Changamoto inayowakabili walemavu wa ngozi.

Na Cantona Joseph 14 Juni 2024

Jinsi walemavu wa ngozi wanavyokabiliana na changamoto za kila siku

Jinsi walemavu wa ngozi wanavyokabiliana na changamoto za kila siku

Takwimu zinaonyesha kuwa mtu mmoja katika kila watu 5,000 Afrika Kusini mwa Jangwa la Sahara anaishi na ulemavu wa ngoziMali Albino / Picha: AP

Vitendo vya kudharauliwa dhidi ya watu wenye ulemavu wa ngozi vimehusishwa na baadhi ya jamii, hasa barani Afrika.

Hata hivyo, hadithi ya Muse Brothers haisimuliwi mara nyingi.

George na Willie Muse walikuwa ni Wamerikani-Waafrika waliokuwa na ulemavu wa ngozi.

Walitekwa nyara wakiwa wavulana huko Truevine, Virginia mwaka 1899, na walitumiwa kwa maonyesho ya sarakasi hadi 1927.

Walivyozaliwa

Ndugu hao, ambao walivumilia majina ya kudhalilisha, walifanywa kama maonesho na karagosi na kutumiwa kwa ajili ya kupata hela.

Hii ni dhuluma ambayo imekuwepo kwa miaka mingi dhidi ya watu wenye ulemavu wa ngozi.

Ualbino unatokana na neno la Kilatini “albus” linalomaanisha “nyeupe.”

Hali hii ni ya kurithi, inamaanisha ipo tangu kuzaliwa. Ualbino ni matokeo ya kupungua au kutokuwepo kwa melanini kwenye ngozi, nywele na macho.

MALAWI watu wenye ulemavu wa ngozi

Walioko hatarini zaidi

Hii inawaacha watu wenye ualbino wakiwa na hatari zaidi ya athari za jua kali.

Takwimu zinaonyesha kuwa mtu mmoja kati ya kila 5,000 katika Afrika Kusini mwa Jangwa la Sahara anaishi na ualbino. Umoja wa Mataifa unasema kwamba mtu mmoja kati ya kila 20,000 barani Ulaya na Amerika Kaskazini ana hali hiyo.

Donald Tampi Bagas ni raia wa Nigeria ambaye alizaliwa na ualbino. Kuishi na hali hiyo “haikuwa tatizo kubwa” kwake, isipokuwa kwa kuona kidogo wakati wa mchana, na unyanyapaa wa mara kwa mara.

Alizaliwa na kukulia katika jimbo la Nasarawa, katikati ya Nigeria. Wazazi wake walimsaidia katika utoto wake mwishoni mwa miaka ya 1980 na 1990.

MALi watu wenye ulemavu wa ngozi

Mwanga mkali

Kijana huyo mwenye umri wa miaka 35, alishinda unyanyapaa unaohusishwa na ulemavu wa ngozi. Leo, anafanya kazi katika mji mkuu Abuja kwa shirika linalotafuta kuwawezesha watu wanaoishi na ulemavu.

Huko Zimbabwe, mtu mmoja kati ya kila 1,000 anaishi na ualbino, wakati huko Tanzania, mtu mmoja kati ya kila 1,400 anaishi na hali hiyo.

Huko Afrika Kusini, mtu mmoja kati ya kila 3,900 wa rangi anaishi na ualbino.

Karibu watu wote wenye hali hiyo wana matatizo ya kuona, kwani mwanga mkali unawaathiri sana.

Shughuli za kawaida

MALAWI- mtoto mwenye Ulemavu wa ngozi

“Mionzi ya jua kali inanifanya nisiwe na raha. Hakuna kitu naweza fanya kubadilisha hali hiyo, na nimejifunza kuishi nayo,” Bagas wa Nigeria arifu wanahabari.

“Nilivyokuwa mtoto, sikupenda makusanyiko ya wanafunzi kwa sababu jua liliathiri kuona kwangu.”

Changamoto za kuona pia ziliathiri shughuli zake za kawaida kama mtoto, ikiwa ni pamoja na kucheza mpira wa miguu.

