Radio Fortune Africa -Ukweli na Burudani
https://zeno.fm/radio/radio-fortune-africa
Na Cantona Joseph Imechapishwa : March 28, 2026 16:44 (EAT)



Waasi wa Houthi wanaoungwa mkono na Iran nchini Yemen wamesema wameishambulia Israel kwa mara ya kwanza tangu kuanza kwa vita kati ya Iran, Marekani na Israel, wakidai kurusha makombora ya balistiki kulenga maeneo nyeti ya kijeshi ya Israel.
Kundi hilo limesema lilirusha makombora kadhaa yakilenga “maeneo nyeti ya kijeshi ya Israel” ikiwa ni sehemu ya kujibu mashambulizi yanayodaiwa kufanywa dhidi ya Iran pamoja na Lebanon, Iraq na maeneo ya Palestina.
Houthi wameongeza kuwa mashambulizi yao yataendelea hadi kile walichokiita “uchokozi” dhidi ya pande zote utakapotamatika.
Taarifa hiyo imekuja baada ya jeshi la Israel kusema limefanikiwa kuzuia kombora lililorushwa kutoka Yemen kuelekea Israel.
Wakati huo huo, Waziri wa Mambo ya Nje wa Marekani, Marco Rubio, amesema Marekani inatarajia kumaliza operesheni za kijeshi ndani ya wiki chache zijazo, huku mvutano ukiendelea kuongezeka katika eneo hilo.
Huenda kombora la Marekani lilitumika katika shambulio lililosababisha vifo Iran – Wataalamu

Wataalamu wa silaha wanasema huenda makombora ya kisasa ya Marekani yalitumika katika shambulio baya lililolenga eneo la makazi nchini Iran mwezi uliopita, kwa mujibu wa uchambuzi wa video za tukio hilo.
Wataalamu hao walisema kuwa kifaa cha kurushwa kilichoonekana kwenye video ya shambulio dhidi ya majengo ya makazi katika mji wa kusini wa Lamerd kinafanana na kombora la Precision Strike Missile (PrSM).
Silaha hiyo ni kombora jipya la masafa marefu linalotumiwa na jeshi la Marekani.
Kwa mujibu wa vyombo vya habari vya serikali ya Iran, watu wasiopungua 21 waliuawa katika mashambulizi mawili yaliyolenga mji huo siku hiyo, yakigonga majengo ya makazi pamoja na ukumbi wa michezo ulioko umbali wa takribani mita 300.
Kamandi ya kijeshi ya Marekani inayosimamia operesheni za Mashariki ya Kati (Centcom) haijatoa maoni kuhusu tukio hilo.
Meli ya kivita ya Marekani inaelekea katika eneo la mashariki ya kati

Meli ya kivita ya Marekani inayobeba ndege, USS George H. W. Bush, ambayo ni kama kambi ya anga inayosafiri baharini ikiwa na uwezo wa kubeba zaidi ya ndege 80, inatarajiwa kupelekwa katika eneo la Kamandi kuu ya jeshi la Marekani (CENTCOM) huko Mashariki ya Kati.
Vyanzo kadhaa vimeliambia shirika la BBC kupitia mshirika wake wa Marekani, CBS News.
Meli hiyo kubwa pamoja na kikosi chake cha mashambulizi ilikamilisha mafunzo ya maandalizi ya kupelekwa vitani mapema mwezi huu, na sasa inaweza kujiunga na operesheni za Marekani dhidi ya Iran, kwa mujibu wa maafisa wa Marekani walioliambia CBS.
Wakati huo huo, manowari mbili za kivita zenye makombora ya kuongozwa, USS Donald Cook na USS Mason, pia zimeondoka Marekani wiki hii zikielekea kujiunga na operesheni hizo dhidi ya Iran.
Nyingine, USS Ross, nayo imeondoka Marekani wiki hii, ingawa hadi sasa haijatajwa hadharani inaelekea wapi.
Tiger Woods akamatwa kwa kuendesha gari akiwa amelewa, asababisha ajali

