Radio Fortune Africa -Ukweli na Burudani
https://zeno.fm/radio/radio-fortune-africa
Na Cantona Joseph Imechapishwa: March 25, 2026 04:27 (EAT)


Baraza la nchi wanachama za Umoja wa Mataifa, hivi leo litapiga kura kuhusu azimio lililowasilishwa na Ghana kuhusu kutambua biashara ya utumwa barani Afrika kama ‘uhalifu mkubwa dhidi ya binadamu’, azimio ambalo wanaharakati wanasema ni njia ya kuelekea uponyaji na haki.

Rais wa Ghana, John Mahama, mmoja ya viongozi wa Afrika ambaye amekuwa mstari wa mbele kupigia chapuo suala la fidia kwa wahanga wa biashara hiyo, alizuru makao makuu ya umoja wa Mataifa hapo jana kuzishawishi nchi wanachama katika tukio hili la kihistoria.
Rais Mahama, amewaambia wajumbe kuwa, azimio hili litaruhusu jumuiya ya kimataifa kuwajibika na kuwa mashahidi kwa wanawake, wanaume na watoto tu zaidi ya milioni 12.5 ambao jamii zao, majina, familia, ndoto, matumaini na maisha zilidhulumiwa katika kipindi cha miaka 400 iliyopita.
Rais Mahama alizinyooshea kidole nchi ambazo zinajaribu kuficha historia ya utumwa wa Afrika, ikiwemo Marekani ambayo hivi karibuni ilipiga marufuku vitabu vya historia ya utumwa ili watoto wasijue ukweli.
Licha ya upinzani toka kwa baadhi ya nchi, bara la Afrika limepata uungwaji mkono wa katibu mkuu wa umoja wa Mataifa, pamoja na nchi za Carribean.
Kenya: Miili 33 yafukuliwa kutoka kwa kaburi la pamoja Kericho

Nchini Kenya, karibia miili 33 imefukuliwa kutoka katika kaburi la pamoja katika kaunti ya Kericho kwenye mkoa wa bonde la ufa. Watu wawili wakiwa tayari wanashikiliwa na polisi wakuhusishwa na tukio hilo.
Miili hiyo inajumuisha watoto 25 nyengine nane ikiwa ni ya watu wazima kulingana na mamlaka kwenye eneo hilo.
Imeripotiwa kwamba baadhi ya miili hiyo ilikuwa imeanza kuoza wakati nyengine ikiwa bado, ishara kuwa huenda ilizikwa kwa nyakati tofauti.
Tayari miili hiyo imehifadhiwa kwenye makafani kwa uchunguzi zaidi kubaini sababu zilizopelekea izikwe kwenye kaburi la pamoja na ilitoka wapi.
Aidha zoezi la upasuaji linatarajiwa kufanyika kwenye miili hiyo kubaini namna watu hao walivyouawa au chanzo cha vifo vyao. Mwaka wa 2024, miili zaidi ya 400 ilifukuliwa kwenye msitu wa Shakahola kaunti ya Malindi pwani ya Kenya.
Uchunguzi wa polisi ulibaini kuwa watu hao walifariki baada yao kufunga kula chakula wakiwa na imani kwamba wangeenda mbinguni, uchunguzi zaidi ukibaini baadhi ya waliofariki waliuawa kwa kupigwa. Mchungaji wao Paul Mackenzie akiwa bado anashikiliwa na polisi.
afghanistan, africa, albania, algeria, America, american-samoa, andorra, angola, anguilla, antarctica, antigua-and-barbuda, argentina, armenia, aruba, arusha, australia, austria, azerbaijan, bahamas, bahrain, bangladesh, barbados, belarus, Belgium, belize, benin, bermuda, bhutan, bolivia, bosnia-and-herzegovina, botswana, Boukinafaso, brazil, brunei-darussalam, bulgaria, burkina-faso, burma, burundi, california, cambodia, cameroon, canada, cape-verde, cayman-islands, central-african-republic, Chad, chicago, chile, china, christmas-island, cocos-keeling-islands, colombia, comoros, congo, cook-islands, costa-rica, cote-divoire-ivory-coast, Croatia, cuba, cyprus, czech-republic, darsalaam, democratic-peoples-rep-north-korea, democratic-republic-of-the-congo-kinshasa, denmark, djibouti, dodoma, dominica, dominican-republic, dr-congo, dubai, east-timor-timor-leste, ecuador, egypt, egypty, el-salvador, england, equatorial-guinea, equitorial-guinea, eritrea, estonia, eswatini, ethiopia, falkland-islands, faroe-islands, federal-states-of-moldova, fiji, finland, Florida, france, french-guiana, french-polynesia, french-southern-territories, gabon, gaza, georgia, germany, ghana, gibraltar, goma, Greece, greenland, grenada, guadeloupe, guam, guatemala, guinea, guinea-bissau, guyana, habari, haiti, holy-see, honduras, hong-kong, houston, hungary, iceland, india, indonesia, Iowa, iran, iran-islamic-republic-of, iraq, ireland, israel, italia, italy, ivory-coast, jamaica, japan, jordan, karatu, kazakhstan, kilimanjaro, kinshasa, kiribati, kiswahili, korea, kosovo, kuwait, kyrgyzstan, lao, latvia-lebanon-lesotho-liberia-libya-liechtenstein-lithuania-luxembourg, Lebanon, liberia, macau, madagascar, malawi, malaysia-maldives, Mali, malta, marshall-islands-martinique-mauritania-mauritius, massechutes, mayotte, mazingira, mbeya, meru, mexico, miami, micronesia, monaco-mongolia-montenegro, montserrat, morocco, mozambique-myanmar, mtwara, mwanza, namibia, nauru, nepal, netherlands, netherlands-antilles, nevada, new-caledonia, new-zealand, newyork, nicaragua, niger, nigeria, niue, north-macedonia, northern-mariana-islands, norway, oman, pakistan, palau, palestine, palestinian-territories, panama, papua-new-guinea, paraguay, peoples-democratic-republic, peru, philadhephia, philipians, Philippines, pitcairn-island, poland, politics, Portugal, puerto-rico, qatar, Norrbottens lan, republic-of-brazzaville, republic-of-south-korea, reunion-island, romania, Russia, russian-federation, rwanda, sahara-occidental, saint-kitts-and-nevis, saint-lucia, saint-vincent-and-the-grenadines, samoa, san-marino, sao-tome-and-principe, saudi-arabia, saudiarabia, scotland, Senegal, serbia, seychelles, sierra-leone, Singapore, singida, slovakia-slovak-republic, slovenia, solomon-islands, somalia, southafrica, spain, sri-lanka, sudan, suriname, swaziland-eswatini, sweden, switzerland, syria, syrian-arab-republic, tabora, taiwan-republic-of-china, tajikistan, tanzania, texas, thailand, the-gambia, tibet, timor-leste-east-timor, togo, tokelau, tonga, toronto, trinidad-and-tobago, tunisia, turkey, turkmenistan, turks-and-caicos-islands, tuvalu, uganda, united-arabs-emirates, united-kingdom, united-states, uruguay, uzbekistan, vancover, vanuatu, vatican-city-state-holy-see, venezuela, vietnam, virgin-islands-british, virgin-islands-u-s, wallis-and-futuna-islands
All Rights Reserved © The Cantona Group PLC||2026
Discover more from cantonadigital
Subscribe to get the latest posts sent to your email.