“Singeweza kuona vitu vilivyo mbali. Hii ilinilazimisha kukaa viti vya mbele darasani,” anakumbuka.

Bagas anasema unyanyapaa unaohusishwa na ualbino ulimfanya ajiunge na TAF Africa, shirika lisilo la kiserikali ambalo linaongeza uelewa kuhusu ualbino, na kutafuta kujumuishwa kwao katika nafasi za kufanya maamuzi.

Katika baadhi ya nchi, idadi kubwa ya watu wenye ualbino hufa kutokana na saratani ya ngozi kati ya miaka 30 na 40, Umoja wa Mataifa unasema.

TAF Africa imesaidia Nigeria kuja na sera zinazoongeza uelewa kuhusu haki za watu wenye ulemavu wa ngozi.

“Katika shughuli zao za kila siku, watu wanaoishi na ualbino wanakabiliwa na jua. Baadhi yao hawajui la kufanya kujikinga na mionzi kali. Tunahitaji kuwaelimisha jinsi ya kulinda afya zao,” Bagas anasema.

Jamii ‘inahitaji kuhamasishwa’

Watu wenye albino hushiriki katika ukurasa wa kike na wa kiume huko Afrika Kusini. / Picha: AP

Anaongeza kuwa jamii kwa ujumla pia inahitaji kuhamasishwa jinsi ya kuwatendea haki watu wenye ualbino.

Katika baadhi ya jamii, watu wenye ulemavu wa ngozi wanakabiliwa na changamoto za kimwili na kihisia, na hata mauaji ya kitamaduni.

ubaguzi dhidi ya watu wanaoishi na ualbino hauna nafasi katika jamii.Umoja wa Mataifa

Jake Epelle, mkurugenzi mtendaji wa TAF Africa, aliipongeza tume ya uchaguzi ya Nigeria kwa kutoa miwani 20,000 inayoongeza ukubwa katika uchaguzi wa 2023 kusaidia watu wenye matatizo ya kuona, pamoja na wale wanaoishi na ualbino.

‘Mabadiliko ya vitendo’

Siku ya Ualbino Duniani huadhimishwa Juni 13 kila mwaka.

UN inasema mabadiliko ya vitendo katika jamii bado yanahitajika ili kuhakikisha watu wanaoishi na ualbino wanafura

Habari zinazohusiana

Kwanini harakati za mapinduzi ya serikali zinaongezeka Afrika

Kwanini harakati za mapinduzi ya serikali zinaongezeka Afrika

Mali, Guinea, Burkina Faso na Sudan ziko chini ya uongozi wa kijeshi

Hali ya mapinduzi ya  Niger inavyoendelea katika eneo la Afrika Magharibi

Hali ya mapinduzi ya  Niger inavyoendelea katika eneo la Afrika Magharibi

Mapinduzi ya Niger ya hivi karibuni ambayo ni zaidi katika mfululizo wa mashambulizi ya kijeshi huko Afrika Magharibi yakiibua maswali mengi kuhusu mustakabali wa eneo hilo katika masuala ya demokrasia, usalama na maendeleo ya kiuchumi.

Traore wa Burkina Faso: Kutajwa, kusifiwa na kukua kwa rais kijana zaidi duniani.

Traore wa Burkina Faso: Kutajwa, kusifiwa na kukua kwa rais kijana zaidi duniani.

Akiwa na umri wa miaka 35, Ibrahim Traore wa Burkina Faso ndiye rais mwenye umri mdogo zaidi duniani, na gumzo la duniani kote.

