DRC: Moïse Katumbi aonya kuhusu marekebisho ya katiba

Radio Fortune Africa -Ukweli na Burudani

https://zeno.fm/radio/radio-fortune-africa

Na Cantona Joseph Imechapishwa : March 30, 2026 07:37 (EAT)

Vocalize Pre-Player Loader

Kiongozi wa upnzani nchini DRC, Moïse Katumbi Chapwe amevunja ukimya wake. Moïse Katumbi ambaye ni mmoja wa wapinzani wakuu wa kisiasa wa rais Félix Tshisekedi pia amepinga wazo la mageuzi ya katiba, wazo linaloungwa mkono sana na wanasiasa kadhaa ndani ya kambi ya rais ambao wanakubali waziwazi nia yao ya kumshawishi rais Tshisekedi kuelekea muhula wa tatu.

Makao makuu ya bunge la taifa la DRC, huko Kinshasa, Februari 2, 2023.
Makao makuu ya bunge la taifa la DRC, huko Kinshasa, Februari 2, 2023. © Alexis Huguet / AFP

Moïse Katumbi anavunja ukimya wake na kuanza tena mashambulizi yake ya kisiasa, kama alivyofanya mwaka wa 2015, dhidi ya jaribio lolote la marekebisho ya katiba. Moïse Katumbi, kiongozi wa chama cha Ensemble pour la République, anaionya serikali dhidi ya marekebisho yoyote ya katiba yaliyopendekezwa ambayo yanaweza kufungua njia kwa muhula wa tatu wa Rais Félix Tshisekedi.

Moïse Katumbi, anasema mageuzi haya yatakuwa usaliti. Anasema kwamba Félix Tshisekedi mwenyewe alikuwa sehemu ya mapambano dhidi ya mageuzi haya miaka kumi iliyopita, wakati Joseph Kabila alipokuwa madarakani.

“Sio kwa sababu ya Katiba kwamba hatuna mwelekeo tena, kwamba watumishi wa umma wanalipwa vibaya, kwamba watoto wanakufa kwa njaa, au kwamba hakuna kazi,” anadai. Kauli hii inakuja huku maaskofu kutoka kanisa Katoliki pia wakishauri dhidi ya mpango wowote kama huo, wakibaini kwamba unaweza kuzidisha mgogoro wa usalama.

Wito wa kuwa makini

Hivyo, Moïse Katumbi hana shaka. “Hali ni nzito,” anasema, huku akitaka umakini mkubwa dhidi ya mpango wowote unaolenga kurekebisha Katiba.

“Ninawasihi raia wa Kongo kuwa macho na kusema hapana kwa mabadiliko haya ya katiba. Tunahitaji amani katika nchi yetu, tunahitaji umoja wa nchi yetu.” “Tuwe tayari; lazima tujilinde ili Katiba yetu isifanyiwe marekebisho. Tuna Katiba bora zaidi duniani,” anadai.

Kulingana na Moïse Katumbi, mgogoro ambao nchi inapitia si kutokana na Katiba, bali ni kwa serikali ya sasa. Anamwambia rais Félix Tshisekedi moja kwa moja, akikumbusha mapambano yao ya pamoja dhidi ya marekebisho yoyote ya katiba chini ya utawala uliopita.

“Fikiria mateso ya raia. Hatutakubali kamwe mabadiliko ya Katiba, hasa kama yatatoka kwako; yatakuwa usaliti kwa raia wa Kongo,” anaonya.

Mkakati wa upinzani

Mkakati wa upinzani sasa umepangwa kwa kuzingatia nguzo nne, kama Olivier Kamitatu, msemaji wa Moïse Katumbi, anavyobainisha: “1: Kuongeza uelewa wa umma, 2: Kuunganisha upinzani, zaidi ya mgawanyiko wa sasa, kwa kuzingatia kanuni rahisi: heshima kwa Katiba. 3: Kutumia mifumo yote ya kidemokrasia na mashirika ya kiraia. Na hatimaye, 4: Upande wazi wa kidiplomasia: kuwaonya washirika wetu wote na kutoa wito wa vikwazo vinavyolengwa dhidi ya jaribio lolote la kupinga Katiba iliyopitishwa na 85% ya raia wa Kongo.”

