
https://zeno.fm/radio/radio-fortune-africa
Na Cantona Joseph June 16, 2026 06:28 (EAT)

Marekani na Iran zimetia saini makubaliano ya awali ya kusitisha vita vya Ghuba, katika juhudi za kumaliza mzozo uliotikisa eneo hilo na kuathiri soko la nishati duniani.
Rais wa Marekani Donald Trump usiku wa kuamkia Jumanne kwa saa za Afrika Mashariki alisema kuwa makubaliano hayo tayari yamesainiwa, ingawa maelezo yake kamili bado hayajawekwa wazi na pande zote mbili zimesema mazungumzo zaidi yanahitajika kabla ya kufikiwa kwa mkataba wa kudumu wa amani.
Makubaliano hayo yanatarajiwa kuongeza siku 60 zaidi za usitishaji vita uliotangazwa mwezi Aprili na pia kufungua tena Mlango-Bahari wa Hormuz, ambao Iran imekuwa ikiuzuia tangu mashambulizi ya Marekani na Israel dhidi ya Iran mwezi Februari.
Masuala nyeti, ikiwemo mustakabali wa mpango wa nyuklia wa Iran, yanatarajiwa kujadiliwa katika hatua inayofuata ya mazungumzo.
“Makubaliano yamesainiwa kikamilifu,” alisema Trump baada ya kuwasili nchini Ufaransa kuhudhuria mkutano wa viongozi wa mataifa tajiri duniani wa G7.
Pamoja na kusema yametiwa saini Trump akaongeza Makamu wa Rais wa Marekani JD Vance anatarajiwa kuhudhuria hafla rasmi ya utiaji saini wa makubaliano hayo mjini Geneva, Uswisi, siku ya Ijumaa.
Habari za makubaliano hayo zilisababisha bei za mafuta duniani kushuka hadi kiwango cha chini zaidi tangu Machi 10, baada ya matarajio ya kufunguliwa tena kwa Mlango-Bahari wa Hormuz, njia muhimu inayopitisha karibu asilimia 20 ya biashara ya mafuta duniani.
Mkataba huo unachukuliwa kuwa hatua kubwa zaidi hadi sasa katika juhudi za kumaliza mzozo ambao umeua watu wasiopungua 7,000, wengi wao nchini Iran na Lebanon, huku pia ukiitikisa sekta ya nishati duniani.
Watu wanane wafariki baada ya ndege aina ya B-52 kuanguka Marekani

Watu wanane, wakiwemo wafanyakazi wawili wa Boeing, wameuawa baada ya ndege aina ya B-52 ya Jeshi la Anga la Marekani kuanguka mara tu baada ya kupaa kutoka Kituo cha Jeshi la Anga cha Edwards kusini mwa California.
Tukio hilo lilitokea saa 11:20 kwa saa za eneo (19:20 GMT) siku ya Jumatatu wakati ndege hiyo ilikuwa katika misheni ya kawaida ya majaribio. Ajali hiyo ilisababisha moshi mkubwa mweusi angani ambao ungeweza kuonekana umbali wa maili nyingi.
“Leo, Kituo cha Jeshi la Anga cha Edwards kilipata ajali mbaya, na tumewapoteza Wamarekani wanane mashuhuri,” Kanali James Hayes alisema, akiwaelezea kama “kikosi mchanganyiko cha wanajeshi, wafanyakazi na wakandarasi wa serikali”.
Awali, Kambi hiyo ilisema kwamba dalili za awali zinaonyesha kuwa ajali hiyo “haingeweza kunusurika”.
Ndugu wa karibu wa wafanyakazi wanaarifiwa na watatajwa baada ya saa 24, Hayes alisema katika mkutano wa alasiri.
Kituo hicho kimesitisha shughuli zake kwa muda.
Alisema ndege aina ya B-52 ilikuwa yenye muundo wa kisasa wa rada na ilianguka mara tu baada ya kupaa na kuwaka moto.
Baada ya kupitia video za awali, tukio hilo lilionekana kutokea “ajali isiyoweza kukingika,” Hayes alisema.
Mtoto wa Rais Jenerali Muhoozi ajisifia kwa kumkamata mpinzani Uganda

