Uganda: Waasi wa zamani zaidi ya Elfu 28 wamepewa msamaha

Radio Fortune Africa -Ukweli na Burudani

https://zeno.fm/radio/radio-fortune-africa

Vocalize Pre-Player Loader

Na Cantona Joseph Imechapishwa : February 26, 2026 05:10 (EAT)

Tume ya kutoa msamaha nchini Uganda, imetoa ahueni kwa waasi wa zamani zaidi ya Elfu 28 na 340 tangu mwaka 2000, mwenyekiti wake akitoa wito kwa wale ambao bado hawajarejea nyumbani kufanya hivyo chini ya muda uliowekwa.

Katika picha hii ya Feb. 12, 2015, eneo la kaburi la pamoja na wahanga wa mauaji ya kundi la Lord's Resistance Army (LRA) mwaka wa 2004 katika eneo la Barlonyo kaskazini mwa Uganda.
Katika picha hii ya Feb. 12, 2015, eneo la kaburi la pamoja na wahanga wa mauaji ya kundi la Lord’s Resistance Army (LRA) mwaka wa 2004 katika eneo la Barlonyo kaskazini mwa Uganda. AP – Rebecca Vassie

Akizungumza kwenye kikao na wanahabari Jumatano ya wiki hii, Mwenyekiti wa Tume hiyo Jaji Mstaafu Peter Onega, alisema walionufaika pakubwa na msamaha huo ni Pamoja na wapiganaji wa Kundi la LRA linaloongozwa na Joseph Kony.

Makundi mengine yaliyonufaika na mpango huu ni pamoja na lile linaloongozwa na Ali Bamuze pamoja na lile la kiislamu la ADF linalofanya shughuli zake Mashariki mwa DRC.

Jaji Onega, amesema juhudi zinafanyika kuwasiliana na viongozi wa makundi hayo waliohasi ili kuwasaidia kurejea nyumbani na kutangamana na jamii.

Hata hivyo, amesema kuna changamoto ya ucheleweshaji wa mchakato wa kuwajumuisha upya watakaonufaika, hali inayochangiwa na unyanyapaa katika baadhi ya maeneo, wanawake na watoto wakiathirika zaidi.

Sudan Kusini: Wakimbizi wakabiliwa na tishio la baa la njaa

Juhudi za utoaji wa misaada ya kibinadamu kwa zaidi ya wakimbizi Milioni Moja nchini Sudan Kusini zinakabiliwa na tishio kutokana na uhaba wa ufadhili katika idara muhimu zinazohusika na misaada kwenye Umoja wa Mataifa.

Wakimbizi wa Sudan Kusini wakiwa katika jimbo la Jonglei.
Wakimbizi wa Sudan Kusini wakiwa katika jimbo la Jonglei. AP – Florence Miettaux

Kulingana na Shirika la kuwahudumia waomba hifadhi (IOM), Sudan Kusini inasalia kuwa nchi ambayo ina idadi kubwa ya watu waliopoteza makazi yao duniani.

IOM inasema karibia watu Milioni 10 wanahitaji msaada wa dharura wa kibinadamu ambapo mwaka huu peke yake Shirika hilo linakabiliwa na upungufu wa Dolla Milioni 29 katika mipango yake ya utoaji wa misaada kwa wakimbizi wa Sudan Kusini.

Mashirika ya kuwasaidia wakimbizi yamepunguza misaada yao kutokana na kukatika kwa ufadhili.
Mashirika ya kuwasaidia wakimbizi yamepunguza misaada yao kutokana na kukatika kwa ufadhili. AP – Florence Miettaux

Juba inaendelea kukabiliwa na changamoto ya idadi kubwa ya wakimbizi, wengi wao wakitokea katika nchi jirani ya Sudan. 

Tangu mwezi Februari mwaka wa 2023, zaidi ya watu Milioni 1 wamevuka mpaka na kuingia Sudan Kusini, asilimia 67 kati yao wakiwa ni raia wa Sudan Kusini wanaorejea kutoka Sudan.

