Radio Fortune Africa -Na Cantona Joseph
https://zeno.fm/radio/radio-fortune-africa

Vikosi vya kijeshi vya Belarusi na Urusi vinashiriki katika mazoezi ya pamoja kwenye uwanja wa Borisovsky, tukio ambalo linashuhudiwa na vyombo habari vya kimataifa.
Katika uwanja mkubwa wa maili 45 (72km) kutoka mji mkuu wa Belarus Minsk, vita vinaendelea.
Kuna milipuko mikubwa huku washambuliaji wa Sukhoi-34 wakidondosha mabomu. Moshi mwingi unafanya anga kuwa giza.
Eneo lote linatoa mwangwi na makombora ya mizinga yanayolipuka. Helikopta ya kijeshi ya kivita inajiunga na shambulio hilo, huku ndege zisizo na rubani zikitanda angani kutazama uharibifu.
Haya yote ni mazoezi tu. Ni sehemu ya mazoezi ya kijeshi ya Zapad-2025 (“West 2025”). Maafisa wengine wa kijeshi kutoka balozi mbalimbali pia walikuwepo kushuhudia kinachoendelea.
Haya ni mazoezi yaliyopangwa ya “West 2025” ambayo hufanyika kila baada ya miaka minne.
Moscow na Minsk zinashikilia kuwa mazoezi hayo ni ya kujilinda tu, kwamba yameandaliwa ili kuimarisha usalama wa Urusi na Belarusi na kukabiliana na tishio lolote la nje linaloweza kutokea.
Madai kama hayo yalisikika miaka mitatu na nusu iliyopita.
Mnamo Februari 2022 BBC ilitembelea Belarusi ili kuripoti juu ya mazoezi ya kijeshi ya Belarusi-Urusi.
Zoezi hilo lilipokamilika, badala ya kurejea nyumbani wanajeshi wa Urusi walivamia nchi jirani ya Ukraine kutoka eneo la Belarus.
Wakati huu Belarus inasisitiza kuwa haina chochote cha kujificha.
China yafyatua maji ya kuwasha kwenye meli za Ufilipino katika Bahari ya China Kusini

Walinzi wa Pwani wa China wamefyatua maji ya kuwasha siku ya Jumanne kwenye meli za Ufilipino karibu na eneo linalozozaniwa la Scarborough katika Bahari ya China Kusini, wakishutumu Ufilipino kwa uvamizi na kugonga moja ya meli zake.
Makabiliano hayo yanatokea wiki moja baada ya China kuidhinisha mipango ya kugeuza eneo hilo kuwa hifadhi ya asili ya kitaifa hatua ambayo inaweza kusababisha mzozo na Ufilipino.
Kuongezeka kwa mvutano juu ya eneo hilo kumesababisha mizozo ya kidiplomasia kati yao katika miaka ya hivi karibuni.
Pande zote mbili zinashutumu kila mmoja kwa uchochezi na uingiliaji haramu katika matukio yanayohusiana na matumizi ya maji ya kuwasha, kugonga meli nyingine na ujanja na Walinzi wa Pwani ya China, Ufilipino ikichukulia hali hiyo kuwa nusura isababishe hatari.
Mvutano wa Jumanne ulihusisha zaidi ya meli 10 za Ufilipino, alisema Gan Yu, msemaji wa Walinzi wa Pwani ya China, akishutumu meli hizo kwa “kuvamia kinyume cha sheria eneo la maji la China la Scarborough kutoka pande tofauti”.
Mahakama yatoa amri ya kukamatwa Muingereza aliyeshtakiwa kwa mauaji ya Agnes Wanjiru
Mahakama Kuu nchini Kenya imetoa hati ya kukamatwa kwa raia wa Uingereza aliyeshtakiwa kwa mauaji ya Agnes Wanjiru mwenye umri wa miaka 21 mjini Nanyuki zaidi ya miaka kumi iliyopita.
Waendesha mashtaka wanasema Wanjiru aliuawa katika nyumba ya kulala wageni mnamo Machi 2012 na mwili wake baadaye ukapatikana kwenye shimo la maji taka.
Mshtakiwa huyo ambaye alifunguliwa mashtaka kwa mauaji, alishindwa kufika mahakamani, hatua ambayo ilifanya amri kesi ya kumrejeshwa nchini kutoka Uingereza kuanza.
Mji wa Nanyuki uliopo katika Kaunti ya Laikipia, ni makao ya kituo cha kijeshi cha muda mrefu cha Uingereza, na kesi hiyo imeibua hasira ya umma nchini Kenya.
Mahakama pia ilifahamishwa kwamba mashahidi walioko Uingereza watapatikana kwa ajili ya kusikilizwa.
Jaji amevizuia vyombo vya habari kuchapisha majina ya mshukiwa au mashahidi, ili kulinda uadilifu wa mchakato wa mahakama.
Vijana wa China kulipa $300,000 kwa kukojoa kwenye supu

