Unapokubali kupitishwa jangwani unaandaliwa kuwa mtu bora.

Ni rahisi zaidi ngamia kupenya tundu la sindano, kuliko tajiri kuingia katika ufalme wa Mungu.Neno hili linatafsiriwa tofauti sana,lakini maana ya neno hilo ni hii hapa tajiri anayezungumzwa hapo ni mtu yule ambaye ameridhika kwenye mambo ya Mungu,anaweza akawa kanisani neno la Mungu linahubiriwa yeye anaona halimuhusu hata muda wa maombi yeye anaondoka anajiona hana haja ya kuomba,hata kutubu hawezi anasema yeye hana dhambi.Kwenye kila jambo la Mungu yeye ni mbishi na kujiona anajua kuliko mtu mwingine mtu huyu ni tajiri ambaye neno lina mzungumzia lakini ngamia ni yule ambaye ni mpole kila analoambiwa analitunza ili liweze kumsaidia baadae ni kama ngamia atunzapo maji kwenye nundu yake,pia ni mvumilivu hukubali kupitishwa jangwani yaani kwenye majaribu ili awe bora zaidi sio mtu wa kukata tamaa watu hawa ni rahisi kupenya na kuuona ufalme wa Mungu.

Tambua kama Biblia ingemaanisha Tajiri hawezi ingia mbinguni basi Mungu asinge kuwa ameweka baraka juu yetu na wala nisingekuwa natamka baraka juu ya watu wake.Nakuombea leo ujitenge na kukaa mbali na matajiri ili uweze kuona baraka za Mungu juu ya maisha yako.

#Iposiku #Getinspired #CantonaJosephMotivates

All rights reserved©2019


Discover more from cantonadigital

Subscribe to get the latest posts sent to your email.

Leave a comment