All Rights Reserved © The Cantona Group PLC||2026

afghanistanafricaalbaniaalgeriaAmericaamerican-samoaandorraangolaanguillaantarcticaantigua-and-barbudaargentinaarmeniaarubaarushaaustraliaaustriaazerbaijanbahamasbahrainbangladeshbarbadosbelarusBelgiumbelizebeninbermudabhutanboliviabosnia-and-herzegovinabotswanaBoukinafasobrazilbrunei-darussalambulgariaburkina-fasoburmaburundicaliforniacambodiacamerooncanadacape-verdecayman-islandscentral-african-republicChadchicagochilechinachristmas-islandcocos-keeling-islandscolombiacomoroscongocook-islandscosta-ricacote-divoire-ivory-coastCroatiacubacyprusczech-republicdarsalaamdemocratic-peoples-rep-north-koreademocratic-republic-of-the-congo-kinshasadenmarkdjiboutidodomadominicadominican-republicdr-congodubaieast-timor-timor-lesteecuadoregyptegyptyel-salvadorenglandequatorial-guineaequitorial-guineaeritreaestoniaeswatiniethiopiafalkland-islandsfaroe-islandsfederal-states-of-moldovafijifinlandFloridafrancefrench-guianafrench-polynesiafrench-southern-territoriesgabongazageorgiagermanyghanagibraltargomaGreecegreenlandgrenadaguadeloupeguamguatemalaguineaguinea-bissauguyanahabarihaitiholy-seehondurashong-konghoustonhungaryicelandindiaindonesiaIowairaniran-islamic-republic-ofiraqirelandisraelitaliaitalyivory-coastjamaicajapanjordankaratukazakhstankilimanjarokinshasakiribatikiswahilikoreakosovokuwaitkyrgyzstanlaolatvia-lebanon-lesotho-liberia-libya-liechtenstein-lithuania-luxembourgLebanonliberiamacaumadagascarmalawimalaysia-maldivesMalimaltamarshall-islands-martinique-mauritania-mauritiusmassechutesmayottemazingirambeyamerumexicomiamimicronesiamonaco-mongolia-montenegromontserratmoroccomozambique-myanmarmtwaramwanzanamibianaurunepalnetherlandsnetherlands-antillesnevadanew-caledonianew-zealandnewyorknicaraguanigernigerianiuenorth-macedonianorthern-mariana-islandsnorwayomanpakistanpalaupalestinepalestinian-territoriespanamapapua-new-guineaparaguaypeoples-democratic-republicperuphiladhephiaphilipiansPhilippinespitcairn-islandpolandpoliticsPortugalpuerto-ricoqatarrepublic-ofrepublic-of-brazzavillerepublic-of-south-koreareunion-islandromaniaRussiarussian-federationrwandasahara-occidentalsaint-kitts-and-nevissaint-luciasaint-vincent-and-the-grenadinessamoasan-marinosao-tome-and-principesaudi-arabiasaudiarabiascotlandSenegalserbiaseychellessierra-leoneSingaporesingidaslovakia-slovak-republicsloveniasolomon-islandssomaliasouthafricaspainsri-lankasudansurinameswaziland-eswatiniswedenswitzerlandsyriasyrian-arab-republictaborataiwan-republic-of-chinatajikistantanzaniatexasthailandthe-gambiatibettimor-leste-east-timortogotokelautongatorontotrinidad-and-tobagotunisiaturkeyturkmenistanturks-and-caicos-islandstuvaluugandaunited-arabs-emiratesunited-kingdomunited-statesuruguayuzbekistanvancovervanuatuvatican-city-state-holy-seevenezuelavietnamvirgin-islands-britishvirgin-islands-u-swallis-and-futuna-islandswallis-and-futuna-islandswallis-et-futunawashington-dcwestern-saharayemenzambiazambiezimbabwe


Discover more from cantonadigital

Subscribe to get the latest posts sent to your email.

Leave a Reply