Maandamano Morocco kushinikiza mageuzi katika sekta ya afya

Radio Fortune Africa -Ukweli na Burudani

https://zeno.fm/radio/radio-fortune-africa

Na:Cantona Joseph|RFA

Maandamano mapya ya kudai mageuzi katika sekta za afya na elimu yamefanyika nchini Morocco kwa siku ya sita mfululizo, kufuatia vifo vya watu watatu vilivyotokea wakati wa makabiliano yaliyotokea jana usiku.

Mjini Rabat, waandamanaji waliobeba bendera za taifa walikusanyika barabarani na kushinikiza kuimarishwa kwa sekta ya afya badala ya kupewa kipaumbele kwa ujenzi wa viwanja vya michezo.

Kwa mujibu wa mwandishi wa shirika la habari la AFP, maandamano ya siku ya Alhamisi yalifanyika kwa amani bila kuripotiwa visa vya vurugu.

Maandamano mengine pia yameripotiwa katika miji ya Casablanca, Marrakech, na Agadir, yote yakifanyika kwa utulivu.

Hali hiyo ya kuongezeka kwa maandamano imechochewa na hasira ya umma kuhusu ukosefu wa usawa wa kijamii, hasa baada ya ripoti za mwezi uliopita kuhusu vifo vya wanawake wanne wajawazito katika hospitali ya umma mjini Agadir—tukio lililoibua maswali kuhusu ubora wa huduma za afya nchini humo.

Wengi wa waandamanaji wanaamini kuwa sekta za afya na elimu ya umma zinahitaji maboresho ya haraka, hasa wakati ambapo mamlaka zinaendelea kusukuma miradi mikubwa ya miundombinu kwa ajili ya kuandaa Kombe la Mataifa ya Afrika mwezi ujao, pamoja na Kombe la Dunia la FIFA la mwaka 2030.

All Rights Reserved © The Cantona Group PLC||2025


Discover more from cantonadigital

Subscribe to get the latest posts sent to your email.

Leave a comment