Shirika la Ndege Tanzania laendelea kuendeshwa kwa hasara.

https://zeno.fm/radio/radio-fortune-africa

Na Cantona Joseph Imechapishwa : March 30, 2026 17:37 (EAT)

Vocalize Pre-Player Loader
XCV

Kwa mujibu wa taarifa iliyowasilishwa leo na Mdhibiti na Mkaguzi Mkuu wa Hesabu za Serikali, Dkt. Charles Kichere, Shirika la Ndege Tanzania (ATCL) linaendelea kujiendesha kwa hasara.

Amesema shirika hilo limepata hasara ya zaidi ya shilingi bilioni 191 ndani ya kipindi cha mwaka mmoja. Kwa ujumla, tangu kuanzishwa kwake, shirika hilo limekusanya hasara ya takribani shilingi bilioni 748.

Katika kipindi hicho cha mwaka mmoja, shirika limelipa zaidi ya shilingi bilioni 310 kwa abiria kama fidia kutokana na safari zilizositishwa au kuahirishwa. Hasara hiyo imechangiwa kwa kiasi kikubwa na gharama za uendeshaji kuwa kubwa kuliko mapato yanayopatikana.

Aidha, matumizi yasiyoridhisha ya ndege ya mizigo yameelezwa kuwa miongoni mwa sababu za hasara. Katika miezi ya hivi karibuni, ndege hiyo ilifanya safari nyingi zisizo na tija na hatimaye kusimamishwa, hali iliyoongeza kiwango cha hasara.

Akizungumzia mashirika mengine ya umma yanayoendeshwa kwa hasara, Dkt. Kichere alilitaja Shirika la Reli Tanzania (TRC).

Alisema licha ya mapato ya reli ya kisasa (SGR) kuongezeka, reli ya zamani imeendelea kupata hasara kutokana na kuongezeka kwa ajali. Ndani ya mwaka mmoja, jumla ya ajali 328 zimeripotiwa, na kusababisha uharibifu wa miundombinu.

Kuhusu hali ya deni la taifa, Dkt. Kichere alisema limeongezeka hadi kufikia shilingi trilioni 110 likijumuisha deni la ndani na la nje. Ndani ya mwaka mmoja, deni hilo limeongezeka kwa zaidi ya shilingi trilioni 12, sawa na asilimia 13.4.

Ongezeko hilo limetokana na kuongezeka kwa mikopo ya nje pamoja na kushuka kwa thamani ya shilingi ya Tanzania dhidi ya dola ya Marekani.

Hata hivyo, alibainisha kuwa pamoja na ongezeko hilo, deni la taifa bado ni himilivu kwani lipo katika kiwango cha asilimia 40.7, ambacho ni chini ya ukomo wa asilimia 55.

Akisoma taarifa ya ukaguzi wa hesabu za vyama vya siasa, Mkaguzi Mkuu alisema vyama viwili CUF na NRA vimepata hati zenye mashaka kutokana na kutokuwasilisha nyaraka zote zinazohitajika. Wakati huo huo, chama kikuu cha upinzani, CHADEMA, hakijakaguliwa kutokana na mashauri yaliyopo mahakamani yanayohusiana na mali za chama hicho.

Kwa upande wake, Rais Samia Suluhu Hassan amesema serikali itafanyia kazi mapendekezo yote yaliyotolewa na Mdhibiti na Mkaguzi Mkuu wa Hesabu za Serikali haraka iwezekanavyo.

Baada ya kusomwa kwa taarifa hizo, zinatarajiwa kuwasilishwa bungeni ndani ya siku saba kwa ajili ya kujadiliwa na kutolewa mapendekezo.

xcv

Donald Trump amesema kuwa Marekani iko katika “mazungumzo muhimu” na utawala mpya wa Iran ambao, kulingana na rais huyo, unaweza “kukomesha operesheni za kijeshi za Marekani nchini Iran.”

