Kenya yajikwaa kwenye tenisi.

Tenisi: Kenya yajikwaa kupandishwa daraja ya Billie Jean kwa kichapo cha Nigeria

Nairobi, Kenya – Nigeria iliishinda Kenya mechi 2-1 siku ya Alhamisi na kupata faida ya mapema katika mbio za kupandishwa daraja.

Kwa mwaka wa pili mfululizo, matumaini ya Kenya kupandishwa daraja kutoka kundi la tatu hadi la pili katika Kombe la Billie Jean King yalipata kipigo mikononi mwa Nigeria ambao waliwasababishia kichapo cha mechi 2-1 dhidi ya wenyeji wa michuano hiyo ya 2024 inayofanyika katika uwanja wa Nairobi Club jijini Nairobi nchini Kenya.

Kenya ilikuwa imepoteza mechi ya ufunguzi wakati Barakat Quadre Oyinlomo alitumia dakika 57 tu kumlaza Alicia Owegi kwa ushindi wa seti 2-0 za 6-0, 6-1. Ila baadaye bingwa wa Afrika Angella Okutoyi alirejesha usawa kwa nchi yake kwa kumchapa Adesuwa Osabuohien 6-3, 6-3 ili kuhakikisha usawa huo ungehitaji kuamuliwa katika mechi ya wachezaji wawili kila upande (doubles).

Nahodha wa timu ya Kenya, Francis Rogoi alichagua kuchezesha Okutoyi na pacha wake Roselida Asumwa kwa matumaini kwamba wawili hao wataibeba timu hiyo kwenye mechi muhimu huku Nigeria ikiendelea na ushirikiano wa Adesuwa na Barakat.

Roselida Asumwa wa Kenya
Roselida Asumwa wa Kenya @Lens Eye Images Limited

Baada ya kuanza vizuri katika dakika za ufunguzi leo, Kenya ilitengeneza nafasi ya kwanza ya kupata alama katika mechi ya tatu lakini Nigeria wakazima hatari hiyo haraka kwa kurejea mchezoni.

Ghafla bin vu, Kenya ilibadilisha mkondo wa kushambulia na kuanza kushambuliwa meza zikibadilika katika mchezo uliofuata huku Nigeria ikibadilisha pointi yake ya kwanza ya mapumziko katika seti na kuongoza 3-1.]

Hata hivyo, wenyeji, wakiungwa mkono na sehemu kubwa ya mashabiki, walirudi wakichaji mara moja huku wakifanikiwa kupata mapumziko ya alama.

Adesuwa Osabouhien wa Nigeria
Adesuwa Osabouhien wa Nigeria © Tennis Kenya

Nigeria hata hivyo walifanikiwa kumenyana na Kenya kwa mara nyingine katika mchezo wa nane walipoongoza kwa alama 5-3 katika mara ya pili ya kubisha huu Asumwa akihangaika kwenye kupakua mipira ya kwanza.

Wenyeji hao wa Afrika Magharibi walifanikiwa kuchukua seti ya kwanza 6-3. Seti ya pili ilionyesha ushindani mkali huku Kenya ikiazimia kutopoteza bila ya kuonyesha makucha yake.  

Walipata mwanzo mzuri walipoiyumbisha Nigeria katika mchezo wa pili lakini hawakuweza kuvumilia na hali hiyo ilitokea walipofanikiwa kupenya tena katika mchezo wa sita, na kulazimisha mechi hiyo kwa sare ya bila kufungana ambayo Nigeria ilishinda 7-5 na kuchukua hatua muhimu kwenye harakati ya kupandishwa daraja.

“Kujitayarisha vyema kisaikolojia kulichangia, tulipanga sehemu maalum ya kupiga mipira, namna ya kupakua na wachezaji kujiamini,” alifichua kocha wa Nigeria, Rotimi Akinloye.

Nahodha wa Kenya, Francis Rogoi wakati wa mechi dhidi ya Nigeria
Nahodha wa Kenya, Francis Rogoi wakati wa mechi dhidi ya Nigeria @Lens Eye Images Limited

“Imekuwa siku ngumu katika michezo kwetu. Tulitoka 0-1 kwenye mechi ya kwanza lakini tuliweza kurejea na kuwa 1-1. Mechi ya mwisho ambayo ilikuwa ya maamuzi ilikuwa na changamaoto kidogo na shinikizo na mipira michache ilitugharimu mechi ili tupate matokeo,” kocha wa Kenya Francis Rogoi alikadiria.

“Kucheza na wenyeji si rahisi, tulijua watakua na presha kwa hivyo tukajituma zaidi na mwishowe tumepata matokeo bora,” aliongeza kocha Akinloye.

Fuatilia habari zote za kimataifa kwa kupakua App ya RFI

“Inapendeza sana, tulikuja kushinda. Mwaka jana tulipoteza mechi kadhaa na tulijifunza, mwaka huu tunayafanyia kazi,” alisema kwa furaha Barakat Oyinlomo.

