Radio Fortune Africa -Ukweli na Burudani
https://zeno.fm/radio/radio-fortune-africa


Ukraine imekuwa ikilenga vituo vya nishati vya Urusi kulipiza kisasi mashambulizi ya Moscow dhidi ya miundombinu yake ya nishati.Picha: Mikhail Razvozhaev/telegram/AP/picture alliance
Na:Cantona Joseph|RFA
Droni ya Ukraine imeshambulia ghala la mafuta katika mji wa Feodosia, mashariki mwa Crimea, na kusababisha moto mkubwa, afisa wa Urusi Sergei Aksyonov amesema.
Afisa wa Urusi aliyeteuliwa kuiongoza Crimea amesema Jumatatu kwamba droni ya Ukraine imeshambulia ghala la mafuta katika mji wa Feodosia, mashariki mwa rasi hiyo, na kusababisha moto mkubwa. Shambulio hilo limeongeza mvutano unaoendelea kati ya Moscow na Kyiv, huku vita vikikosa dalili za kumalizika.
Kiongozi wa utawala wa Urusi katika eneo hilo, Sergei Aksyonov, alisema kupitia Telegram kwamba zaidi ya droni 20 zimedunguliwa na vikosi vya ulinzi wa anga, na hakuna majeruhi waliothibitishwa. Hata hivyo, hakutoa maelezo kuhusu ukubwa wa uharibifu uliosababishwa na shambulio hilo.

Oktoba 8, 2022, shambulio la Ukraine liliharibu daraja linaloiunganisha Crimea na Urusi.Picha: AFP/Getty Images
Ghala la mafuta la Feodosia na miundombinu mingine ya nishati na kijeshi ya Crimea imekuwa ikilengwa mara kwa mara na mashambulizi ya Ukraine tangu Urusi ilipoanza uvamizi wake mwaka 2022.
Wakati huo huo, Ukraine na Urusi zimezidisha mashambulizi dhidi ya miundombinu ya nishati za kila upande, katika kipindi ambacho juhudi za kidiplomasia za kurejesha mazungumzo ya amani zimeendelea kukwama kwa miezi kadhaa.
All Rights Reserved © The Cantona Group PLC||2025
Discover more from cantonadigital
Subscribe to get the latest posts sent to your email.