Rajoelina amteua Waziri Mkuu mpya mwanajeshi

Radio Fortune Africa -Ukweli na Burudani

https://zeno.fm/radio/radio-fortune-africa

Rais wa Nice Madagascar Andry Rajoelina akiwa katika mji wa Riviera wa Ufaransa wa Nice, Juni 8, 2025.

Na:Cantona Joseph|RFA

Rais wa Madagascar Andry Rajoelina alimteua Jenerali Ruphin Fortunat Dimbisoa Zafisambo kuwa Waziri Mkuu, akitumaini kutuliza maandamano yanayoendelea dhidi ya uongozi wake ambayo yameitumbukiza nchi katika mgogoro.

Akizungumza akiwa ikulu, Rajoelina alisema waziri Mkuu mpya anapaswa “kuwahudumia wananchi” na awe “mtu safi, mwenye uadilifu, na anayefanya kazi kwa haraka.” Pamoja na kiongozi huyo kutoa ahadi ya  kile alichokiita “tayari kuiokoa Madagascar”, hatua yake ya kuvunja serikali nzima wiki iliyopita haikuweza kukidhi kiu ya waandamanaji.

Maandamano hayo, ambayo yalianza kutokana na hasira dhidi ya kukatika kwa maji na umeme mara kwa mara katika kisiwa hicho cha Bahari ya Hindi chenye umasikini, yamegeuka kuwa harakati za kupinga serikali zinazomtaka Rajoelina ajiuzulu.

All Rights Reserved © The Cantona Group PLC||2025


Discover more from cantonadigital

Subscribe to get the latest posts sent to your email.

Leave a comment