Radio Fortune Africa -Ukweli na Burudani
https://zeno.fm/radio/radio-fortune-africa
Na Cantona Joseph Imechapishwa: March 23, 2026 14:19 (EAT)



Uhaba wa mafuta unaendelea kushuhudiwa kote nchini Kenya, huku wamiliki wa magari wakilalamikia kuwekwa kwa viwango vya ununuzi na ugumu wa kupata vituo vyenye mafuta.
Hali hii inajiri licha ya serikali kuwahakikishia wananchi kuwa akiba ya mafuta ya kitaifa inatosha. Hata hivyo, katika jiji la Nairobi, hususan barabara ya Lang’ata, vituo kadhaa vya mafuta vimeripotiwa kukosa mafuta.
“Nimezunguka vituo vya mafuta vitano ndipo nimepata mafuta hapa kwa kituo hiki. Ukweli ni kwamba hakuna mafuta,” alisema Marvin Ogeta, dereva wa teksi, akizungumza na vyombo vya habari. Aliongeza kuwa alipata kiasi kidogo cha mafuta katika kituo kimoja kilichopo barabara ya Lang’ata.
Ripoti zinaonyesha kuwa baadhi ya vituo vina upungufu mkubwa wa petroli, huku dizeli ikiwa ndiyo inayopatikana kwa kiasi fulani.
”Usiku wa Alhamisi nilikosa mafuta katika kituo cha mafuta cha springvalley jijini Nairobi na tulikuwa wengi sana, mmiliki wa gari aiambia BBC Swahili.
Wakati huohuo, hali hiyo imechochewa na shinikizo la soko la kimataifa, likihusishwa na vita vinavyoendelea nchini Iran na tishio la kufungwa kwa Mlango-Bahari wa Hormuz—njia muhimu ya usafirishaji wa mafuta duniani.
Wachambuzi wa sekta ya viwanda wanaonya kuwa gharama za usafirishaji huenda zikaongezeka maradufu, hali itakayoongeza presha kwa uchumi.
George Omuga, Mkurugenzi Mtendaji wa Shirikisho la Biashara la Afrika Mashariki, amesema kuwa vita hivyo vinaweza kuisababishia Kenya hasara ya zaidi ya asilimia 20 ya mauzo yake katika eneo la Mashariki ya Kati.
Aidha, sekta ya mauzo ya nje, hususan chai, inaweza kuathirika iwapo wanunuzi wakuu kutoka Iran, Pakistan na mataifa ya Ghuba watapunguza ununuzi wao.
Katika bandari ya Mombasa, matarajio ya hali kuwa nafuu bado ni madogo.
Kati ya takriban meli 60 zinazotarajiwa kuwasili ndani ya wiki mbili zijazo, ni meli chache tu zinazobeba bidhaa za mafuta, huku nyingi zikiwa zimebeba mizigo mingine kama kontena, chuma, magari, ngano na mbolea.
Mashambulizi ya Marekani na Israel yaendelea katika maeneo mbalimbali nchini Iran

Kumekuwa na ripoti nyingi za mashambulizi ya anga katika mji mkuu na miji mingine ya Iran. Picha na ushuhuda wa mashahidi zinaonyesha kuwa baadhi ya mashambulizi hayo yalilenga kumuua mtu mmoja au watu fulani mahsusi, huku pia kukiripotiwa milipuko mikubwa.
Milipuko imeripotiwa kusini mwa Iran, katika visiwa vya Kharg na Kish.
Aidha, milipuko kadhaa imesikika mjini Tehran, hasa katika eneo la jeshi la anga.
Wakati huo huo, Idara ya Mawasiliano ya Jeshi imesema kuwa jeshi la majini limeangamiza “ndege mbili zisizo na rubani za kivita za kujitoa muhanga” za Marekani katika eneo la Bandar Abbas.
Kwa upande mwingine, Press TV, kituo cha televisheni cha Kiingereza cha shirika la utangazaji la Iran, kimeripoti kuwa ndege ya kivita aina ya F-15 ya Marekani imeanguka nchini Kuwait. Video inayodaiwa kuonyesha tukio hilo pia imesambazwa.
Uchumi wa dunia uko katika “tishio kubwa” kutokana na mgogoro wa Mlango-Bahari wa Hormuz: Mkuu wa IEA

