Radio Fortune Africa -Ukweli na Burudani
https://zeno.fm/radio/radio-fortune-africa

Na:Cantona Joseph|RFA
Uturuki imewatuma wataalamu kadhaa wa uokozi kwenda Ukanda wa Gaza kulisaidia kundi la Hamas kuitafuta miili ya mateka wa Israel ambao inaaminika imefunikwa na vifusi vya majengo yaliyoporomoshwa kwa vita.

Familia za mateka wa Israel zimeongeza shinikizo kwa serikali kuliandama kundi la Hamas lirejeshe miili ya jamaa zao.Picha: DW
Tangazo la kutumwa waatalamu hao limetolewa katika wakati hasira inaongezeka nchini Israel hususani miongoni mwa familia za mateka baada ya Hamas kusema imeshindwa kuipata miili ya ndugu na jamaa zao.
Familia hizo zimeitaka serikali ya Israel kusitisha utekelezaji wa hatua zinazofuata za mkataba wa kusitisha vita hadi pale Hamas itakapoikabidhi miili ya mateka 19 waliopoteza maisha wakiwa kizuizini.
Hamas imesema imedhamiria kutimiza matakwa ya mkataba uliosimamiwa na Marekani ikiwa ni pamoja na kuikabidhi miili yote ya mateka itakapopatikana.
Viongozi wa Israel wametishia kuanzisha tena vita au kuzuia upelekwaji misaada Ukanda wa Gaza iwapo miili hiyo haitopatikana haraka.
All Rights Reserved © The Cantona Group PLC||2025
Discover more from cantonadigital
Subscribe to get the latest posts sent to your email.