Hata hivyo, bado hatujapoteza matumaini, mwaka jana tuliifunga Morocco mechi ya kwanza lakini wao ndio waliofuzu. Kwa hivyo mchezo bado unaendelea na mechi za mchujo katika kundi lolote hutokea na tunataka kupata ahueni na kujiandaa vyema. Ikiwa tutaweza kufanya makubwa Jumamosi basi kila kitu kitakuwa sawa,” Rogoi alisema na matumaini makubwa.

Barakat Quadre Oyinlomo wa Nigeria
Barakat Quadre Oyinlomo wa Nigeria © Tennis Kenya

Kenya itakuwa na siku ya mapumziko Ijumaa huku Nigeria ikichuana na Afrika Kusini.

“Afrika Kusini! Lazima tumakinike asilimia mia, nguvu zetu ziwe juu,” alisema Adesuwa.

Kenya itahitaji Afrika Kusini kuiadhibu Nigeria kwa kipigo kikubwa ili kupata nafasi yoyote ya kupandishwa daraja watakapochuana na Afrika Kusini siku ya Jumamosi.

Kusambaza :

Soma zaidi mada inayofanana:

Kuhusu mada hiyohiyo

Cynthia Cheruto na Angella Okutoyi wa Kenya

BILIE JEAN KING CUP

 

Tenisi: Kenya yajikwaa kupandishwa daraja ya Billie Jean kwa kichapo cha Nigeria

Kocha wa Borussia Dortmund Edin Terzic (kulia), na kocha wa PSG Luis Enrique (kushoto).

Ujerumani: Terzic anaondoka kwenye wadhifa wake kama kocha wa Borussia Dortmund

Timu ya raga ya taifa la kenya, kinadada Lionesses baada ya kumaliza mazoezi ya asubuhi katika uwanja wa Kasarani jijini Nairobi.

Kenya: Lionesses kutafuta tiketi ya Olimpiki katika mashindano ya Repechage

Angella Okutoyi wa Kenya akisherekea kufunga pointi kwenye mechi yake dhidi ya Sada Nahimana wa Burundi

BILIE JEAN KING CUP

Tenisi: Kenya, Afrika Kusini na Nigeria zafuzu mchujo wa Billie Jean King Cup

Kocha mkuu wa klabu ya Real Madrid Carlo Ancelotti.

Ancelotti: Real Madrid haitashiriki michuano mipya ya klabu bingwa ya dunia

Mchezaji tenisi kutoka Italia Jannik Sinner, aliye hapa Roland-Garros mnamo Juni 4, 2024, ametangazwa rasmi kuwa nambari moja duniani katika viwango vya ATP mnamo Jumatatu Juni 10, 2024.

Tenisi: Jannik Sinner anakuwa mchezaji wa kwanza wa Italia nambari moja katika historia

Picha kutoka maktaba: Wachezaji wa timu ya taifa ya Cameroon wakishangilia wakati wa mechi za fainali za kombe la mataifa ya Afrika zilizofanyika Ivory Coast. Januari 23, 2024.

Kenya, DRC kabaruani, Cameroon yafanya kweli mechi za kufuzu kombe la dunia la FIFA

Wachezaji wa timu ya taifa ya Rwanda wakati wa mechi ya kufuzu kwa kombe la dunia.

Rwanda yapoteza ugenini, mechi za kufuzu fainali za kombe la dunia

Mchezaji wa timu ya taifa ya Senegal na mwenzake wa Cameroon wakati wa mechi ya awali.

Mechi za mataifa ya Afrika kufuzu kwa kombe la dunia zinaendelea

Timu ya Kenya ya raga wakipokezwa hundi ya dola elfu 43 na waziri wa michezo Ababu Namwamba

KENYA RAGA

Kenya 7s yatuzwa kibabe huku ikilenga maandalizi ya Olimpiki

Mshambuliaji Kylian Mbappé akiwa na timu ya Ufaransa dhidi ya Gibraltar mjini Nice, Novemba 18, 2023.

Kandanda: Mshambulizi wa Ufaransa Kylian Mbappé hatimaye ajiunga na klabu ya Real Madrid

Mwanasoka wa zamani na rais wa sasa wa Shirikisho la Soka la Cameroon, Samuel Eto'o, wakati wa mazoezi ya mwaka 2022 huko Doha wakati wa Kombe la Dunia nchini Qatar.

Ndtoungou Mpilé na David Pagou wakataa uteuzi wa Samuel Eto’o

Wachezaji wa Ahly wakishangilia bao la kwanza la timu yao wakati wa mchezo wa mkondo wa pili wa fainali ya Ligi ya Mabingwa Afrika kati ya Al-Ahly Tunis na Esperance Sportive de Tunis kwenye uwanja wa kimataifa wa Cairo Mei 25, 2024.

Timu ya Al Ahly ya Misri yashinda tena Ligi ya

OUR PRODUCTS:
Cantona Digital
Queens Safaris
SkizaRecords
FBE Records
FBE Photography
FBE Brands& Events Management Ltd

Let’s do Business/Let’s Build Brands.

Build Brands for Generations.

All Rights|Reserved ©|Cantona Group Ltd


Discover more from cantonadigital

Subscribe to get the latest posts sent to your email.

Leave a comment