Wapalestina katika Ukingo wa Magharibi wakwama huku Israel ikifunga vivuko vya kimataifa

Radio Fortune Africa -Na Cantona Joseph

https://zeno.fm/radio/radio-fortune-africa

Eneo la kivuko

Israel imefunga kivuko pekee kati ya Ukingo wa Magharibi unaokaliwa na Israel na nchi jirani ya Jordan, na kuwazuia zaidi ya Wapalestina milioni mbili kuingia.

Mamlaka ya viwanja vya ndege vya Israel, ambayo inasimamia kivuko cha Allenby Bridge, ilisema kuwa itafungwa kwa muda usiojulikana kuanzia Jumatano asubuhi “kwa maelekezo ya uongozi wa kisiasa”. Haikutoa sababu.

Kufungwa huko kumekwamisha Wapalestina wengi katika Ukingo wa Magharibi, ambao hawawezi kwenda kwa safari zilizopangwa nje ya nchi.

Wale ambao wako nje ya nchi wameshindwa kusafiri nyumbani.

Hatua hii inakuja siku chache baada ya wanajeshi wawili wa Israel kuuawa kwa kupigwa risasi karibu na kivuko na mtu aliyekuwa na bunduki kutoka Jordan, ambaye aliuawa katika eneo la tukio.

Kivuko hicho, pia kinajulikana kama Daraja la King Hussein, kiko karibu nusu kati ya Amman na Jerusalem na ndio kivuko pekee rasmi kati ya Ukingo wa Magharibi na Jordan.

Pia ni sehemu ya pekee ya kuingia Ukingo wa Magharibi ambayo haipiti Israeli. Wapalestina wengi katika Ukingo wa Magharibi hawaruhusiwi kusafiri kupitia viwanja vya ndege vya Israel au vivuko vingine vya mpaka wa Israel, kumaanisha daraja hilo ni muunganisho muhimu kwa ulimwengu wa nje.

Mwanasiasa mashuhuri wa Palestina Mustafa Barghouti aliiambia BBC kuwa ni “hatua hatari” ambayo ilimaanisha “kuwafunga” watu katika Ukingo wa Magharibi na “kuwanyima njia pekee ya kutoka”. “Unazungumza hapa kuhusu kuvuruga uhusiano kati ya mamia ya maelfu ya familia ambazo kwa kawaida huunganishwa kupitia Jordan,” alisema.

Nicolas Sarkozy ahukumiwa miaka mitano jela katika kesi ya ufadhili wa kampeni

Sarkozy

Rais wa zamani wa Ufaransa Nicolas Sarkozy amehukumiwa kifungo cha miaka mitano jela baada ya kupatikana na hatia ya kula njama ya uhalifu katika kesi inayohusiana na mamilioni ya euro ya fedha haramu kutoka kwa kiongozi wa Libya marehemu Kanali Muammar Gaddafi.

Mahakama ya jinai ya Paris ilimuondolea mashtaka mengine yote, ikiwa ni pamoja na rushwa na ufadhili haramu wa kampeni.

Akizungumza na waandishi wa habari baada ya kusikilizwa kwa kesi hiyo mzee huyo mwenye umri wa miaka 70, ambaye alikuwa rais wa Ufaransa kuanzia 2007 hadi 2012, aliitaja hukumu hiyo kuwa “haijazingatiautawala wa sheria”.

Sarkozy, ambaye anadai kesi hiyo ina msukumo wa kisiasa, alituhumiwa kutumia fedha kutoka kwa Gaddafi kufadhili kampeni yake ya uchaguzi wa 2007.

Jeshi la wanamaji la Ufaransa lanasa karibu tani 10 za kokeni pwani ya Afrika Magharibi

Kokeni hiyo ilinaswa kutoka kwenye meli ya uvuvi isiyo na bendera karibu na Ghuba ya Guinea

Jeshi la wanamaji la Ufaransa limenasa karibu tani 10 za kokeni, yenye thamani ya $610m (£540m) katika pwani ya Afrika Magharibi, mamlaka ya Ufaransa imesema.

Meli mbili za wanamaji za Ufaransa zinazofanya kazi kama sehemu ya Operesheni Corymbe zilinasa kokeni kutoka kwenye meli ya uvuvi isiyo na bendera siku ya Jumatatu, zikifanya kazi baada ya kuarifiwa na ujasusi wa baharini, mamlaka ya kupambana na dawa za kulevya na Shirika la Kitaifa la Uhalifu la Uingereza.

