Mwamini Mungu katika hali yoyote ile.

Katika maisha haya yenye vita,changamoto na dhiki za kila aina nimejifunza kumwamini Mungu katika hali yoyote ile ninayoipitia

Unaweza kuwa umepoteza kazi,umepoteza marafiki,umepoteza mchumba,umepoteza nafasi mbalimbali ambazo zingekufanikisha

Niko hapa kukwambia mwamini Mungu hata katika mazingira magumu unayoyapitia,Mungu anajua kesho yako imebeba nini kwa ajili yako

Unaweza kudharauliwa,unaweza kuonekana hufai,unaweza kuonekana huna faida,unaweza kuchekwa na watu wako wa karibu katikati ya mambo yote mwamini Mungu

Katika majira na saa usiyodhani,saa ambayo akili zako zimefika mwisho moyo umechoka na mwili wako umechekaa ndipo Mungu unayemwamini atatokea na kukusaidia

Niko hapa kukutia moyo na kukuombea we mwamini Mungu tu atafanya, ninakuombea najua umefika mahali umechoka Mungu unaemwamini ashuke na kukusaidia

Biblia inasema kwenye

Isaya 43:18:19

Msiyakumbuke mambo ya kwanza, wala msiyatafakari mambo ya zamani.

Tazama, nitatenda neno jipya; sasa litachipuka; je! Hamtalijua sasa? Nitafanya njia hata jangwani, na mito ya maji nyikani.

Sijajua ninani lakini Mungu amenisemesha ya kwamba wako watu ambao kibinadamu wamechoka na akili zao zimefika mwisho

Inawezekana ni kwenye mahusiano umeumizwa mpaka umefika mahali unasema nimefika mwisho sitaki tena,inawezekana ni kwenye ndoa akili zako zimefika mwisho

Moyo wako umejaa maumivu na uchungu uliopelekea hata chakula kukosa radha mdomoni mwako kwasababu ya akili kufika mwisho

Nikiwa katika kuomba na kusali nikasikia sauti ikiniambia sio mwisho, hata kama akili zimefika mwisho Mungu bado hajafika mwisho

Mahali akili za mwanadamu zinapoishia ndipo Mungu anapoanzia inuka tena, Mungu akupe nguvu mpya bado safari inaendalea hapo sio mwisho

Ninakuombea sana Mungu akupe nguvu ya kuinuka tena,ninekuombea Mungu akupe nguvu ya kuendelea tena kesho yako ni nzuri kuliko leo yako sio mwisho songa mbele


Discover more from cantonadigital

Subscribe to get the latest posts sent to your email.

Leave a comment