Mkuu wa majeshi ya Ulinzi nchini Uganda Jenerali Muhoozi siku ya Jumatatu alijisifu kwa kupanga kumsababishia “maumivu na uchungu” mwanasiasa wa upinzani ambaye amemkamata, aliyekuwa akijiandaa kuwasilisha pingamizi la kisheria dhidi yake.
Muhoozi Kainerugaba, mwana wa Rais aliyetawala kwa muda mrefu Yoweri Museveni, alichapisha picha kwenye mtandao wa X ya Erias Lukwago, mwanasiasa wa upinzani na wakili anayeshikiliwa na jeshi.
“Ninajivunia maumivu na uchungu WOTE nitakaoupata kwa LUKWAGO MHALIFU!” Kainerugaba alichapisha ujumbe huo kwa wafuasi wake milioni 1.3 kwenye mtandao wa X.
“Anaendelea kusema ‘Samahani, samahani’. Haitamsaidia kwa sasa,” aliandika kando ya picha ya Lukwago, akiwa amevaa fulana nyeupe.
Picha nyingine inaonyesha mwanamume aliyevaa nguo kama hiyo, kwenye mandhari kama hayo hayo, uso wake ukiwa umefunikwa kwa kitambaa na mikono ikiwa imeunganishwa kana kwamba anaomba dua.
Katika chapisho la awali kwenye mtandao wa X, Kainerugaba alisema “alimkamata mjinga na kumpeleka kwenye chumba cha chini ya ardhi”, lakini hakumtaja Lukwago.
Aliandika katika chapisho lingine: “aliniita?? Unathubutuje kutamka maneno hayo”, akiongeza: “mpumbavu huyu atajifunza kutokana na makosa yake”.
Kombe la Dunia 2026: Saudi Arabia walazimishwa sare na Uruguay

Saudi Arabia wamelazimishwa sare ya 1-1 na Uruguay waliosawazisha dakika ya 80 baada ya Saudia kuongoza dakika ya 41 ya mchezo huo uliopigwa usiku wa manane.
Mapema usiku wawakilishi wa Afrika Misri walitoshana nguvu na Ubelgiji kwa sare ya goli 1-1.
Misri waliongoza katika dakika ya 20 kupitia kwa Emam Ashour aliyeachia mkwaju mkali baada ya pasi safi ya Mohamed Salah.

Ubelgiji walisawazisha dakika ya 66 baada ya mlinzi wa kulia wa Misri Mohamed Hany kujifunga katika harakati za kuokoa.
Mapema zaidi, Cape Verde waliiwakilisha Afrika na kushangaza dunia baada ya kuonesha mbinu za hali ya juu za ulinzi na kutoka sare ya bila kufungana na Hispania ambao ni mabingwa wa dunia wa mwaka 2010 na mabingwa wa sasa wa Ulaya huku mlinda lango wa Cape Verde, Vozinha mwenye umri wa miaka 40 akijizolea sifa kemkem kwa umahiri wake.
Alibubujikwa na machozi baada ya kipenga cha mwisho.
Kombe ya Dunia 2026: Iran na New Zealand zatoshana nguvu

