Freiburg yatinga nusu fainali DFB Porkal

Radio Fortune Africa -Ukweli na Burudani

https://zeno.fm/radio/radio-fortune-africa

Vocalize Pre-Player Loader

Na : Cantona Joseph|RFA

Mchezaji wa Freiburg Jan Niklas akiutia mpira wavuni katika moja ya mchezo wa timu hiyoPicha: Bosco/Beautiful Sports/picture alliance

Kipa wa Freiburg, Florian Muller, aliokoa mkwaju wa penalti wa Pascal Klemens katika uwanja wa Olympia-stadion mjini Berlin na kuisaidia timu yake kupata ushindi muhimu.

Klabu ya Freiburg ya hapa Ujerumani imefuzu hatua ya nusu ya fainali ya Kombe la Ujerumani la DFB Pokal baada ya kupata ushindi wa penalti 5-4 dhidi ya Hertha Berlin usiku wa kuamkia leo.

Kipa wa Freiburg, Florian Muller, aliokoa mkwaju wa penalti wa Pascal Klemens katika uwanja wa Olympia-stadion mjini Berlin na kuisaidia timu yake kupata ushindi muhimu.

Hii leo mabingwa wa kihistoria wa michuano hiyo Bayern Munich watawakaribisha  RB Leipzig katika mchezo wa mwisho wa hatua ya robo fainali.

Wiki iliyopita, mabingwa watetezi wa kombe hili, Stuttgart na Bayer Leverkusen walitinga katika hatua hiyo ya nusu fainali. Droo ya mechi zijazo itafanyika Februari 22, huku mechi za nusu fainali ikiwa ni Aprili 21 na 22. Fainali itafanyika mjini Berlin Mei 23.

All Rights Reserved © The Cantona Group PLC||2026


Discover more from cantonadigital

Subscribe to get the latest posts sent to your email.

Leave a comment