Takriban Wakorea Kaskazini 100 waliuawa’ katika vita vya Urusi na Ukraine

Radio Fortune Africa -Na Cantona Joseph

https://zeno.fm/radio/radio-fortune-africa

Takriban wanajeshi 100 wa Korea Kaskazini waliotumwa kupigana pamoja na vikosi vya Urusi dhidi ya Ukraine waliuawa kwenye uwanja wa vita mwezi Desemba, anasema mbunge wa Korea Kusini Lee Sung-kwon. 

Ukraine ilizindua mashambulizi ya kushtukiza katika eneo la Urusi la Kursk mwanzoni mwa mwezi Agosti, kubwa zaidi katika eneo la Urusi tangu Vita vya Pili vya Dunia. Bado inadhibiti sehemu ndogo ya eneo hili.
Ukraine ilizindua mashambulizi ya kushtukiza katika eneo la Urusi la Kursk mwanzoni mwa mwezi Agosti, kubwa zaidi katika eneo la Urusi tangu Vita vya Pili vya Dunia. Bado inadhibiti sehemu ndogo ya eneo hili. © Yan Dobronosov / Reuters

“Mnamo mwezi Desemba, walishiriki katika mapigano ya kweli, ambapo vifo vya angalau 100 vilitokea,” Mbunge Lee Seong-kweun amesema kuhusu wanajeshi wa Korea Kaskazini, baada ya taarifa fupi iliyotolewa na idara ya ujasusi (NIS) kwa wabunge huko Seoul.

“NIS pia imesema idadi ya waliojeruhiwa inatarajiwa kufikia karibu 1,000” kati ya wanajeshi wa Korea Kaskazini, Bw. Lee ameongeza.

Kulingana na Bw. Lee, kuna ripoti kwamba “hasara kadhaa za Korea Kaskazini, ikiwa ni pamoja na zile za maafisa wa ngazi za juu, zilitokea katika mashambulizi ya makombora ya Ukraine na ndege zisizo na rubani, pamoja na ajali za mafunzo.”

Kulingana na NIS, iliyonukuiwa na Bw. Lee, idadi kubwa ya waathiriwa inaweza kuelezewa na “mazingira yasiyojulikana ya uwanja wa vita, ambapo vikosi vya Korea Kaskazini vinatumiwa kama vitengo vya shambulio la mstari wa mbele ambavyo “tunaweza kujitolea, na kwa ukosefu wao uwezo wa kukabiliana na mashambulizi ya ndege zisizo na rubani.”

Mbunge huyo pia amebainisha “malalamiko kati ya jeshi la Urusi kwamba wanajeshi wa Korea Kaskazini, kwa sababu ya ukosefu wao wa maarifa kuhusu ndege zisizo na rubani, ni mzigo zaidi kuliko mali.”

Maelfu kadhaa ya wanajeshi wa Korea Kaskazini wametumwa Urusi katika wiki za hivi karibuni kusaidia jeshi la Urusi, kulingana na nchi za Magharibi.

Kwa upande wake, Kremlin kila wakati imekwepa maswali juu ya mada hiyo, bila kutaka kudhibitisha habari hii.

“Mashambulio makali”

Siku ya Jumanne, kamanda mkuu wa jeshi la Ukraine, Oleksandr Syrsky, alisema kwamba jeshi la Urusi lilikuwa likifanya “operesheni kali za kujibu katika mkoa wa Kursk, kwa kutumia vitengo vya jeshi la Korea Kaskazini,” na kuongeza kuwa tayari ” walipata hasara kubwa”.

Siku hiyo hiyo, afisa mkuu wa Marekani aliyezungumza kwa sharti la kutotajwa jina alikadiria hasara ya Korea Kaskazini kuwa “mamia kadhaa”, “kutoka kwa waliojeruhiwa kidogo hadi wale waliouawa katika mapigano”. Marekani na washirika wake walikuwa, tena siku ya Jumanne, wamelaani katika taarifa ya pamoja “kupanuka kwa hatari” kwa vita nchini Ukraine na kuitaka Korea Kaskazini kuwarejesha nyumbani wanajeshi wake.

Ukraine ilizindua mashambulizi ya kushtukiza katika eneo la Urusi la Kursk mwanzoni mwa mwezi Agosti, kubwa zaidi katika eneo la Urusi tangu Vita vya Pili vya Dunia. Bado inadhibiti sehemu ndogo ya eneo hili.

Korea Kaskazini haijawahi kuthibitisha au kukanusha kuwepo kwa wanajeshi wake pamoja na Urusi. Siku ya Alhamisi, hata hivyo, msemaji wa Wizara yake ya Mambo ya Nje alielezea ukosoaji wa Washington wa uungaji mkono wake kwa Moscow kama “chokozi zisizowajibika”.

Korea Kaskazini na Urusi zimeimarisha uhusiano wa kijeshi tangu mashambulizi ya Moscow nchini Ukraine mnamo mwezi wa Februari 2022.

Mkataba wa kihistoria wa ulinzi wa pande zote kati ya Pyongyang na Moscow, uliotiwa saini mwezi Juni, ulianza kutumika mapema mwezi huu. Unatoa “msaada wa kijeshi wa haraka” katika tukio la uvamizi wa silaha na nchi ya tatu.

All Rights Reserved © Cantona Group PLC||2024


Discover more from cantonadigital

Subscribe to get the latest posts sent to your email.

Leave a comment