Uchumi wa dunia uko katika “tishio kubwa” kufuatia mgogoro wa nishati uliosababishwa na vita vya Mashariki ya Kati, na “hakuna nchi itakayokuwa salama” dhidi ya athari zake, amesema mkuu wa Wakala wa Kimataifa wa Nishati (IEA), Fatih Birol, siku ya Jumatatu.
Akizungumza katika Klabu ya Waandishi wa Habari ya Kitaifa katika mji mkuu wa Australia, Birol alifananisha mgogoro wa sasa wa nishati na ile ya miaka ya 1970 pamoja na athari za uvamizi wa Urusi dhidi ya Ukraine mwaka 2022.
“Kwa hali ilivyo sasa, mgogoro huu ni muunganiko wa migogoro miwili ya mafuta na anguko moja la gesi,” alisema Birol.
“Uchumi wa dunia unakabiliwa na tishio kubwa sana leo, na ninatumaini kwa dhati kuwa suala hili litapatiwa ufumbuzi haraka iwezekanavyo.
“Hakuna nchi itakayoweza kujiepusha na athari za mgogoro huu ikiwa utaendelea katika mwelekeo huu. Hivyo, kunahitajika juhudi za pamoja za kimataifa.”
Rais wa Marekani, Donald Trump, na Tehran wametoa vitisho vya kujibizana huku vita vikiingia wiki ya nne, ambapo rais huyo wa Marekani anaitaka Jamhuri ya Kiislamu kufungua tena Mlango-Bahari wa Hormuz uliokuwa umefungwa, njia muhimu ambayo takribani asilimia 20 ya usafirishaji wa mafuta na gesi duniani hupitia.
Kuzibwa kwa njia hiyo kumekaribia kusimamisha kabisa usafirishaji wa mafuta kupitia mkondo huo mwembamba wa bahari.
Bei ya mafuta ilipanda tena mapema Jumatatu, huku mafuta ghafi ya kiwango cha Marekani yakifikia kwa muda mfupi dola 100 kwa pipa.
Birol aliieleza vyombo vya habari vya Australia kuwa angalau miundombinu 40 ya nishati katika eneo hilo “imeharibiwa vibaya au kwa kiwango kikubwa sana” kutokana na mzozo huo.
afghanistan, africa, albania, algeria, America, american-samoa, andorra, angola, anguilla, antarctica, antigua-and-barbuda, argentina, armenia, aruba, arusha, australia, austria, azerbaijan, bahamas, bahrain, bangladesh, barbados, belarus, Belgium, belize, benin, bermuda, bhutan, bolivia, bosnia-and-herzegovina, botswana, Boukinafaso, brazil, brunei-darussalam, bulgaria, burkina-faso, burma, burundi, california, cambodia, cameroon, canada, cape-verde, cayman-islands, central-african-republic, Chad, chicago, chile, china, christmas-island, cocos-keeling-islands, colombia, comoros, congo, cook-islands, costa-rica, cote-divoire-ivory-coast, Croatia, cuba, cyprus, czech-republic, darsalaam, democratic-peoples-rep-north-korea, democratic-republic-of-the-congo-kinshasa, denmark, djibouti, dodoma, dominica, dominican-republic, dr-congo, dubai, east-timor-timor-leste, ecuador, egypt, egypty, el-salvador, england, equatorial-guinea, equitorial-guinea, eritrea, estonia, eswatini, ethiopia, falkland-islands, faroe-islands, federal-states-of-moldova, fiji, finland, Florida, france, french-guiana, french-polynesia, french-southern-territories, gabon, gaza, georgia, germany, ghana, gibraltar, goma, Greece, greenland, grenada, guadeloupe, guam, guatemala, guinea, guinea-bissau, guyana, habari, haiti, holy-see, honduras, hong-kong, houston, hungary, iceland, india, indonesia, Iowa, iran, iran-islamic-republic-of, iraq, ireland, israel, italia, italy, ivory-coast, jamaica, japan, jordan, karatu, kazakhstan, kilimanjaro, kinshasa, kiribati, kiswahili, korea, kosovo, kuwait, kyrgyzstan, lao, latvia-lebanon-lesotho-liberia-libya-liechtenstein-lithuania-luxembourg, Lebanon, liberia, macau, madagascar, malawi, malaysia-maldives, Mali, malta, marshall-islands-martinique-mauritania-mauritius, massechutes, mayotte, mazingira, mbeya, meru, mexico, miami, micronesia, monaco-mongolia-montenegro, montserrat, morocco, mozambique-myanmar, mtwara, mwanza, namibia, nauru, nepal, netherlands, netherlands-antilles, nevada, new-caledonia, new-zealand, newyork, nicaragua, niger, nigeria, niue, north-macedonia, northern-mariana-islands, norway, oman, pakistan, palau, palestine, palestinian-territories, panama, papua-new-guinea, paraguay, peoples-democratic-republic, peru, philadhephia, philipians, Philippines, pitcairn-island, poland, politics, Portugal, puerto-rico, qatar, Norrbottens lan, republic-of-brazzaville, republic-of-south-korea, reunion-island, romania, Russia, russian-federation, rwanda, sahara-occidental, saint-kitts-and-nevis, saint-lucia, saint-vincent-and-the-grenadines, samoa, san-marino, sao-tome-and-principe, saudi-arabia, saudiarabia, scotland, Senegal, serbia, seychelles, sierra-leone, Singapore, singida, slovakia-slovak-republic, slovenia, solomon-islands, somalia, southafrica, spain, sri-lanka, sudan, suriname, swaziland-eswatini, sweden, switzerland, syria, syrian-arab-republic, tabora, taiwan-republic-of-china, tajikistan, tanzania, texas, thailand, the-gambia, tibet, timor-leste-east-timor, togo, tokelau, tonga, toronto, trinidad-and-tobago, tunisia, turkey, turkmenistan, turks-and-caicos-islands, tuvalu, uganda, united-arabs-emirates, united-kingdom, united-states, uruguay, uzbekistan, vancover, vanuatu, vatican-city-state-holy-see, venezuela, vietnam, virgin-islands-british, virgin-islands-u-s, wallis-and-futuna-islands
All Rights Reserved © The Cantona Group PLC||2026
Discover more from cantonadigital
Subscribe to get the latest posts sent to your email.