Shambulizi katika pwani ya Somalia laibua hofu ya uharamia

Radio Fortune Africa -Ukweli na Burudani

https://zeno.fm/radio/radio-fortune-africa

Vocalize Pre-Player Loader

Na : Cantona Joseph|RFA

Shambulizi dhidi ya meli katika pwani ya Somalia limeibua hofu ya kurejea tena kwa uharamia.Picha: Indian Navy/AP/picture alliance

Shambulizi dhidi ya meli katika pwani ya Somalia limeibua hofu ya kurejea tena kwa matukio ya uharamia katika eneo hilo.

Shirika la usalama wa baharini la Uingereza limeonya kwamba washambuliaji walipanda meli karibu na pwani ya Somalia siku ya Alhamisi, baada ya matukio mawili ya hivi karibuni kuzua hofu ya kuibuka tena kwa uharamia.

Meli hiyo, inayoendeshwa na kampuni ya Ugiriki ya Latsco Marine Management, ilishambuliwa muda mfupi kabla ya adhuhuri na washambuliaji wenye silaha ilipokuwa ikisafiri kwenda Afrika Kusini kutoka India.

Kampuni hiyo ilisema katika taarifa kwamba wafanyakazi wote 24 wako salama na wanahesabiwa, na wanaendelea kuwasiliana nao kwa karibu, huku ikikataa kutoa taarifa zaidi kwa sababu za kiusalama.

Kituo cha Operesheni za Biashara za Baharini cha Uingereza (UKMTO) kilisema mashua hiyo, Hellas Aphrodite, ilikaribiwa kutoka nyuma na meli ndogo,  kabla ya kuingiliwa na wafanyakazi ambao hawakuwa na idhini.

Mamlaka wanachunguza kisa hicho. Kikosi cha wanamaji cha Umoja wa Ulaya kinachopambana na uharamia kimesema katika taarifa yake kwenye mtandao wa X kwamba kilikuwa karibu na tukio hilo na kiko tayari kuchukua hatua zinazofaa ili kujibu ipasavyo tahadhari hii ya uharamia.

All Rights Reserved © The Cantona Group PLC||2025


Discover more from cantonadigital

Subscribe to get the latest posts sent to your email.

Leave a comment