Radio Fortune Africa -Ukweli na Burudani
https://zeno.fm/radio/radio-fortune-africa

Na:Cantona Joseph|RFA
Kama ambavyo tumekuwa tukiripoti, maelezo kamili ya mpango wa awamu ya kwanza wa kusitisha mapigano hayajafichuliwa rasmi.
Hivi ndivyo tunavyojua hadi sasa:
Chanzo cha habari cha Palestina kimeiambia BBC kwamba makubaliano hayo yanabainisha kuwa wafungwa 250 wa Kipalestina na Wagaza 1,700 wanaozuiliwa na wanajeshi wa Israel tangu vita hivyo kuanza wataachiliwa huru.
Chanzo hicho kilisema Hamas haijapokea orodha ya wafungwa wa Kipalestina ambao Israel inapanga kuwaachilia lakini suala hili linatarajiwa kutatuliwa ndani ya saa chache.
Afisa mkuu wa Palestina pia ameiambia BBC kuwa chini ya makubaliano hayo, Israel itaruhusu malori 400 ya misaada kuingia Gaza kila siku, na idadi hiyo ikiongezeka polepole katika hatua za baadaye.
Kwamujibu wa afisa wa Ikulu, Hamas itawaachilia mateka 20 walio hai wakati wa awamu ya kwanza ingawa ni mafanikio makubwa, mpango wa awamu ya kwanza ni mwanzo tu, sio mwisho.
Ni usitishaji vita, sio mpango wa amani, anaandika mwandishi wetu mkuu wa kimataifa Lyse Doucette.
All Rights Reserved © The Cantona Group PLC||2025
Discover more from cantonadigital
Subscribe to get the latest posts sent to your email.