Mchuano kati ya Iran na New Zealand umekamilika kwa sare ya mabao 2-2.
New zealand walikuwa wa kwanza kugusa nyavu dakika ya 7 kupitia kwa Elijah Just.
Iran wakasawazisha dakika ya 32 kupitia kwa Ramin Rezaeian.
New Zealand wakaongoza tena dakika ya 54 kwa bao la Elijah Just tena, kisha Iran wakasawazisha tena dakika ya 64 kupitia kwa Mhammad Mohebi.
Sasa kuna ugumu wa kundi G kwani timu zote nne Iran New Zealand, Misri na Ubelgiji zote zina alama moja.
All Rights Reserved © Cantona Group PLC||2026
afghanistan, africa, albania, algeria, America, american-samoa, andorra, angola, anguilla, antarctica, antigua-and-barbuda, argentina, armenia, aruba, arusha, australia, austria, azerbaijan, bahamas, bahrain, bangladesh, barbados, belarus, Belgium, belize, benin, bermuda, bhutan, bolivia, bosnia-and-herzegovina, botswana, Boukinafaso, brazil, brunei-darussalam, bulgaria, burkina-faso, burma, burundi, california, cambodia, cameroon, canada, cape-verde, cayman-islands, central-african-republic, Chad, chicago, chile, china, christmas-island, cocos-keeling-islands, colombia, comoros, congo, cook-islands, costa-rica, cote-divoire-ivory-coast, Croatia, cuba, cyprus, czech-republic, darsalaam, democratic-peoples-rep-north-korea, democratic-republic-of-the-congo-kinshasa, denmark, djibouti, dodoma, dominica, dominican-republic, dr-congo, dubai, east-timor-timor-leste, ecuador, egypt, egypty, el-salvador, england, equatorial-guinea, equitorial-guinea, eritrea, estonia, eswatini, ethiopia, falkland-islands, faroe-islands, federal-states-of-moldova, fiji, finland, Florida, france, french-guiana, french-polynesia, french-southern-territories, gabon, gaza, georgia, germany, ghana, gibraltar, goma, Greece, greenland, grenada, guadeloupe, guam, guatemala, guinea, guinea-bissau, guyana, habari, haiti, holy-see, honduras, hong-kong, houston, hungary, iceland, india, indonesia, Iowa, iran, iran-islamic-republic-of, iraq, ireland, israel, italia, italy, ivory-coast, jamaica, japan, jordan, karatu, kazakhstan, kilimanjaro, kinshasa, kiribati, kiswahili, korea, kosovo, kuwait, kyrgyzstan, lao, latvia-lebanon-lesotho-liberia-libya-liechtenstein-lithuania-luxembourg, Lebanon, liberia, macau, madagascar, malawi, malaysia-maldives, Mali, malta, marshall-islands-martinique-mauritania-mauritius, massechutes, mayotte, mazingira, mbeya, meru, mexico, miami, micronesia, monaco-mongolia-montenegro, montserrat, morocco, mozambique-myanmar, mtwara, mwanza, namibia, nauru, nepal, netherlands, netherlands-antilles, nevada, new-caledonia, new-zealand, newyork, nicaragua, niger, nigeria, niue, north-macedonia, northern-mariana-islands, norway, oman, pakistan, palau, palestine, palestinian-territories, panama, papua-new-guinea, paraguay, peoples-democratic-republic, peru, philadhephia, philipians, Philippines, pitcairn-island, poland, politics, Portugal, puerto-rico, qatar, republic-of, republic-of-brazzaville, republic-of-south-korea, reunion-island, romania, Russia, russian-federation, rwanda, sahara-occidental, saint-kitts-and-nevis, saint-lucia, saint-vincent-and-the-grenadines, samoa, san-marino, sao-tome-and-principe, saudi-arabia, saudiarabia, scotland, Senegal, serbia, seychelles, sierra-leone, Singapore, singida, slovakia-slovak-republic, slovenia, solomon-islands, somalia, southafrica, spain, sri-lanka, sudan, suriname, swaziland-eswatini, sweden, switzerland, syria, syrian-arab-republic, tabora, taiwan-republic-of-china, tajikistan, tanzania, texas, thailand, the-gambia, tibet, timor-leste-east-timor, togo, tokelau, tonga, toronto, trinidad-and-tobago, tunisia, turkey, turkmenistan, turks-and-caicos-islands, tuvalu, uganda, united-arabs-emirates, united-kingdom, united-states, uruguay, uzbekistan, vancover, vanuatu, vatican-city-state-holy-see, venezuela, vietnam, virgin-islands-british, virgin-islands-u-s, wallis-and-futuna-islands, wallis-and-futuna-islands, wallis-et-futuna, washington-dc, western-sahara, yemen, zambia, zambie, zimbabwe
Discover more from cantonadigital
Subscribe to get the latest posts sent to your email.