Upo katika kipindi kipi maishani?

Kuna kipindi unaweza kukipitia kwenye maisha haya,kikawa ni kipindi cha machozi na kilio na hasara katika kipindi maisha yanaweza kukosa maana kabisa

Nikiwa katika kuomba Bwana akaniambia wambie hata kama wamelia Bwana atawafuta machozi, walioona njaa na kiu hawata ona njaa na kiu tena

Ufunuo 7:16:17
Hawataona njaa tena, wala hawataona kiu tena, wala jua halitawapiga, wala hari iliyo yote.
Kwa maana huyo Mwana-Kondoo, aliye katikati ya kiti cha enzi, atawachunga, naye atawaongoza kwenye chemchemi za maji yenye uhai, na Mungu atayafuta machozi yote katika macho yao.

Mpendwa wangu acha Mungu akufute machozi yako, aziondoe na hasara saa imefika hutalia tena ukiwa na uharibifu havitatajwa tena kwenye maisha yako

Ninakuombea neema ikufunike na Mungu akufute machozi uliyolia kwa muda mrefu Mungu akupe kicheko katika jina la Yesu

Ikiwa unaamini mwambie Mungu “Baba yatosha nifute machozi sasa na ukanipe kicheko katika jina la Yesu”


Discover more from cantonadigital

Subscribe to get the latest posts sent to your email.

Leave a comment