Madagascar yatangaza hali ya dharura kutokana na uhaba mkubwa wa mafuta unaohusishwa na vita vya Iran

https://zeno.fm/radio/radio-fortune-africa

Na Cantona Joseph April 08, 2026 11:40 (EAT)

Vocalize Pre-Player Loader
Mafuta

Madagascar imetangaza hali ya dharura kwa muda wa wiki mbili kufuatia uhaba mkubwa wa mafuta uliosababishwa na vita vya Marekani na Israel dhidi ya Iran.

Mamlaka zimesema uamuzi huo ulifikiwa baada ya kikao cha baraza la mawaziri Jumanne, kutokana na hofu kwamba hali hiyo inaweza kusababisha vurugu za kijamii.

Kisiwa hicho cha Bahari ya Hindi, ambacho hutegemea mafuta kuzalisha sehemu kubwa ya umeme wake, kinategemea uagizaji wa mafuta kutoka Mashariki ya Kati na usambazaji unatarajiwa kuathirika kwa muda, licha ya kusitishwa kwa mapigano kwa wiki mbili kulikotangazwa usiku.

Mwaka jana, kukatika kwa mara kwa mara kwa umeme na maji nchini Madagascar kulisababisha maandamano yaliyoongozwa na vijana, ambayo baadaye yaligeuka kuwa machafuko ya kisiasa na kusababisha jeshi kuchukua madaraka.

Haijulikani wazi hatua mahsusi ambazo serikali inapanga kuchukua, lakini imesema sasa ina mamlaka ya kuimarisha sekta ya umeme, kupunguza usumbufu zaidi, kudhibiti matumizi, na kuhakikisha huduma za umma zinaendelea.

Meli zaripotiwa kupita katika Mlango bahari wa Hormuz

Mlango bahari wa Hormuz

Kampuni ya kufuatilia meli, MarineTraffic imeonesha leo asubuhi kwamba kumekuwa na “dalili za awali za shughuli za meli” katika Mlango bahari wa Hormuz baada ya njia hiyo kuzuiwa kwa kiasi kikubwa na Iran.

Shirika hilo linaeleza kuwa meli mbili zimepita katika mlango huo, moja inayomilikiwa na Ugiriki na nyingine iliyosajiliwa Liberia.

BBC haijathibitisha taarifa hizi.

Upitishaji wa meli katika mlango huo umekuwa chanzo cha mvutano katika wiki za hivi karibuni, na ingawa mpango wa muda mrefu kuhusu njia hiyo bado haujafahamika, makubaliano ya kusitisha mapigano yaliyotangazwa usiku kucha yanaitaka Iran kuufungua tena.

Baadhi ya nchi zilikuwa tayari zimefikia makubaliano na Iran ili meli zao ziendelee kutumia njia hiyo muhimu ya usafirishaji wa kimataifa zikiwemo Pakistan, India na Ufilipino.

Nchi nyingine zilikuwa zimeshambuliwa katika maeneo karibu na mlango huo, pamoja na maeneo mengine katika Ghuba.

Trump amesema Marekani inafanya kazi kwa karibu na Iran

Trump

Rais wa Marekani Donald Trump amechapisha kwenye mtandao wa Truth Social, akisema kwamba Marekani itafanya kazi na Iran, “ambayo tumebaini imepitia mabadiliko makubwa ya utawala!”

Trump anasema Iran haitarutubisha urani, na Marekani itashirikiana na Tehran “kuchimba na kuondoa ‘chembechembe’ zote za Nyuklia zilizo ardhini. (B-2 Bombers).

“Sasa, na imekuwa, chini ya Ufuatiliaji mkali wa Satilaiti”. Anaongeza: “Hakuna kilichoguswa tangu tarehe ya shambulio. Tunazungumza, na tutazungumza, kuhusu unafuu wa Ushuru na Vikwazo na Iran.

Vipengele vingi kati ya 15 tayari vimekubaliwa.”

Mwenyekiti wa tume ya AU aunga mkono makubaliano ya kusitisha mapigano kati ya Marekani na Iran

Athari za mashambulizi

Mwenyekiti wa Tume ya Umoja wa Afrika ameunga mkono makubaliano ya kusitisha mapigano kati ya Marekani na Iran, akielezea kama hatua muhimu kuelekea kupungua kwa mzozo wa kiuchumi na utulivu wa kikanda.