Kupitia chapisho lake kwenye mtandao Truth Social, Trump aliandika: “Marekani iko katika mazungumzo muhimu na UTAWALA MPYA, NA WENYE BUSARA ZAIDI ili kumaliza operesheni zetu za kijeshi nchini Iran.

“Maendeleo makubwa yamepatikana, lakini ikiwa kwa sababu yoyote makubaliano hayatapatikana hivi karibuni, ingawa huenda yakapatikana na ikiwa Mlango-Bahari wa Hormuz hautafunguliwa mara moja kuruhusu biashara, tutahitimisha ‘uwepo’ wetu mzuri nchini Iran kwa kulipua na kuharibu kabisa mitambo yao yote ya kuzalisha umeme, visima vya mafuta na Kisiwa cha Kharg (na huenda pia mitambo yote ya kuondoa chumvi kwenye maji ya bahari!), ambayo kwa makusudi bado hatujaigusa.

“Hii itakuwa ni kulipiza kisasi kwa wanajeshi wetu wengi, na wengine, ambao Iran imewaua na kuwachinja katika kipindi cha miaka 47 cha ‘Utawala wa Hofu’ uliopita nchini Iran.

XCV

Waziri mkuu wa Uingereza Keir Starmer amesisitiza kuwa wanajeshi wa Uingereza hawatapelekwa nchini Iran.

Alipoulizwa na waandishi wa habari asubuhi hii kama anafikiria kupeleka wanajeshi wa Uingereza kupigana vita Mashariki ya Kati, Starmer alisema: “Hii si vita yetu na hatutajiingiza.”

Aidha waziri mkuu Starmer aliendelea kutetea msimamo wake kuhusu mzozo huo, akisema kuwa Uingereza inachukua “hatua za kujilinda” kulinda “maisha ya Waingereza, maslahi ya Uingereza na, bila shaka, washirika wetu katika eneo hilo.”

Starmer amesema Uingereza itaendelea kulinda maslahi yake na kushiriki katika jitihada za kufungua tena Mlango-Bahari wa Hormuz, lakini akaongeza: “Hatutaingizwa kwenye vita hii.”

xcv

Wakati Israel ikiendelea kusonga mbele kusini mwa Lebanon, BBC imezungumza na wakazi wa mji wa Metula ulioko upande wa Israel, karibu na mpaka.

Gabriella Kopellowitz ni mfanyakazi wa kijamii mwenye umri wa miaka 28 anayefanya kazi katika mji huo. Anasema, “Tuko karibu sana na mpaka kiasi kwamba tunaweza kuona vijiji vilivyoko ndani ya Lebanon kutoka hapa.”

Anaongeza kuwa kuna ving’ora vinavyolia takribani mara tano kwa siku, vikitoa tahadhari ya makombora au roketi zinazokuja.

“Makombora yanapokuja kutoka Iran, tunakuwa na takribani dakika tano za kukimbilia kwenye hifadhi ya kujikinga dhidi ya mabomu, lakini yanapokuja kutoka Hezbollah tunakuwa na chini ya dakika moja.”

Kama mfanyakazi wa kijamii, Gabriella amekuwa akisaidia kuwahamisha watu ambao nyumba zao zimeharibiwa na makombora, na pia huzunguka mjini akiwapelekea chakula wazee ambao hawawezi kutoka nje.

Anasema mji huo ni tulivu zaidi kuliko kawaida.

“Familia nyingi zimeondoka – si jambo la kufurahisha kujua kwamba Hezbollah wanataka kukulenga,” anasema Gabriella.

“Kwa kiasi fulani tuko katika hatari hapa Metula,” anaongeza, lakini pia anasema, “unazoea. Mimi siogopi. Mara nyingi makombora hayo huzuiwa kabla hayajafika.”

xcv

Mbunge wa Iran, Alaeddin Boroujerdi, amesema kuwa mpango mpya wa bunge kuhusu mlango bahari wa Hormuz unatarajiwa kupitishwa hivi karibuni.