Ujumbe wa wanamaji wa Corymbe umetumwa na Ufaransa katika Ghuba ya Guinea tangu 1990 ili kuhakikisha usalama katika eneo ambalo uharamia ni wa kawaida. “Tani 9.6 za kokeni zimenaswa na meli mbili za Ufaransa,” jeshi la wanamaji la Ufaransa lilisema.

Imeongeza kuwa tani 54 za dawa za kulevya zimenaswa katika eneo hilo tangu mwanzoni mwa mwaka.

Ghuba ya Guinea, karibu na pwani ya magharibi mwa Afrika, imeshuhudia visa vingi vya dawa za kulevya katika miezi ya hivi karibuni, huku eneo hilo likiwa kituo kikuu cha usafirishaji wa mihadarati duniani, hasa kokeni kutoka Amerika Kusini ikisafirishwa hadi Ulaya.

Eneo hilo liliwahi kuchukuliwa kuwa eneo hatari zaidi duniani kwa uharamia wa baharini, likipita maji ya Somalia.

Nchi kadhaa za Magharibi zimetuma meli kusaidia kukabiliana na uharamia katika eneo hilo.

Rekodi ya kunaswa kokeni ya tani 10.7 ilifanywa na jeshi la wanamaji la Ufaransa mnamo Machi mwaka jana, katika kile kilichokuwa kizuizi kikubwa cha biashara hiyo haramu katika pwani ya Afrika Magharibi.

Zaidi ya watoto 1,000 waugua kutokana na chakula cha bure shuleni nchini Indonesia

Mtoto

Zaidi ya watoto 1,000 wameugua kutokana na chakula cha mchana cha bure shuleni nchini Indonesia wiki hii, kulingana na mamlaka, tukio la hivi karibuni zaidi katika msururu wa matukio ya sumu ya chakula yanayohusishwa na mpango wa chakula bora wa Rais Prabowo Subianto wa mabilioni ya dola.

Yuyun Sarihotima, mkuu wa Kituo cha Afya cha Jamii cha Cipongkor Magharibi mwa Java, aliiambia BBC Indonesia kuwa jumla ya waathiriwa wa sumu iliyorekodiwa kati ya Jumatatu na Jumatano imefikia 1,171.

Inafuatia kuwekewa sumu kwa wanafunzi 800 wiki iliyopita huko Java Magharibi na majimbo ya Sulawesi ya Kati.

Rais Prabowo amefanya mpango wa chakula bora, ambao unalenga kutoa chakula cha mchana bila malipo kwa watoto wa shule milioni 80.

Lakini matukio mengi ya sumu kwenye chakula yamesababisha mashirika yasiyo ya kiserikali kutoa wito kwa mamlaka kusimamisha mpango huo kutokana na wasiwasi wa kiafya.

Muhaimin Iskandar, Waziri Mratibu wa Uwezeshaji Jamii, alisema Jumatano kwamba “hakuna mipango ya kuizuia”.

Waathiriwa wa hivi karibuni walilalamika kwa maumivu ya tumbo, kizunguzungu, na kichefuchefu, pamoja na changamoto yakupumua, ambayo ni dalili isiyo ya kawaida ya sumu ya chakula.

Matukio ya awali ya sumu ya chakula vinavyotokana na mpango wa bure wa chakula cha mchana vimetaja utayarishaji wa chakula kizembe kama sababu inayoshukiwa.

Waathirika wa wiki hii walikula milo iliyojumuisha kuku wa mchuzi wa soya, tofu iliyokaangwa, mboga mboga na matunda, lakini matukio ya hapo awali ya sumu yamehusishwa na mchuzi ulioharibika na, katika kisa kimoja, samaki papa wa kukaanga.

Mkuu wa Wakala wa Kitaifa wa Lishe wa Indonesia Dadan Hindayana alisema Jumatano kwamba sumu kubwa ya chakula huko Cipongkor wiki iliyopita ilitokana na makosa ya kiufundi ya Kitengo cha Huduma ya Utimilifu wa Lishe (SPPG).

Operesheni za SPPG huko Cipongkor zimeripotiwa kusitishwa, kulingana na Shirika la Kitaifa la Lishe.

