Uchaguzi Tanzania 2025: Tume ya Uchaguzi Tanzania yaanza kutangaza matokeo

Radio Fortune Africa -Ukweli na Burudani

https://zeno.fm/radio/radio-fortune-africa

Vocalize Pre-Player Loader

By : Cantona Joseph|RFA

.
Maelezo ya picha,Mkurugenzi wa Uchaguzi Ndugu Ramadhani Kailima

Tume ya Uchaguzi nchini Tanzania INEC imeanza kutangaza matokeo ya uchaguzi wa urais.

Hadi kufikia sasa ni mikoa minne pekee iliofanikiwa kuwasilisha matokeo yake.

Kulingana na matokeo hayo Mgombea wa urais kupitia tiketi ya chama tawala cha CCM Samia Suluhu Hassan anaongoza kulingana na kura zilizohesabiwa.

Aidha maandamano yameripotiwa katika eneo la Meriwa lililopo barabara ya jiji kuu la Dodoma na Dar es Salaam ambapo polisi wamewatawanya waandamanaji.

Polisi vilevile wameripotiwa kufunga barabara ya Singida – Arusha kwa hofu ya kuzuka maandamano zaidi.

Marekani yatoa tahadhari ya kiusalama kwa raia wake wanaoishi Tanzania

Ubalozi wa Marekani nchini Tanzania umetoa tahadhari ya kiusalama kwa raia wa taifa hilo wanaoishi nchini humo .

Kulingana na tahadhari hiyo ubalozi huo umewataka raia wa taifa hilo kuepuka maandamano yanayoendelea, kuepekuka mikusanyiko ya watu kufuatialia kwa karibu taarifa za vyombo vya habari ili kujifahamisha yanayoendelea mbali na kuchukua tahadhari ya juu katika maeneo waliopo.

Hatua hiyo inajiri kufuatia maandamano yanayoendelea nchini humo.

Kulingana na taarifa hiyo kuna ripoti za maandamano kote nchini ambayo yamesababisha kuzuka kwa ghasia na kufungwa kwa baadhi ya barabara.

Ripoti hiyo imeelezea kwamba baadhi ya barabara kama ile ya kuelekea katika uwanja wa ndege wa Julius Nyerere imefungwa.

Aidha taarifa hiyo imeongeza kuhusu kuzimwa kwa mtandaohali ambayo imeathiri pakubwa mawasiliano.

Maandamano yaendelea kwa siku ya pili mjini Dar es Salaam

.

Polisi katika mji wa Dar nchini Tanzania wamefyatua risasi na vitoa machozi siku ya Alhamisi kutawanya waandamanaji waliorejea barabarani siku moja baada ya uchaguzi uliogubikwa na maandamano yenye vurugu, kwa mujibu wa chombo cha habari cha Reuters.

Maandamano yalizuka mjini Dar es Salaam na miji mingine kadhaa wakati wa upigaji kura siku ya Jumatano, huku waandamanaji wakilalamikia kukamatwa kwa viongozi wakuu wa upinzani na kuzuiliwa kushiriki katika uchaguzi wa Urais mbali na madai ya ukandamizaji wa wakosoaji wa serikali.

Kwa mujibu wa Reuters baadhi ya maeneo ambayo maandamano hayo yameripotiwa kufanyika hii leo ni pamoja na Mbagala, Gongo la Mboto and Kiluvya.

Hali ya wasiwasi yaendelea kuripotiwa Tanzania

.

Hali ya wasiwasi inaendelea kushuhudiwa nchini Tanzania kufuatia maandamano ya ghasia yaliofanyika hapo jana.

Hatahivyo baadhi ya barabara ambazo zilikuwa zimefungwa hapo jana sasa zimefunguliwa.

Baadhi ya raia ambao walikuwa wamekwama kutokana na maandamano yaliosababisha amri ya kutotoka nje kuwekwa hapo jana wamefanikiwa kufika makwao.

Aidha kuna ripoti za maandamano kuzuka katika mji wa kaskazini wa Mwanza.

Taarifa mjini humo zinasema kwamba waandamanaji walifanikiwa kupenya hadi katikati ya jiji na kusababisha makabiliano ya umwagaji damu dhidi ya polisi.

Mwanza ni jiji la pili kwa ukubwa kwa idadi ya watu na biashara baada ya Dar Es Salaam na liko kwenye mwambao wa kusini mwa Ziwa Victoria.

Aidha kuna madai kwamba baadhi ya waandamanaji mjini Dar, Mbeya na Dodoma wamekuwa wakiwashambulia walioshiriki katika shughuli ya kupiga kura hapo jana

Vilevile huku mitandao ikiendelea kuminywa kwa siku ya pili mfululizo ni simu za kawaida pekee zinazotumika kwa mawasiliano.

Uchaguzi mkuu wa Tanzania 2025: Mtandao waendelea kuminywa kwa siku ya pili mfululizo

.

Tanzania inaendelea kushuhudia siku ya pili ya kukatwa kwa mtandao hatua ambayo imefanya mawasiliano kuwa changamoto.

Hapo jana siku ya uchaguzi, shirika la kimataifa la uchunguzi wa mtandao wa Netblocks, lilisema kuwa limegundua kufinywa kwa mtandao kote nchini humo.

“Imethibitishwa: Takwimu za mtandao wa moja kwa moja zinaonyesha usumbufu wa kitaifa kwa kuunganishwa kwa mtandao nchini Tanzania Siku ya Uchaguzi,” Netblocks aliandika katika machapisho kwenye vyombo vya habari vya kijamii.

Tatizo la ukosefu wa mtandao limeathiri pia wafanyabiashara wanaoendesha shughuli zao kwa njia hiyo.

Hata hivyo, hii si mara ya kwanza Tanzania kukutana na tukio kama hili ikikumbukwa pia uchaguzi wa 2020 mtandao wa X ulifungwa.

Wafanyakazi wa serikali ya Marekani Tanzania watakiwa kuchukuwa tahadhari

.

Wafanyakazi wa Serikali ya Marekani wanaoishi nchini Tanzania wameshauriwa kuchukua tahadhari na kujilinda kufuatia ghasia na maandamano yalioripotiwa nchini humo.

Kulingana na taarifa ya ubalozi huo iliotolewa hapo jana tarehe 29 Oktoba, ubalozi huo aidha umesema kwamba shughuli zake hii leo zitakuwa hudumu za dharura pekee na za kibalozi.

Vilevile wafanyakazi hao wametakiwa kuepuka maandamano, mikusanyiko ya watu, kutazama taarifa za vyombo vya habari ili kujua yanayoendelea mbali na kuchukua tahadhari kuu katika maeneo walipo.

Hatua hiyo inajiri kufuatia maandamano yaliofanyika hapo jana wakati ambapo upigaji kura ulikuwa ukiendelea.

Raia wa Tanzania hapo jana walipiga kura kumchagua rais wabunge na madiwani licha ya maandamano hayo yaliofanywa na vijana.

All Rights Reserved © The Cantona Group PLC||2025


Discover more from cantonadigital

Subscribe to get the latest posts sent to your email.

Leave a comment