Kwa mujibu wa Boroujerdi, chini ya “mfumo mpya” unaopendekezwa, hakuna meli itakayoruhusiwa kupita katika mlango huo muhimu bila kupata kibali kutoka Iran.

Aidha, Iran inapanga kuanzisha mfumo wa kutoza ushuru kwa meli zinazopita katika eneo hilo.

Alieleza kuwa kulinda usalama na kutoa huduma kwa meli kunahitaji gharama, hivyo ni muhimu kuweka mfumo wa kukusanya kodi ya usafirishaji.

Katika hatua nyingine, mbunge huyo alisema kuwa “wakati umefika” kwa Iran kujiondoa katika mkataba wa kuzuia usambazaji wa silaha za nyuklia, Treaty on the Non-Proliferation of Nuclear Weapons (NPT).

Alidai kuwa mkataba huo umepoteza umuhimu wake kufuatia mashambulizi yaliyolenga miundombinu ya nyuklia ya Iran, ambayo yalihusishwa na Israel pamoja na Marekani.

.

Picha zilizothibitishwa zinaonyesha ndege ya Marekani yenye kutoa amri katika uwanja wa vita ikiwa imeharibiwa katika kambi ya kijeshi nchini Saudi Arabia.

Picha hizo zinaonekana kusambazwa kwa mara ya kwanza kwenye ukurasa wa Facebook wenye habari za kijeshi za Marekani.

Zinaonyesha ndege ya E-3 Sentry ambayo imevunjwa vipande viwili.

Tumethibitisha kuwa picha hizo zilipigwa katika kambi ya jeshi la wanahewa ya Prince Sultan yapata kilomita 100 (maili 62) kusini-mashariki mwa mji mkuu wa Saudi Arabia Riyadh.

Kile kinachoonekana kwenye picha hizo, ikiwa ni pamoja na nguzo za chuma, vitengo vya kuhifadhia na alama kwenye maeneo ya lami, vinaendana na picha za setilaiti.

Jeshi Kuu la Marekani bado halijatoa maoni yake hadharani kuhusu tukio hilo. BBC imeomba maoni.

Siku ya Ijumaa afisa mmoja wa Marekani aliiambia Reuters kwamba wafanyakazi 12 wa Marekani walikuwa wamejeruhiwa, wawili kati yao wakiwa wamejeruhiwa vibaya katika shambulizi la kijeshi la Iran kwenye kambi ya wanajeshi.

Gazeti la Wall Street Journal liliripoti kwamba takriban ndege mbili za Marekani za kujaza mafuta pia ziliharibiwa.

Siku ya Jumapili shirika la habari la Fars linalohusishwa na Kikosi cha Jeshi la Iran la IRGC lilisema ndege isiyo na rubani ya Shahed ilishambulia ndege ya E-3.

BBC Verify pia imeona ndege aina ya E-3 katika eneo hili katika picha ya setilaiti iliyopigwa tarehe 11 Machi. Hatuwezi kusema kama ni ndege hiyo hiyo

Katika moja ya picha zilizothibitishwa, nambari ya mkia wa ndege inaonekana. Kwa kutumia hii tuliangalia tovuti ya kufuatilia ndege ya Flightradar24 ambayo ilionyesha ilikuwa ikipaa angani karibu na kambi ya kijeshi mnamo Machi 18.

Picha ya setilaiti iliyopigwa Ijumaa inaonekana kuonyesha moto kwenye eneo la kuegesha ndege katika kambi ya kijeshi, yapata mita 1,600 (futi 5,200) mashariki mwa E-3.

Haijulikani wazi kama hii ilikuwa sehemu ya shambulizi lile lile ambapo ndege inaonekana kwenye picha hizi iliharibiwa.

.

