Radio Fortune Africa -Ukweli na Burudani
https://zeno.fm/radio/radio-fortune-africa
Shirika la Kimataifa la kutetea haki za binadamu la Human Rights Watch, katika ripoti yake inaishtumu serikali ya Tanzania kwa kuminya uhuru wa kisiasa, hatua ambayo inatilia shaka iwapo uchaguzi mkuu wa tarehe 29 mwezi huu utakuwa wa huru na haki.

Na:Cantona Joseph|RFA
Human Rights Watch katika ripoti yake, inasema serikali nchini Tanzania, imeendelea kukandamiza wanasiasa wa upinzani na wakosoaji wa chama tawala CCM, kuminya uhuru wa vyombo vya Habari, na kuingilia uhuru wa Tume ya Uchaguzi.
Nomathamsanqa Masiko-Mpaka, mtafiti wa Shirika hilo barani Afrika, amesema serikali ya Tanzania, inapaswa kuacha vitendo hivyo na badala yake kushiriki kwenye majadiliano na wapinzani wake, ili kuleta mageuzi muhimu, yatakayosaidia uchaguzi huo kuwa huru na haki.
Aidha, Shirika hilo linasema, limenakili visa 10 ambapo wapinzani wa serikali, wametekwa, kukamatwa na kuteswa kwa sababu ya misimamo yao ya kisiasa, akiwemo kiongozi mkuu wa upinzani Tundu Lissu ambaye alikamatwa mwezi Aprili, na kufunguliwa mashtaka ya uhaini.
All Rights Reserved © The Cantona Group PLC||2025
Discover more from cantonadigital
Subscribe to get the latest posts sent to your email.