Mahakama ya Kimataifa ya Jinai na Utawala wa Magharibi dhidi ya Afrika

Mahakama ya Kimataifa ya Jinai na Utawala wa Magharibi dhidi ya Afrika

Kwa Miaka mingi Mahakama ya Kimataifa ya Jinai ya ICC imejikita zaidi katika uhalifu unaodaiwa kufanywa na baadhi ya viongozi wa Afrika huku ikizingatia kidogo au kutozingatia kabisa jinai zinazohusishwa na viongozi wa Magharibi

Makala yanayovuma katika kategoria hii

Uonevu mtandaoni: Kwa nini Afrika inahitaji kuchukua hatua sasa

Uonevu mtandaoni: Kwa nini Afrika inahitaji kuchukua hatua sasa

Unyanyasaji mtandaoni umeongezeka kote barani Afrika na ufikiaji mkubwa wa teknolojia na kuenea kwa majukwaa ya mitandao ya kijamii na programu zinazoruhusu kutokujulikana, mara nyingi huwafanya waathiriwa kukata tamaa

Uchaguzi Mkuu wa Afrika Kusini: Viongozi wa vyama

Uchaguzi Mkuu wa Afrika Kusini: Viongozi wa vyama

Mnamo Mei 29, 2024, Afrika Kusini itakuwa na uchaguzi mkuu, hatua muhimu katika historia ya kidemokrasia ya nchi hiyo. Tangu kumalizika kwa utawala wa weupe wachache mwaka 1994, nchi hii imefanya uchaguzi mara saba

Ombi la mwendesha mashtaka wa ICC: Netanyahu wa Israel atakamatwa?

Ombi la mwendesha mashtaka wa ICC: Netanyahu wa Israel atakamatwa?

Hatua ya mahakama ya ICC kutafuta vibali vya kukamatwa kwa Waziri Mkuu wa Israel Benjamin Netanyahu, mkuu wake wa ulinzi Yoav Gallant na viongozi watatu wa Hamas inaashiria wakati mgumu katika historia ya mahakama ya kimataifa ya uhalifu.

Uchaguzi wa Afrika Kusini 2024: Ramaphosa, ANC hali ya sintofahamu ya uchaguzi

Uchaguzi wa Afrika Kusini 2024: Ramaphosa, ANC hali ya sintofahamu ya uchaguzi

Cyril Ramaphosa anakadiria matumaini juu ya mustakabali wa Afrika Kusini licha ya kupungua kwa umaarufu wa chama tawala kutokana na kiwango kikubwa cha ukosefu wa ajira, matatizo ya nishati ya muda mrefu na kashfa za rushwa

Nini kingine ungependa kujua?

Vile vile

Kwanini harakati za mapinduzi ya serikali zinaongezeka Afrika

Kwanini harakati za mapinduzi ya serikali zinaongezeka Afrika

Hali ya mapinduzi ya  Niger inavyoendelea katika eneo la Afrika Magharibi

Hali ya mapinduzi ya  Niger inavyoendelea katika eneo la Afrika Magharibi

Traore wa Burkina Faso: Kutajwa, kusifiwa na kukua kwa rais kijana zaidi duniani.

Traore wa Burkina Faso: Kutajwa, kusifiwa na kukua kwa rais kijana zaidi duniani.

Mahakama ya Kimataifa ya Jinai na Utawala wa Magharibi dhidi ya Afrika

Mahakama ya Kimataifa ya Jinai na Utawala wa Magharibi dhidi ya Afrika

Mapitio ya Afrika 2023: Kuondoka kwa wanajeshi wa UN, vikosi vya Ufaransa

Mapitio ya Afrika 2023: Kuondoka kwa wanajeshi wa UN, vikosi vya Ufara

Katika Picha: Vijana waliochoshwa na vita DRC wapata faraja mchezo wa kuteleza

DRC: Jeshi la Kongo lataka ushirikiano wa raia ili kuwadhibiti wanamgAMbo.

Tovuti hii hutumia vidakuzi. Kwa kuendelea kuangalia tovuti hii, unakubaliana na utumizi wa vidakuzi.Sera ya Vidakuzi.

OUR PRODUCTS:
Cantona Digital
Queens Safaris
SkizaRecords
FBE Records
FBE Photography
FBE Brands& Events Management Ltd

Let’s do Business/Let’s Build Brands.

Build Brands for Generations.

All Rights|Reserved ©|Cantona Group Ltd


Discover more from cantonadigital

Subscribe to get the latest posts sent to your email.

Leave a comment