiyo ilikuwa kisa cha kwanza cha aina hiyo kukiona katika maisha yake yote ya taaluma.

Baada ya miaka kadhaa ya kupona, sasa anataka kutumia uzoefu wake kuhamasisha watu kuhusu ugonjwa huo.

Lissu afika Mahakama ya Rufani, marejeo ya kesi ya uhaini yasikilizwa leo

g

Mwenyekiti wa Chama cha Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA), Tundu Antipas Lissu, tayari amefika katika Mahakama ya Rufani jijini Dar es Salaam ambako mahakama hiyo inatarajiwa kusikiliza maombi ya marejeo yanayohusiana na kesi ya uhaini inayomkabili.

Mahakama hiyo inasikiliza maombi ya marejeo Na. 7440840/2026 katika shauri la Mkurugenzi wa Mashitaka (DPP) dhidi ya Tundu Lissu.

Maombi hayo yanasikilizwa na jopo la majaji watatu linaloundwa na Jaji Mwarija, Jaji Muruke na Jaji Khamis.

Shauri la msingi la kesi ya uhaini lilisimama kwa takriban miezi minne ili kupisha usikilizaji wa rufaa ya Jamhuri iliyopinga uamuzi wa Mahakama Kuu wa kutupilia mbali ombi lake la kuwasilisha ushahidi wa nyongeza kupitia shahidi wake, ACP Amini Mahamba.

Lissu alishtakiwa kwa kosa la uhaini mwezi Aprili 2025, miezi mitatu baada ya kuchaguliwa kuwa Mwenyekiti wa CHADEMA.

Upande wa mashtaka unadai alitoa kauli zilizolenga kuhamasisha wananchi kuzuia kufanyika kwa Uchaguzi Mkuu wa 2025.

Mahakama ya Rufani inatarajiwa kutoa mwelekeo kuhusu maombi hayo baada ya kusikiliza hoja za pande zote.

Katika picha: Hali ilivyo katika mahakama ya Rufani kabla ya kesi kuanzwa

CantonaDigital
CantonaDigital

Listen Live Radio Fortune Africa
Ukweli Na Burudani.

-Be ready to be Impacted, Inspired & Empowered.

-Keep watching our Channels

Cantona Cast Television,

Fortune Television Network (FTN)

Donation
Paypal https://www.paypal.com/donate/?hosted_button_id=6EKXMLNW8W6A2&fbclid=IwY2xjawQxeChleHRuA2FlbQIxMABicmlkETFRdkNBRndpclRDQTB5bXZZc3J0YwZhcHBfaWQQMjIyMDM5MTc4ODIwMDg5MgABHq960uGsyU3ABRIBc2h-iXGhHATvuEqe55gFsQ-rDb0fT-Z7SIQ3TV8LnkpD_aem_ybU2SvBlvyqrVsS9NAczRw

An attitude determines an altitude.

All Rights Reserved © Cantona Group PLC||2025

5,560 posts
0 followers

Fediverse Followers


Discover more from Cantona. Digital

Subscribe to get the latest posts sent to your email.

Leave a Reply

About us

Welcome to Cantona Group PLC-Where media meets moments.

Cantona Group PLC is a Premier Multi Media Group, where we connect live Broadcasting with world-class Production. We break the latest news in real-time, shape public perception, and produce captivating audio-visual content all under one roof.

Discover more from Cantona. Digital

Subscribe now to keep reading and get access to the full archive.

Continue reading

Discover more from Cantona. Digital

Subscribe now to keep reading and get access to the full archive.

Continue reading