Mahmoud Ali Youssouf alisema makubaliano hayo, yaliyotangazwa na waziri mkuu wa Pakistan, yanaonesha “uongozi unaostahili pongezi na kujitolea kwa pamoja” katika kupunguza mvutano kati ya pande hizo mbili na washirika wao.

Alisema maendeleo hayo yanaendana na wito wa muda mrefu wa Umoja wa Afrika wa kuzuia na kusuluhisha migogoro kwa amani.

Mwenyekiti wa AU pia alisifu jukumu la wapatanishi, ikiwa ni pamoja na Oman, Uturuki na Misri, ambao juhudi zao za kidiplomasia zilisaidia kupata usitishaji mapigano.

Bw. Youssouf alionya kwamba athari za mgogoro huo zimeonekana zaidi ya eneo la karibu, ikiwa ni pamoja na kote Afrika, ambapo usumbufu wa usambazaji wa mafuta duniani umesababisha ongezeko kubwa la bei za mafuta na mfumuko wa bei.

Kote barani, athari hizo zimeenea. Reuters inaripoti kwamba usumbufu wa mnyororo wa usambazaji unaohusishwa na mgogoro huo pia umeathiri masoko ya mbolea, huku bei zinazoongezeka na uhaba zikitishia uzalishaji wa kilimo katika nchi kadhaa za Afrika.

Hii imezua wasiwasi kuhusu mavuno ya chini ya mazao na kuongezeka kwa ukosefu wa uhakika wa chakula, hasa katika nchi zinazotegemea uagizaji kutoka nje.

Wachambuzi wanasema mataifa mengi ya Afrika yanategemea sana mbolea inayoagizwa kutoka nje, sehemu kubwa ikihusishwa na masoko ya nishati duniani na njia za usafirishaji zinazoweza kuathiriwa na mvutano wa kijiografia.

Kadiri bei zinavyopanda, wakulima mara nyingi hupunguza matumizi, jambo ambalo linaweza kupunguza mavuno na kupanda kwa bei za chakula.

Mwenyekiti wa Tume ya AU alielezea kuunga mkono mazungumzo ya Islamabad na akazitaka pande zote kudumisha kasi kuelekea azimio la kudumu, akisema diplomasia inabaki kuwa njia pekee inayofaa ya kutatua migogoro ya kimataifa.

Zaidi ya vifo 1500 vimeripotiwa nchini Lebanon, Israel ikiapa kuendelea na mashambulizi
.Chanzo cha picha,Reuters
Tangu kuanza kwa vita vya Marekani na Israel dhidi ya Iran mwezi mmoja uliopita, zaidi ya watu 1,530 wameuawa nchini Lebanon, baada ya Israel kuanzisha mashambulizi ya kuwalenga wapiganaji wa Hezbollah, Shirika la habari la AFP limeripoti.

Idadi hiyo ya vifo kulingana na AFP ilitolewa na wizara ya afya ya Lebanon, ambayo inajumuisha vifo vya wanawake 102 na Watoto 130. Zaidi ya watu 4,812 wamejeruhiwa.

Licha ya kusitishwa kwa mapigano nchini Iran, Israel imesisitiza kuwa makubaliano hayo hayajumuishi Lebanon na wataendelea kulenga kundi la Hezbollah.

Katika wiki kadhaa zilizopita, Israel imewatuma wanajeshi wake kusini mwa Lebanon na kudhibiti eneo karibu na mto Litani, Israel ikiapa kuwa lazima iondoe tishio la Hezbollah.

Mapema leo Israel imetekeleza mashambulizi kusini mwa Lebanon.

Falme za kiarabu “ilishinda” vita hivyo

.

Mshauri wa rais wa Falme za Kiarabu amesema kuwa taifa hilo “lilipata ushindi” baada ya kushambuliwa mara kadhaa na Iran tangu kuanza kwa vita hivyo.

“Tulishinda kupitia ulinzi wa kitaifa wa kihistoria uliolinda uhuru, heshima, na kutunza mafanikio yetu baada ya kuchokozwa,” alisema Anwar Gargash.

“Leo, tunasonga mbele tukikabiliana na mazingira magumu kwenye ukanda wetu tukiwa na nguvu zaidi, uelewa zaidi, na uwezo thabiti wa kushawishi mustakabali wa siku za usoni.”

