Wagombea wa Urais Ivory Coast wafanya kampeini ya mwisho

Radio Fortune Africa -Ukweli na Burudani

https://zeno.fm/radio/radio-fortune-africa

Vocalize Pre-Player Loader

Na: Cantona Joseph|RFA

Rais wa Ivory Coast Alassane Ouattara afanya kampeini za urais mnamo Oktoba 18, 2025 mjini AbidjanPicha: Joseph Zahui/Matrix Images/IMAGO

Wagombea urais nchini Ivory Coast jana walihitimisha kampeni zao kabla ya uchaguzi mkuu utakaofanyika kesho Jumamosi.

Rais aliyepo madarakani Alassane Ouattara, mwenye umri wa miaka 83, anawania muhula wa nne, hatua itakayopanua utawala wake hadi karibu miongo miwili.

Maelfu ya wafuasi wake walijitokeza mjini Abidjan, ambapo aliwahakikishia ushindi akisema, “Mbwa wanabweka lakini msafara tayari umesonga.”

Wagombea wa upinzani, akiwemo Simone Gbagbo, mke wa rais wa zamani Laurent Gbagbo, na Jean-Louis Billon, waziri wa zamani wa biashara, pia walifanya mikutano yao ya mwisho.

Wagombea wawili waondolewa kwenye kinyang’anyiro

Uchaguzi huu unakuja huku wagombea wawili wakuu wa upinzani, Laurent Gbagbo na Tidjane Thiam, wakiondolewa kwenye kinyang’anyiro — hali iliyosababisha maandamano na hofu ya vurugu.

Shughuli mjini Abidjan zimepungua kwa hofu ya ghasia, huku wachambuzi wakisema Ouattara ana nafasi kubwa ya kushinda katika raundi ya kwanza.

All Rights Reserved © The Cantona Group PLC||2025


Discover more from cantonadigital

Subscribe to get the latest posts sent to your email.

Leave a comment