Kamishna wa West Bandung Jeje Ritchie Ismail alisema chama chake kilitangaza sumu ya watu wengi huko Cipongkor “tukio la ajabu ili tukio hilo lishughulikiwe kwa haraka na kwa kina zaidi”.

Nicolas Sarkozy apatikana na hatia ya kula njama ya uhalifu katika kesi ya Libya

Sarkozy

Rais wa zamani wa Ufaransa Nicolas Sarkozy amepatikana na hatia ya kula njama ya uhalifu katika kesi inayohusiana na kuchukua mamilioni ya euro ya fedha haramu kutoka kwa kiongozi wa Libya marehemu Kanali Muammar Gaddafi.

Mahakama ya jinai ya Paris ilimuondolea mashtaka mengine yote, ikiwa ni pamoja na rushwa na ufadhili haramu wa kampeni.

Sarkozy, ambaye anadai kesi hiyo ina msukumo wa kisiasa, alituhumiwa kutumia fedha kutoka kwa Gaddafi kufadhili kampeni yake ya uchaguzi wa 2007.

Badala yake mwendesha mashtaka alidai Sarkozy aliahidi kumsaidia Gaddafi kumpambania kama mshirika na nchi za Magharibi. Sarkozy, 70, alikuwa rais wa Ufaransa kutoka 2007 hadi 2012.

Uchunguzi huo ulianzishwa mwaka wa 2013, miaka miwili baada ya Saif al-Islam, mtoto wa kiongozi wa wakati huo wa Libya, kwanza kumshutumu Sarkozy kwa kuchukua mamilioni ya pesa za baba yake kwa ufadhili wa kampeni.

Mwaka uliofuata, mfanyabiashara wa Lebanon Ziad Takieddine, ambaye kwa muda mrefu alikuwa kama mtu kati kati ya Ufaransa na Mashariki ya Kati, alisema alikuwa ameandika uthibitisho kwamba zabuni ya kampeni ya Sarkozy “ilifadhiliwa” na Tripoli, na kwamba malipo ya thamani ya € 50m (£ 43m) yaliendelea baada ya kuwa rais.

Mkewe Sarkozy, mwanamitindo mkubwa wa zamani na mwimbaji mzaliwa wa Italia, Carla Bruni-Sarkozy, alishtakiwa mwaka jana kwa kuficha ushahidi unaohusishwa na kesi ya Gaddafi na kujihusisha na wahalifu kufanya ulaghai, ambayo yote anakanusha.

Tangu kupoteza nafasi ya kuchaguliwa tena mwaka wa 2012, Sarkozy amekuwa akilengwa na uchunguzi kadhaa wa uhalifu.

Rwanda na DRC zakubaliana kuanza utekelezaji wa hatua za usalama zilizosimamiwa na Marekani

g
Maelezo ya picha,Mawaziri hao wa mambo ya nje wa Congo Thérèse Kayikwamba Wagner (kulia) na Rwanda Olinier Nduhungirehe (kushoto walitia saini mkataba wa amani mjini Washington na Rais Donald Trump Juni 27

Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo (DRC) na Rwanda zimekubaliana kuanza kutekeleza hatua za kiusalama chini ya makubaliano ya upatanishi wa Marekani mwezi ujao, nchi hizo zilisema katika taarifa yake ya pamoja siku ya Jumatano, katika kile ambacho kitakuwa ni hatua muhimu katika utekelezaji wa makubaliano hayo ya amani huku kukiwa na wasiwasi juu ya ukosefu wa maendeleo.

Makubaliano hayo yaliyofikiwa katika mkutano wa Washington Septemba 17-18 , yatawezesha kuanza kwa utekelezaji tarehe 1 Oktoba , kwa mujibu wa taarifa ya pamoja, ambayo pia ilitolewa na Marekani, Qatar, Togo na Kamisheni ya Umoja wa Afrika.

Nchi hizo zilikubali kukamilisha hatua hizo ifikapo mwisho wa mwaka, vyanzo vitatu vinavyofahamu suala hilo vililiambia shirika la habari la Reuters.

Operesheni za kuondoa tisho hilo kutoka kwa kundi lenye makao yake makuu nchini Congo la Democratic Forces for the Liberation of Rwanda (FDLR) na kuwezesha kuondolewa kwa wanajeshi wa Rwanda zitaanza kati ya Oktoba 21 na 31, kwa mujibu wa vyanzo.