Wizara ya ulinzi ya taifa hilo imekuwa ikichapisha taarifa ya jinsi imekuwa ikidungua makombora ya Iran.

Hapo jana katika taarifa waliyoitoa, tangu kuanza kwa vita hivyo wameweza kudundua ndege zisizo na rubani 2221, makombora ya majini 26 na makombora ya kibalistiki 520.

Waziri wa mambo ya kigeni wa Oman, ameipongeza Pakistan kwa juhudi zao za kuhakikisha mkataba huo unaafikiwa na kusema kuwa anatumai utakuwa wa kudumu.

“Tutafanya kila tuwezalo kuunga mkono usitishaji mapigano” – Keir Starmer

.
Maelezo ya picha,Waziri mkuu wa Uingereza Keir Starmer

Waziri mkuu wa Uingereza Keir Starmer amesema `watafanya kila wawezalo kuhakikisha makubaliano ya kusitisha vita kwa muda nchini Iran yanadumu`

“Tumepokea vyema makubaliano ya kusitisha mapigano yaliyoafikiwa na yataleta afueni kwa ukanda huo na kote duniani` alisema Starmer

“Pamoja na washirika wetu tutaunga mkono makubaliano hayo ya kusitisha vita hadi suluhu ya kudumu ipatikane na Mlango Bahari wa Hormuz ufunguliwe`

Ofisi ya Waziri huyo mkuu imetangaza kuwa atasafiri kukutana na viongozi wa mataifa ya Ghuba na kutangaza atakavyounga mkono makubaliano ya kusitisha vita.

Katika mikutano na viongozi wa kikanda, atasisitiza uungwaji mkono usioyumba wa Uingereza na hitaji la azimio la kidiplomasia la muda mrefu ili kuhakikisha usitishaji mapigano unapelekea makubaliano ya kudumu.

Pia atashiriki katika mazungumzo kuhakikisha Mlango Bahari wa Hormuz unasalia wazi.

Wairani wakusanyika mjini Tehran baada ya tangazo la kusitishwa mapigano

.

Raia wa Iran wamekusanyika katika mji mkuu wa taifa hilo, Tehran, wakiwa wamebeba bendera ya taifa na mabango yenye picha ya Kiongozi Mkuu Mojtaba Khamenei.

Raia wa Iran wamejitokeza katika barabara za mji wa Tehran baada ya kutangazwa kwa makubaliano ya kusitisha mapigano kwa muda.

.

Kusitishwa kwa vita hivyo kwa muda kumepokelewa kwa hisia mseto miongoni mwa raia wa Iran.

Kuna afueni kwa sababu viwanda vya nishati havitashambuliwa tena, lakini kwa wale ambao wanapinga utawala wa taifa hilo, hawajalipokea vyema.

.

Soma zaidi:

Mlinda lango Raya ataisaidia Arsenal kurejea kwenye mstari?

.

David Raya ndiye kipa bora zaidi duniani, kulingana na wachezaji wenzake wa Arsenal.

Kipa huyo wa Gunners aliokoa mipira minne katika mchezo wake wa mwisho wa Ligi ya Mabingwa dhidi ya Sporting, huku Kai Havertz akifunga bao la ushindi dakika za mwisho.

Mchezaji huyo wa kimataifa wa Uhispania ameweka rekodi ya kufungwa mabao 22 katika mechi 41 katika mashindano yote msimu huu.

Arsenal ilisafiri hadi Sporting na kiwango cha Raya dhidi ya Sporting kilionyesha kwa nini mchezaji huyo wa miaka 30 ndiye nambari moja kwa Gunners.

Raya ameweka rekodi ya kutofungwa mabao mengi kuliko kipa yeyote katika ligi tano bora barani Ulaya, akiwa amefungwa mabao 22 tu katika mashindano yote mbele ya Yann Sommer wa Inter.