Boeing E-3 Awacs – imetokana na ndege ya Boeing 707 na ina diski ya rada inayozunguka iliyowekwa nyuma ya mwili wa ndege.

Rada hii inaruhusu kugundua na kufuatilia maeneo yanayoweza kulengwa katika masafa marefu ili kutoa onyo la mapema kuhusu vitisho vinavyoweza kutokea wakati wa vita.

Ndege hiyo inatoa “taarifa kwa makamanda wanaoendesha shughuli zao angani ili kupata na kudumisha udhibiti wa vita vya anga”, kulingana na tovuti ya USAF.

Ndege ya kwanza ya aina hiyo ilianza kutumika mwaka wa 1977 na imeripotiwa kwamba E-3 inatarajiwa kuendelea kufanya kazi na USAF hadi 2035.

xcv

Wizara ya ulinzi ya Iraq imesema kuwa makombora yamelenga kambi ya anga ya Mohammed Alaa, na kuharibu ndege moja ya Jeshi la Iraq.

Hakuna vifo vilivyoripotiwa katika shambulio hilo lililotokea alfajiri ya leo karibu na Baghdad International Airport.

Katika taarifa iliyotolewa kupitia tovuti yake, wizara ya ulinzi ya Iraq imelaani tukio hilo na kulielezea kama “kitendo cha woga na cha kihalifu kinacholenga taasisi ya kijeshi na uwezo wake wa ulinzi”.

Mapema leo, Jeshi la Syria, lilisema limefanikiwa kuzima shambulio kubwa la ndege zisizo na rubani lililolenga vituo vyake kadhaa vya kijeshi karibu na mpaka wa Iraq, kwa mujibu wa shirika la habari la serikali la SANA.

Kamandi ya operesheni ya jeshi hilo iliambia SANA kuwa ndege nyingi zisizo na rubani zilidunguliwa na kuangushwa kabla ya kufikia maeneo yaliyokusudia kulengwa.

xcv

Jeshi la Israel limetangaza kuwa limeanza kushambulia miundombinu ya kundi la Hezbollah katika mji mkuu wa Lebanon, Beirut.

Picha zilizopigwa asubuhi zinaonyesha moshi ukifuka kutoka katika vitongoji vya kusini mwa mji huo.

Jeshi la Ulinzi la Israel, (IDF) limesema kuwa linalenga “miundombinu ya kigaidi” ya kundi hilo linaloungwa mkono na Iran.

Vyombo vya habari vya Lebanon pia vimeripoti wimbi jipya la mashambulizi ya anga ya Israel katika eneo la kusini mwa Beirut.

Zaidi ya watu milioni moja wamelazimika kuhama makazi yao nchini Lebanon, huku vita vinavyoihusisha Marekani na Israel dhidi ya Iran vikiendelea kuathiri eneo pana la mashariki ya kati.

Mtoto mmoja aliyezungumza na BBC alisema anahisi “aibu” kulala barabarani baada ya familia yake kulazimika kukimbia makazi yao mjini Beirut.