Moïse Katumbi anatetea kipaumbele kingine: kufungua mazungumzo ili kukomesha vurugu Mashariki  ya Kongo na kufanya kazi kuelekea kuungana tena kwa nchi.

afghanistanafricaalbaniaalgeriaAmericaamerican-samoaandorraangolaanguillaantarcticaantigua-and-barbudaargentinaarmeniaarubaarushaaustraliaaustriaazerbaijanbahamasbahrainbangladeshbarbadosbelarusBelgiumbelizebeninbermudabhutanboliviabosnia-and-herzegovinabotswanaBoukinafasobrazilbrunei-darussalambulgariaburkina-fasoburmaburundicaliforniacambodiacamerooncanadacape-verdecayman-islandscentral-african-republicChadchicagochilechinachristmas-islandcocos-keeling-islandscolombiacomoroscongocook-islandscosta-ricacote-divoire-ivory-coastCroatiacubacyprusczech-republicdarsalaamdemocratic-peoples-rep-north-koreademocratic-republic-of-the-congo-kinshasadenmarkdjiboutidodomadominicadominican-republicdr-congodubaieast-timor-timor-lesteecuadoregyptegyptyel-salvadorenglandequatorial-guineaequitorial-guineaeritreaestoniaeswatiniethiopiafalkland-islandsfaroe-islandsfederal-states-of-moldovafijifinlandFloridafrancefrench-guianafrench-polynesiafrench-southern-territoriesgabongazageorgiagermanyghanagibraltargomaGreecegreenlandgrenadaguadeloupeguamguatemalaguineaguinea-bissauguyanahabarihaitiholy-seehondurashong-konghoustonhungaryicelandindiaindonesiaIowairaniran-islamic-republic-ofiraqirelandisraelitaliaitalyivory-coastjamaicajapanjordankaratukazakhstankilimanjarokinshasakiribatikiswahilikoreakosovokuwaitkyrgyzstanlaolatvia-lebanon-lesotho-liberia-libya-liechtenstein-lithuania-luxembourgLebanonliberiamacaumadagascarmalawimalaysia-maldivesMalimaltamarshall-islands-martinique-mauritania-mauritiusmassechutesmayottemazingirambeyamerumexicomiamimicronesiamonaco-mongolia-montenegromontserratmoroccomozambique-myanmarmtwaramwanzanamibianaurunepalnetherlandsnetherlands-antillesnevadanew-caledonianew-zealandnewyorknicaraguanigernigerianiuenorth-macedonianorthern-mariana-islandsnorwayomanpakistanpalaupalestinepalestinian-territoriespanamapapua-new-guineaparaguaypeoples-democratic-republicperuphiladhephiaphilipiansPhilippinespitcairn-islandpolandpoliticsPortugalpuerto-ricoqatarrepublic-ofrepublic-of-brazzavillerepublic-of-south-koreareunion-islandromaniaRussiarussian-federationrwandasahara-occidentalsaint-kitts-and-nevissaint-luciasaint-vincent-and-the-grenadinessamoasan-marinosao-tome-and-principesaudi-arabiasaudiarabiascotlandSenegalserbiaseychellessierra-leoneSingaporesingidaslovakia-slovak-republicsloveniasolomon-islandssomaliasouthafricaspainsri-lankasudansurinameswaziland-eswatiniswedenswitzerlandsyriasyrian-arab-republictaborataiwan-republic-of-chinatajikistantanzaniatexasthailandthe-gambiatibettimor-leste-east-timortogotokelautongatorontotrinidad-and-tobagotunisiaturkeyturkmenistanturks-and-caicos-islandstuvaluugandaunited-arabs-emiratesunited-kingdomunited-statesuruguayuzbekistanvancovervanuatuvatican-city-state-holy-seevenezuelavietnamvirgin-islands-britishvirgin-islands-u-swallis-and-futuna-islandswallis-and-futuna-islandswallis-et-futunawashington-dcwestern-saharayemenzambiazambiezimbabwe

CantonaDigital
CantonaDigital

Listen Live Radio Fortune Africa
Ukweli Na Burudani.

-Be ready to be Impacted, Inspired & Empowered.

-Keep watching our Channels

Cantona Cast Television,

Fortune Television Network (FTN)

Donation
Paypal https://www.paypal.com/donate/?hosted_button_id=6EKXMLNW8W6A2&fbclid=IwY2xjawQxeChleHRuA2FlbQIxMABicmlkETFRdkNBRndpclRDQTB5bXZZc3J0YwZhcHBfaWQQMjIyMDM5MTc4ODIwMDg5MgABHq960uGsyU3ABRIBc2h-iXGhHATvuEqe55gFsQ-rDb0fT-Z7SIQ3TV8LnkpD_aem_ybU2SvBlvyqrVsS9NAczRw

An attitude determines an altitude.

All Rights Reserved © The Cantona Group PLC||2025

5,290 posts
0 followers

Fediverse Followers


Discover more from cantonadigital

Subscribe to get the latest posts sent to your email.

Leave a Reply