Kipa huyo wa zamani wa Brentford amek

afghanistanafricaalbaniaalgeriaAmericaamerican-samoaandorraangolaanguillaantarcticaantigua-and-barbudaargentinaarmeniaarubaarushaaustraliaaustriaazerbaijanbahamasbahrainbangladeshbarbadosbelarusBelgiumbelizebeninbermudabhutanboliviabosnia-and-herzegovinabotswanaBoukinafasobrazilbrunei-darussalambulgariaburkina-fasoburmaburundicaliforniacambodiacamerooncanadacape-verdecayman-islandscentral-african-republicChadchicagochilechinachristmas-islandcocos-keeling-islandscolombiacomoroscongocook-islandscosta-ricacote-divoire-ivory-coastCroatiacubacyprusczech-republicdarsalaamdemocratic-peoples-rep-north-koreademocratic-republic-of-the-congo-kinshasadenmarkdjiboutidodomadominicadominican-republicdr-congodubaieast-timor-timor-lesteecuadoregyptegyptyel-salvadorenglandequatorial-guineaequitorial-guineaeritreaestoniaeswatiniethiopiafalkland-islandsfaroe-islandsfederal-states-of-moldovafijifinlandFloridafrancefrench-guianafrench-polynesiafrench-southern-territoriesgabongazageorgiagermanyghanagibraltargomaGreecegreenlandgrenadaguadeloupeguamguatemalaguineaguinea-bissauguyanahabarihaitiholy-seehondurashong-konghoustonhungaryicelandindiaindonesiaIowairaniran-islamic-republic-ofiraqirelandisraelitaliaitalyivory-coastjamaicajapanjordankaratukazakhstankilimanjarokinshasakiribatikiswahilikoreakosovokuwaitkyrgyzstanlaolatvia-lebanon-lesotho-liberia-libya-liechtenstein-lithuania-luxembourgLebanonliberiamacaumadagascarmalawimalaysia-maldivesMalimaltamarshall-islands-martinique-mauritania-mauritiusmassechutesmayottemazingirambeyamerumexicomiamimicronesiamonaco-mongolia-montenegromontserratmoroccomozambique-myanmarmtwaramwanzanamibianaurunepalnetherlandsnetherlands-antillesnevadanew-caledonianew-zealandnewyorknicaraguanigernigerianiuenorth-macedonianorthern-mariana-islandsnorwayomanpakistanpalaupalestinepalestinian-territoriespanamapapua-new-guineaparaguaypeoples-democratic-republicperuphiladhephiaphilipiansPhilippinespitcairn-islandpolandpoliticsPortugalpuerto-ricoqatarrepublic-ofrepublic-of-brazzavillerepublic-of-south-koreareunion-islandromaniaRussiarussian-federationrwandasahara-occidentalsaint-kitts-and-nevissaint-luciasaint-vincent-and-the-grenadinessamoasan-marinosao-tome-and-principesaudi-arabiasaudiarabiascotlandSenegalserbiaseychellessierra-leoneSingaporesingidaslovakia-slovak-republicsloveniasolomon-islandssomaliasouthafricaspainsri-lankasudansurinameswaziland-eswatiniswedenswitzerlandsyriasyrian-arab-republictaborataiwan-republic-of-chinatajikistantanzaniatexasthailandthe-gambiatibettimor-leste-east-timortogotokelautongatorontotrinidad-and-tobagotunisiaturkeyturkmenistanturks-and-caicos-islandstuvaluugandaunited-arabs-emiratesunited-kingdomunited-statesuruguayuzbekistanvancovervanuatuvatican-city-state-holy-seevenezuelavietnamvirgin-islands-britishvirgin-islands-u-swallis-and-futuna-islandswallis-and-futuna-islandswallis-et-futunawashington-dcwestern-saharayemenzambiazambiezimbabwe

CantonaDigital
CantonaDigital

Listen Live Radio Fortune Africa
Ukweli Na Burudani.

-Be ready to be Impacted, Inspired & Empowered.

-Keep watching our Channels

Cantona Cast Television,

Fortune Television Network (FTN)

Donation
Paypal https://www.paypal.com/donate/?hosted_button_id=6EKXMLNW8W6A2&fbclid=IwY2xjawQxeChleHRuA2FlbQIxMABicmlkETFRdkNBRndpclRDQTB5bXZZc3J0YwZhcHBfaWQQMjIyMDM5MTc4ODIwMDg5MgABHq960uGsyU3ABRIBc2h-iXGhHATvuEqe55gFsQ-rDb0fT-Z7SIQ3TV8LnkpD_aem_ybU2SvBlvyqrVsS9NAczRw

An attitude determines an altitude.

All Rights Reserved © The Cantona Group PLC||2025

5,446 posts
0 followers

Fediverse Followers


Discover more from cantonadigital

Subscribe to get the latest posts sent to your email.

Leave a Reply