Mchezaji mashuhuri wa gofu Tiger Woods amekamatwa kwa tuhuma za kuendesha gari akiwa chini ya ushawishi wa kilevi baada ya kupata ajali katika jimbo la Florida, mamlaka zimethibitisha. Polisi pia wamesema ameshtakiwa kwa kusababisha uharibifu wa mali na kukataa kufanya kipimo cha kisheria.
Kwa mujibu wa Ofisi ya Sheriff ya Martin County, Woods mwenye umri wa miaka 50 alipindua gari lake aina ya Land Rover baada ya kugonga lori alipokuwa akijaribu kulipita kwa mwendo kasi katika eneo la Jupiter Island. Hakuna mtu aliyejeruhiwa katika ajali hiyo.
Maafisa walisema hawakushuku uwepo wa pombe mwilini mwake, lakini walihisi huenda alikuwa chini ya ushawishi wa dutu isiyojulikana. Woods alifaulu kipimo cha pumzi (breathalyser) lakini alikataa kutoa sampuli ya mkojo kwa uchunguzi zaidi.
Sheriff John Budensiek alisema uchunguzi wa awali ulionyesha dalili za ulevi, ingawa Woods alieleza kuwa ana historia ya majeraha na upasuaji ambayo yalizingatiwa wakati wa vipimo vilivyofanyika barabarani.
Baada ya tukio hilo, Woods aliwekwa chini ya ulinzi wa polisi kwa muda kabla ya kuachiwa kwa dhamana. Mashtaka dhidi yake ni ya kiwango cha chini (misdemeanours), na mamlaka zimesema huenda isiwezekane kubaini kwa uhakika aina ya dutu iliyosababisha hali hiyo.
Urusi na Iran zajadili uwezekano wa kumaliza vita kwa njia ya mazungumzo

Mawaziri wa mambo ya nje wa Urusi na Iran wamejadili uwezekano wa kumaliza mzozo unaoendelea kwa njia ya kidiplomasia, huku wakisisitiza umuhimu wa suluhisho la kisiasa katika vita vinavyoendelea Mashariki ya Kati.
Waziri wa Mambo ya Nje wa Urusi, Sergei Lavrov, alifanya mazungumzo na mwenzake wa Iran, Abbas Araqchi, kuhusu namna ya kuhamisha mzozo huo kutoka uwanja wa kijeshi kwenda kwenye mazungumzo ya kisiasa na kidiplomasia (Reuters).
Kwa mujibu wa taarifa ya Wizara ya mambo ya nje ya Urusi, mawaziri hao walijadili kwa kina hali ya kisiasa na kijeshi katika eneo la Mashariki ya Kati, wakieleza kuwa mgogoro huo umetokana na kile walichokiita uchokozi wa Marekani na Israel dhidi ya Iran.
Pia walibadilishana mawazo kuhusu uwezekano wa kufikia suluhisho la kudumu kwa kuzingatia sheria za kimataifa na maslahi ya nchi zote katika ukanda huo.
Taarifa hiyo ilieleza pia kuwa Urusi imewasilisha misaada ya kibinadamu nchini Iran kama sehemu ya ushirikiano wao wa kimkakati unaojumuisha sekta za siasa, uchumi, kijeshi na nishati. Hata hivyo, makubaliano hayo hayajumuishi ulinzi wa pamoja kati ya nchi hizo mbili.
Wakati huo huo, Mawaziri wa mambo ya nje wa Ulaya walitumia mkutano wa G7 kumueleza Waziri wa Mambo ya Nje wa Marekani kuwa Urusi inashutumiwa kusaidia Iran kulenga majeshi ya Marekani katika vita vinavyoendelea Mashariki ya Kati.
Wanajeshi wa Marekani wajeruhiwa Saudi Arabia baada ya shambulio la Iran

