Radio Fortune Africa -Na Cantona Joseph
https://zeno.fm/radio/radio-fortune-africa

Israel yafanya uvamizi viungani mwa miji ya na Homs na Latakia nchini Syria

Israel imeanzisha mashambulizi ya anga Jumatatu jioni viungani mwa miji ya Homs na Latakia, nchini Syria, rasmi za vyombo vya habari vya Syria zimesema.
Uvamizi wa Israel ulilenga eneo la Maskana viungani mwa Homs.
Mashambulizi kama hayo ya ndege pia yalilenga maeneo ya karibu na eneo la Saqoubin nje kidogo ya Latakia, lakini hakuna hasara iliyoripotiwa, kulingana na shirika la habari la Syria, ambalo lilithibitisha kuwa magari ya zima moto yalitumwa kwenye eneo la shambulio hilo.
Kwa upande wake, Shirika la uangalizi wa haki za inadamu la Syria limeripoti kuwa “ndege za kivita za Israel zilifanya shambulizi la anga zikilenga kikosi cha anga kilichoko kusini mashariki mwa mji wa Homs. Milipuko mikubwa ilisikika katika eneo lililolengwa, huku kukiwa na ripoti za awali za uharibifu wa mali.”
Wizara ya mambo ya nje ya Syria ililaani “uvamizi wa anga unaofanywa na vikosi vya Israel vinavyokalia kwa mabavu,” kama ilivyoeleza, na kuyataka kama “ukiukaji wa wazi” wa sheria za kimataifa na kanuni za Mkataba wa Umoja wa Mataifa.
Ilisema kuwa uvamizi huu “ni sehemu ya mfululizo wa mashambulizi ya kichokozi yanayofuatiliwa na Israeli dhidi ya ardhi ya Syria.
Israel imeanzisha mashambulizi ya anga Jumatatu jioni viungani mwa miji ya Homs na Latakia, nchini Syria, rasmi za vyombo vya habari vya Syria zimesema.
Ufaransa katika mzozo mpya wa kisiasa baada ya wabunge kumtimua waziri mkuu

Ufaransa imetumbukia katika mzozo mpya wa kisiasa baada ya kushindwa kwa Waziri Mkuu François Bayrou katika kura ya imani katika Bunge la taifa.
Kushindwa kwa Bayrou kwa kura 364 dhidi ya 194 kunamaanisha kwamba Jumanne atawasilisha barua ya kujiuzulu kwa serikali yake kwa Rais Emmanuel Macron, ambaye lazima sasa aamue kuhusu hatua zitakazofuata. Ofisi ya Macron ilisema hii itafanyika “katika siku zijazo”.
Hatua zitakazochukuliwa na kumtaja waziri mkuu mpya kutoka mrengo wa kulia wa kati; kuelekea kushoto na kutafuta jina linaloendana na Chama cha Kisoshalisti; na kuvunja bunge ili uchaguzi mpya ufanyike.
Maadui wakubwa wa Macron katika chama cha mrengo wa kushoto cha France Unbowed wanamtaka yeye binafsi kujiuzulu, lakini wachambuzi wachache wanafikiri hilo linawezekana.
Kwa hivyo Ufaransa iko njiani kupata waziri mkuu wa tano katika kipindi cha chini ya miaka miwili, rekodi mbaya ambayo inadhihirisha kuyumba na kutoridhika na Macron ambako kumetawala katika muhula wa pili wa rais nchini Ufaransa.
All Rights Reserved © The Cantona Group PLC||2025
Discover more from cantonadigital
Subscribe to get the latest posts sent to your email.