Ratiba hiyo inatoa tarehe maalum kwa Rwanda na DRC kutekeleza mpango wa amani.

Mawaziri hao wa mambo ya nje wa Congo na Rwanda walitia saini mkataba wa amani mjini Washington Juni 27 na kukutana siku hiyo hiyo na Rais wa Marekani Donald Trump, ambaye ana nia ya kuchota mabilioni ya dola za uwekezaji wa nchi za Magharibi katika eneo lenye utajiri wa tantalum, dhahabu, kobalti, shaba, lithiamu na madini mengine.

Mashambulizi ya Marekani dhidi ya boti za dawa za kulevya ‘kitendo cha dhuluma’ – Rais wa Colombia

.

Mashambulizi ya anga ya Marekani dhidi ya boti zinazodaiwa kusafirisha dawa za kulevya katika Bahari ya Caribbea ni “kitendo cha dhuluma”,

Rais wa Colombia Gustavo Petro aliambia BBC katika mahojiano akitoa wito wa maafisa wa Marekani kufunguliwa mashtaka ya jinai ikiwa uchunguzi utabaini kuwa raia wa Colombia waliuawa katika mashambulizi hayo.

Rais Donald Trump ameyataja mashambulizi hayo, ambayo yameripotiwa kuwaua 17 tangu yaanze mwezi huu, kama hatua ya kukomesha mtiririko wa wa dawa aina ya fentanyl na mihadarati mingine nchini Marekani.

Wataalamu wa sheria na wabunge, hata hivyo, wamehoji ikiwa wanakiuka sheria za kimataifa za haki za binadamu.

“Kwa nini utumia kombora ikiwa unaweza kusimamisha boti kuwakamata wafanyakazi?” Alisema Petro. Vinginevyo “Hayo ni mauaji.”

Akizungumza na BBC siku ya Jumatano, Petro alisema “watu wasiuawa” katika katika operesheni ta kukabiliana na boti za mwendo kasi zinazoaminika kuhusika na ulanguzi wa dawa za kulevya.

Trump ataka uchunguzi ufanyike kuhusu ‘hujuma’ anazodai kufanyiwa Umoja wa Mataifa

,

Donald Trump ametaka uchunguzi ufanyike kuhusu kile alichokiita “hujuma tatu” wakati wa ziara yake kwenye Baraza Kuu la Umoja wa Mataifa siku ya Jumatano.

Katika chapisho kwenye mtandao wa kijamii, rais wa Marekani alitaja tukio la ngazi inayotumia umeme kukwama akiwa na mkewe Melania Trump, kuharibika kwa kifaa cha kumwezeha kusoma hotuba yake, na suala la kusikika kwenye ukumbi kama hujuma.

Afisa wa Umoja wa Mataifa alisema mfumo huo wa sauti uliundwa ili kuwawezesha watu kusikia hotuba zilizotafsiriwa kupitia visikizi.

Trump aliangazia matukio hayo kwenye mtandao wake wa Truth Social na kuongeza kuwa atamuandikia Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa Antonio Guterres kuomba uchunguzi kuanzishwa mara moja.

“Kilichofanyika jana katika Mkutano wa Umoja wa Mataifa ni FEDHEHA – Sio mara moja, au mbwili, bali mara matatu!” aliandika.

“Hii haikuwa bahati mbaya, hii ilikuwa hujuma ya wazi katika ofisi za Umoja wa Mataifa. Wanapaswa kuona haya.”

Pia alitoa wito wa kukamatwa kwa watu waliohusika na tukio la kukwama kwa ngazi, akigusia taarifa ya gazeti la Times ambayo ilisema wafanyakazi wa Umoja wa Mataifa walitania kuhusu kuzima ngazi.

“Hii ilikuwa hujuma ya wazi… Kanda zote za usalama kwenye sehemu ya ngazi ya kuingia kwenue jengo hilo zinapaswa kuhifadhiwa, hasa kitufe cha kusimamisha ngazi kwa dharura,” Trump aliongeza.

Balozi wa Marekani katika Umoja wa Mataifa, Mike Waltz, aliunga mkono wito wa rais wa uchunguzi rasmi, akisema matukio hayo “hayakubaliki”.

All Rights Reserved © The Cantona Group PLC||2025


Discover more from cantonadigital

Subscribe to get the latest posts sent to your email.

Leave a comment