afghanistanafricaalbaniaalgeriaAmericaamerican-samoaandorraangolaanguillaantarcticaantigua-and-barbudaargentinaarmeniaarubaarushaaustraliaaustriaazerbaijanbahamasbahrainbangladeshbarbadosbelarusBelgiumbelizebeninbermudabhutanboliviabosnia-and-herzegovinabotswanaBoukinafasobrazilbrunei-darussalambulgariaburkina-fasoburmaburundicaliforniacambodiacamerooncanadacape-verdecayman-islandscentral-african-republicChadchicagochilechinachristmas-islandcocos-keeling-islandscolombiacomoroscongocook-islandscosta-ricacote-divoire-ivory-coastCroatiacubacyprusczech-republicdarsalaamdemocratic-peoples-rep-north-koreademocratic-republic-of-the-congo-kinshasadenmarkdjiboutidodomadominicadominican-republicdr-congodubaieast-timor-timor-lesteecuadoregyptegyptyel-salvadorenglandequatorial-guineaequitorial-guineaeritreaestoniaeswatiniethiopiafalkland-islandsfaroe-islandsfederal-states-of-moldovafijifinlandFloridafrancefrench-guianafrench-polynesiafrench-southern-territoriesgabongazageorgiagermanyghanagibraltargomaGreecegreenlandgrenadaguadeloupeguamguatemalaguineaguinea-bissauguyanahabarihaitiholy-seehondurashong-konghoustonhungaryicelandindiaindonesiaIowairaniran-islamic-republic-ofiraqirelandisraelitaliaitalyivory-coastjamaicajapanjordankaratukazakhstankilimanjarokinshasakiribatikiswahilikoreakosovokuwaitkyrgyzstanlaolatvia-lebanon-lesotho-liberia-libya-liechtenstein-lithuania-luxembourgLebanonliberiamacaumadagascarmalawimalaysia-maldivesMalimaltamarshall-islands-martinique-mauritania-mauritiusmassechutesmayottemazingirambeyamerumexicomiamimicronesiamonaco-mongolia-montenegromontserratmoroccomozambique-myanmarmtwaramwanzanamibianaurunepalnetherlandsnetherlands-antillesnevadanew-caledonianew-zealandnewyorknicaraguanigernigerianiuenorth-macedonianorthern-mariana-islandsnorwayomanpakistanpalaupalestinepalestinian-territoriespanamapapua-new-guineaparaguaypeoples-democratic-republicperuphiladhephiaphilipiansPhilippinespitcairn-islandpolandpoliticsPortugalpuerto-ricoqatarrepublic-ofrepublic-of-brazzavillerepublic-of-south-koreareunion-islandromaniaRussiarussian-federationrwandasahara-occidentalsaint-kitts-and-nevissaint-luciasaint-vincent-and-the-grenadinessamoasan-marinosao-tome-and-principesaudi-arabiasaudiarabiascotlandSenegalserbiaseychellessierra-leoneSingaporesingidaslovakia-slovak-republicsloveniasolomon-islandssomaliasouthafricaspainsri-lankasudansurinameswaziland-eswatiniswedenswitzerlandsyriasyrian-arab-republictaborataiwan-republic-of-chinatajikistantanzaniatexasthailandthe-gambiatibettimor-leste-east-timortogotokelautongatorontotrinidad-and-tobagotunisiaturkeyturkmenistanturks-and-caicos-islandstuvaluugandaunited-arabs-emiratesunited-kingdomunited-statesuruguayuzbekistanvancovervanuatuvatican-city-state-holy-seevenezuelavietnamvirgin-islands-britishvirgin-islands-u-swallis-and-futuna-islandswallis-and-futuna-islandswallis-et-futunawashington-dcwestern-saharayemenzambiazambiezimbabwe

CantonaDigital
CantonaDigital

Listen Live Radio Fortune Africa
Ukweli Na Burudani.

-Be ready to be Impacted, Inspired & Empowered.

-Keep watching our Channels

Cantona Cast Television,

Fortune Television Network (FTN)

Donation
Paypal https://www.paypal.com/donate/?hosted_button_id=6EKXMLNW8W6A2&fbclid=IwY2xjawQxeChleHRuA2FlbQIxMABicmlkETFRdkNBRndpclRDQTB5bXZZc3J0YwZhcHBfaWQQMjIyMDM5MTc4ODIwMDg5MgABHq960uGsyU3ABRIBc2h-iXGhHATvuEqe55gFsQ-rDb0fT-Z7SIQ3TV8LnkpD_aem_ybU2SvBlvyqrVsS9NAczRw

An attitude determines an altitude.

All Rights Reserved © The Cantona Group PLC||2025

5,344 posts
0 followers

Fediverse Followers


Discover more from cantonadigital

Subscribe to get the latest posts sent to your email.

Leave a Reply