Shughuli za upigaji kura Arusha ni tulivu

Radio Fortune Africa -Ukweli na Burudani

https://zeno.fm/radio/radio-fortune-africa

Vocalize Pre-Player Loader

Na: Cantona Joseph|RFA

a
Maelezo ya picha,Mkuu wa mkoa wa Arusha, Amos Makalla

Mkoa wa Arusha kuna utulivu shughuli za upigaji kura zikiendelea. Kwa mujibu wa mwandishi wetu jijini humo, ametueleza kuwepo kwa utulivu mkubwa, mtu mmoja mmoja wakionekana mtaani.

Mkuu wa Mkoa huo, Amos Makalla alikuwa miongoni mwa waliojitokeza mepema mara baada ya vituo kvya kura kufunguliwa.

Mkuu huo wa mkoa alipiga kura katika kituo cha AICC Hospitali.

s
Maelezo ya picha,Mkuu wa mkoa wa Arusha, Amos Makalla (kulia) akipanga mstari kwenda kupiga kura kwenye kituo cha AICC Hospitali
s
s
s

Upigaji kura waanza rasmi

a

Shughuli za upigaji zimeanza rasmi katika maeneo mengi ya nchi. Katika maeneo ya miji ya Dar es Salaam, Arusha, Kilimanjaro, Mbeya, Zanzibar, Tanga wapiga kura wameonekana wakifika vituoni tangu mapema alfajiri.

Maafisa wa uchaguzi katika maeneo hayo wanasema vituo vimefunguliwa kwa wakati, na kuhimiza kufuatwa kwa taratibu zote ikiwemo uhakiki wa wapiga kura kwa njia ya kielektroniki (BVR).

Baadhi ya wapiga kura wameeleza kufurahishwa na maandalizi ya tume na kuhimiza wananchi wenzao kujitokeza kwa wingi kutekeleza haki yao ya kikatiba.

Awali Tume ya Taifa ya Uchaguzi ya Uchaguzi (INEC) ilitoa wito kwa wapiga kura kutokaa majumbani na kuendelea kujitokeza hadi muda wa kufunga vituo utakapofika saa 10:00 jioni.

Siku ya pili ya upigaji kura Zanzibar

Visiwani Zanzibar

Leo ni siku ya pili ya upigaji kura Zanzibar. Jumla ya vituo 1,756 vya kupigia kura kote Unguja na Pemba vimefunguliwa saa 6:00 asubuhi na kufungwa saa 12:00 asubuhi.

Zaidi ya wapiga kura 700,000 waliojiandikisha wanatarajiwa kupiga kura zao katika uchaguzi mkuu ambao hadi sasa umebaki shwari kwa kiasi kikubwa katika visiwa hivyo, ambavyo vina historia ya mashindano ya kisiasa yenye mvutano.

Wapiga kura

Mchuano mkuu ni kati ya mgombea wa Chama Cha Mapinduzi (CCM), Dkt. Hussein Mwinyi, na mgombea wa ACT-Wazalendo, Othman Masoud Othman.

Dkt. Mwinyi anatarajiwa kupiga kura yake katika kituo cha kupigia kura cha Kariakoo saa 2:00 asubuhi, huku Othman Masoud akipiga kura katika kituo cha kupigia kura cha Mpendaye.

Matokeo yanatarajiwa kutangazwa ndani ya saa 24.

Rais aliye madarakani Hussein Ali Mwinyi anaangazia rekodi ya kuvutia ya maendeleo ya miundombinu, ikiwa ni pamoja na majengo ya shule ya hali ya juu, vituo vya afya vya kisasa, na mtandao wa kilomita mia kadhaa za barabara katika visiwa hivyo.

Kwa upande mwingine, upinzani umejikita katika ahadi za kutokomeza ufisadi, ambao unadai umekuwa mkubwa sana chini ya utawala wa sasa unapotekeleza miradi yake ya miundombinu iliyotangazwa sana.

ACT Wazalendo pia imeapa kushinikiza uhuru zaidi kwa Zanzibar, ikisema kwamba maendeleo ya visiwa hivyo yamezuiwa na hitaji la kutafuta idhini kutoka kwa serikali ya bara kuhusu maamuzi mengi muhimu.

Uhakiki

Mshirikishe mwenzako, Siku ya pili ya upigaji kura Zanzibar

Vituo vya kupigia kura kufunguliwa saa moja asubuhi

s
Maelezo ya picha,Maafisa wa Uchaguzi katika Kituo cha Viwandani, WEO, namba moja jijini Dodoma

Kwa mujibu wa Tume yta Taifa ya Uchaguzi, Vituo vya kupigia kura vinafunguliwa saa moja kamili asubuhi.

Katika maeneo Mbalimbali ya nchi, kumeonekana maandalizi yakiendelea kwa maafisa wa uchaguzi kuandaa mazingira ya kupigia kura.

Na katika baadhi ya maeneo tayari watu wanaonekana kusogea vituoni tayari kwa ajili ya kupiga kura. Picha chini ni Maafisa wa Uchaguzi katika Kituo cha Viwandani, WEO, namba moja jijini Dodoma wakiendelea na maandalizi ya mwisho.

a
A
Msimamizi
Uchaguzi

Mshirikishe mwenzako, Vituo vya kupigia kura kufunguliwa saa moja asubuhi

Watanzania wanapiga kura leo

S

Watanzania wanapiga kura leo katika Uchaguzi Mkuu wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, ambapo Rais Samia Suluhu Hassan wa chama tawala Chama Cha Mapinduzi (CCM) anatazamiwa kutetea nafasi yake kwa muhula mwingine wa miaka mitano.

Ni uchaguzi wa saba tangu kurejeshwa kwa mfumo wa vyama vingi mwaka 1992, na unafanyika wakati vyama vikuu vya upinzani vikiwa na misimamo tofauti kuhusu ushiriki wao katika mchakato huu.

Chama kikuu cha upinzani, CHADEMA, hakishiriki uchaguzi huo kikishinikiza mabadiliko ya mfumo wa uchaguzi, wakidai unakipendelea chama tawala.

Wakati huo huo, chama cha ACT-Wazalendo hakina mgombea urais baada ya Luhaga Mpina kuenguliwa na Tume Huru ya Taifa ya Uchaguzi (INEC) kwa kutokidhi matakwa ya kikanuni.

Kwa mujibu wa INEC, vituo vya kupigia kura vinafunguliwa saa 1:00 asubuhi na vitafungwa saa 10:00 jioni kabla ya kuanza kwa zoezi la kuhesabu kura mara moja baada ya upigaji kura kukamilika.

Hapo jana, wakaazi wa visiwa vya Zanzibar walipiga kura ya mapema kwa makundi maalum ikiwemo askari, maafisa wa tume na wahudumu wa afya. Tume imesema maandalizi yote yamekamilika na imewataka wapiga kura kufika vituoni mapema ili kuepuka msongamano.

All Rights Reserved © The Cantona Group PLC||2025


Discover more from cantonadigital

Subscribe to get the latest posts sent to your email.

Leave a comment