Vijana wawili ambao walikojoa kwenye sufuria ya mchuzi kwenye mkahawa mmoja wameagizwa kulipa Yuan 2.2m ($309,000; £227,000) kwa kampuni mbili za upishi nchini Uchina.
Tukio hilo, lililotokea Februari katika tawi la Shanghai la kampuni kubwa ya Uchina ya Haidilao na lilisababisha ukosoaji mkubwa baada ya vijana hao wa miaka 17 kuchapisha video ya kitendo chao mtandaoni.
Hakuna kilichoonyesha kwamba kuna mtu yeyote aliyekunywa supu hiyo iliyokojolewa lakini mgahawa wa Haidilao ulikuwa amejitolea kulipa maelfu ya waliokula katika mkahawa huo siku zilizofuata.
Mnamo mwezi Machi, Haidilao ilisema imeingia hasara ya zaidi ya Yuan 23m, kama kiasi ambacho kilifidia wateja juu ya tukio hilo.
Israeli yaanzisha mashambulizi ya ardhini kuuteka mji wa Gaza, Axios inaripoti

Jeshi la Israeli limeanzisha mashambulizi ya ardhini leo Jumatatu ili kuuteka mji wa Gaza, Axios iliripoti, ikinukuu maafisa wa Israeli.
Jeshi la Israeli halikujibu mara moja ombi la kutoa maoni kuhusu hatua hiyo iliyoripotiwa, ambayo inakuja baada ya wiki kadhaa za mashambulizi makali ya Israel katika mji huo.
Waziri Mkuu wa Israel Benjamin Netanyahu aliamuru wanajeshi mwezi uliopita kuuteka mji wa Gaza, ambao anautaja kuwa ngome ya kundi la wanamgambo wa Hamas ambalo lilianzisha shambulizi ya ghafla Oktoba 2023 dhidi ya Israel.
Jeshi tangu wakati huo limeuzingira Ukanda wa Gaza, na kusababisha janga la kibinadamu na uharibifu mkubwa, uhamishaji wa watu wengi na uhaba mkubwa wa chakula na maji.
Vikosi vya Israel vimekuwa vikiendesha operesheni zake kwenye viunga vya mji wa Gaza kwa wiki kadhaa, vikikaribia katikati mwa mji huo ambapo takriban Wapalestina milioni 1 walikuwa wametafuta hifadhi mwezi uliopita.
“Gaza inaungua,” Waziri wa Ulinzi wa Israeli Israel Katz alisema katika ujumbe kwenye mtandao wa X mapema Jumanne. “IDF inashambulia kwa nguvu kwenye miundombinu ya kigaidi na wanajeshi wa IDF wanapigana kwa ujasiri ili kutengeneza mazingira ya kuachiliwa kwa mateka na kushindwa kwa Hamas.”
Mshukiwa wa Charlie Kirk ahusishwa na eneo la uhalifu kwa DNA, asema mkuu wa FBI

DNA kwenye taulo iliyozungushiwa bunduki inayoshukiwa kutumika kumuua Charlie Kirk imelingana na DNA ya mshukiwa aliye kizuizini, mkurugenzi wa FBI amesema siku ya Jumatatu.
Tyler Robinson, 22, alikamatwa kufuatia kifo cha Kirk katika hafla kwenye Chuo Kikuu cha Utah Valley mnamo Jumatano. Bunduki aina ya ‘bolt-action’ ilipatikana karibu na eneo la tukio huku bisibisi ikionekana kwenye paa ambapo risasi iliyomuua mfuasi huyo ilifyatuliwa.
“Naweza kusema leo kwamba DNA iliyokuwa kwenye taulo iliyofungwa kwenye bunduki na DNA kwenye bisibisi zimelingana na ile ya mshukiwa aliye kizuizini,” Kash Patel aliiambia Fox and Friends.
Mashtaka rasmi yanatarajiwa wiki hii.
Mkurugenzi wa FBI – ambaye anatarajiwa kuhojiwa katika kikao cha Bunge siku ya Jumanne – pia alitaja barua iliyogunduliwa nyumbani kwa mshukiwa, ambayo iliapa “kumuondoa” Kirk.
“Kimsingi inasema… ‘Nina fursa ya kumuondoa Charlie Kirk’, na nitatumia fursa hiyo. Maelezo hayo yaliandikwa kabla ya Kirk kupigwa risasi,” alisema Patel.
Aliongeza, “ingawa imeharibiwa, tumepata ushahidi wa kitaalamu wa barua hiyo”.
All Rights Reserved © The Cantona Group PLC||2025
Discover more from cantonadigital
Subscribe to get the latest posts sent to your email.