Radio Fortune Africa -Ukweli na Burudani
https://zeno.fm/radio/radio-fortune-africa

Na: Cantona Joseph|RFA

Wafuasi wa upinzani wakiandamana barabaraniPicha: Zohra Bensemra/REUTERS
Watu wanne wameuawa katika makabiliano kati ya vikosi vya usalama na wafuasi wa kiongozi wa upinzani wa Cameroon ambaye anadai kushinda uchaguzi wa hivi karibuni wa rais.
Watu wanne wameuawa katika makabiliano kati ya vikosi vya usalama na wafuasi wa kiongozi wa upinzani wa Cameroon ambaye anadai kushinda uchaguzi wa hivi karibuni wa rais, kabla ya matokeo rasmi kutangazwa hii leo.
Issa Tchiroma, ambaye alipambana na Rais Paul Biya aliyetawala kwa miaka 43 katika uchaguzi wa Oktoba 12, aliwataka wafuasi wake kuandamana kwa amani usiku wa kuamkia tangazo hilo, licha ya marufuku ya mikusanyiko ya umma.
Tchiroma anasema alishinda asilimia 54.8 ya kura, lakini wachambuzi wengi wanatarajia Biya mwenye umri wa miaka 92 kushinda muhula wa nane katika uchaguzi ambao wakosoaji wake wanasema umezidi kuibiwa.
Katika jiji kubwa zaidi la Cameroon la Douala, gavana wa mkoa alisema waandamanaji “walishambulia” kikosi cha polisi na vituo vya polisi katika wilaya mbili.
All Rights Reserved © The Cantona Group PLC||2025
Discover more from cantonadigital
Subscribe to get the latest posts sent to your email.