Kinacho sababisha watu wasitimize malengo.

Dr. Joshua Grubbs (PhD) mtaalamu wa saikolojia alifanya utafiti katika chuo kikuu cha Western Reserve kutaka kujua…….sababu mojawapo inayochangia watu wasifisafinikiwe kutimiza Malengo waliyojiwekea.Moja ya sababu kubwa aliyoigundua ni hali ya kuwa “disappointed“.

Hii inatokea pale ambapo matarajio ya mtu yanapishana na uhalisia wa jambo.Kwa mujibu wa utafiti huu ilionesha kuwa “millennials”(Kizazi cha sasa) kinapata……changamoto kubwa sana katika eneo hili kwa sababu ya matarajio Makubwa……ya kutaka kuishi katika mazingira yaliyokamilika katika Kila Kitu.

“Dissapointment” hutokea pale ambapo unafanya biashara ukitarajia upate faida mara mbili……halafu unapata hasara na mtaji unapoteza.Unatarajia mahusiano uliyoanza yatakuwa na furaha sana lakini yanageuka kuwa mateso.

Unatarajia kwa 100% kupata kazi uliyoomba badala yake unaikosa.Unatarajia Kipaji chako kitaonekana kwa juhudi unayofanya lakini hakuna anayeona n.k

Njia 2 za kuishinda hali hii ni:

1. Kila wakati unapokuwa “disappointed” Kumbuka iko Njia nyingine ya kufanikiwa.Usikate tamaa kwa sababu ulichotarajia hakijatokea.

2. Usimchukie na kuendelea kumjadili “aliyekudisapoint”.UKifanya hivyo utaendelea kudumaa hapo ulipo na akili yako haitapiga hatua kwenda mbele.Leo kuna WATU na MAZINGIRA yatakudisapoint pia.Wakati Mwingine mambo hayo yatatokea asubuhi mapema kabisa.

USIKUBALI SIKU YAKO IHARIBIKE.


Discover more from cantonadigital

Subscribe to get the latest posts sent to your email.

Leave a comment