Angalau wanajeshi 12 wa Marekani wamejeruhiwa kufuatia shambulio lililolenga kambi ya anga ya Prince Sultan nchini Saudi Arabia, huku vita kati ya Iran na Marekani na Israel ikiingia mwezi wa pili.
Idadi hiyo imeongezeka kutoka 10 iliyoripotiwa awali, kwa mujibu wa taarifa za vyombo vya habari vya Marekani.
Vyombo vya habari vya Marekani vinaripoti kuwa wanajeshi hao walijeruhiwa katika shambulio la Iran lililohusisha angalau kombora moja pamoja na ndege zisizo na rubani (drones), kwa mujibu wa mshirika wa habari wa BBC, CBS.
Inaelezwa kuwa angalau wanajeshi wawili wako katika hali mbaya sana baada ya jengo walilokuwwepo ndani kulengwa moja kwa moja wakati wa shambulio hilo.
Vyanzo visivyotajwa vimeeleza kuwa pia ndege kadhaa za kujaza mafuta angani ziliharibiwa katika tukio hilo.
Hadi wakati wa kuripoti habari hii, Wizara ya Ulinzi ya Marekani (Pentagon) pamoja na Kamandi Kuu ya Marekani (US Central Command) hazikuwa zimetoa tamko rasmi kujibu taarifa hizo.
afghanistan, africa, albania, algeria, America, american-samoa, andorra, angola, anguilla, antarctica, antigua-and-barbuda, argentina, armenia, aruba, arusha, australia, austria, azerbaijan, bahamas, bahrain, bangladesh, barbados, belarus, Belgium, belize, benin, bermuda, bhutan, bolivia, bosnia-and-herzegovina, botswana, Boukinafaso, brazil, brunei-darussalam, bulgaria, burkina-faso, burma, burundi, california, cambodia, cameroon, canada, cape-verde, cayman-islands, central-african-republic, Chad, chicago, chile, china, christmas-island, cocos-keeling-islands, colombia, comoros, congo, cook-islands, costa-rica, cote-divoire-ivory-coast, Croatia, cuba, cyprus, czech-republic, darsalaam, democratic-peoples-rep-north-korea, democratic-republic-of-the-congo-kinshasa, denmark, djibouti, dodoma, dominica, dominican-republic, dr-congo, dubai, east-timor-timor-leste, ecuador, egypt, egypty, el-salvador, england, equatorial-guinea, equitorial-guinea, eritrea, estonia, eswatini, ethiopia, falkland-islands, faroe-islands, federal-states-of-moldova, fiji, finland, Florida, france, french-guiana, french-polynesia, french-southern-territories, gabon, gaza, georgia, germany, ghana, gibraltar, goma, Greece, greenland, grenada, guadeloupe, guam, guatemala, guinea, guinea-bissau, guyana, habari, haiti, holy-see, honduras, hong-kong, houston, hungary, iceland, india, indonesia, Iowa, iran, iran-islamic-republic-of, iraq, ireland, israel, italia, italy, ivory-coast, jamaica, japan, jordan, karatu, kazakhstan, kilimanjaro, kinshasa, kiribati, kiswahili, korea, kosovo, kuwait, kyrgyzstan, lao, latvia-lebanon-lesotho-liberia-libya-liechtenstein-lithuania-luxembourg, Lebanon, liberia, macau, madagascar, malawi, malaysia-maldives, Mali, malta, marshall-islands-martinique-mauritania-mauritius, massechutes, mayotte, mazingira, mbeya, meru, mexico, miami, micronesia, monaco-mongolia-montenegro, montserrat, morocco, mozambique-myanmar, mtwara, mwanza, namibia, nauru, nepal, netherlands, netherlands-antilles, nevada, new-caledonia, new-zealand, newyork, nicaragua, niger, nigeria, niue, north-macedonia, northern-mariana-islands, norway, oman, pakistan, palau, palestine, palestinian-territories, panama, papua-new-guinea, paraguay, peoples-democratic-republic, peru, philadhephia, philipians, Philippines, pitcairn-island, poland, politics, Portugal, puerto-rico, qatar, republic-of, republic-of-brazzaville, republic-of-south-korea, reunion-island, romania, Russia, russian-federation, rwanda, sahara-occidental, saint-kitts-and-nevis, saint-lucia, saint-vincent-and-the-grenadines, samoa, san-marino, sao-tome-and-principe, saudi-arabia, saudiarabia, scotland, Senegal, serbia, seychelles, sierra-leone, Singapore, singida, slovakia-slovak-republic, slovenia, solomon-islands, somalia, southafrica, spain, sri-lanka, sudan, suriname, swaziland-eswatini, sweden, switzerland, syria, syrian-arab-republic, tabora, taiwan-republic-of-china, tajikistan, tanzania, texas, thailand, the-gambia, tibet, timor-leste-east-timor, togo, tokelau, tonga, toronto, trinidad-and-tobago, tunisia, turkey, turkmenistan, turks-and-caicos-islands, tuvalu, uganda, united-arabs-emirates, united-kingdom, united-states, uruguay, uzbekistan, vancover, vanuatu, vatican-city-state-holy-see, venezuela, vietnam, virgin-islands-british, virgin-islands-u-s, wallis-and-futuna-islands, wallis-and-futuna-islands, wallis-et-futuna, washington-dc, western-sahara, yemen, zambia, zambie, zimbabwe
Discover more from cantonadigital
Subscribe to get the latest posts sent to your email.