Radio Fortune Africa -Na Cantona Joseph
https://zeno.fm/radio/radio-fortune-africa

Mamia ya wafuasi na wasio wafuasi wa Chama ACT Wazalendo walikuwepo katika Mahakama Kuu, Masijala kuu ya Dodoma kufuatilia uamuzi wa shauri la Luhaga Mpina.
Luhaga Mpina ameshinda shauri la kupinga kuenguliwa kugombea urais wa Tanzania kwa tikiti ya ACT Wazalendo.
Uamuzi huo umetolewa na majaji watatu wa Mahakama Kuu ya Tanzania jijini Dodoma muda mfupi uliopita.
Mamia ya wafuasi na wasio wafuasi wa Chama ACT Wazalendo walikuwepo katika Mahakama Kuu, Masijala kuu ya Dodoma kufuatilia uamuzi wa shauri la Luhaga Mpina.
Baadhi ya wanasiasa mashuhuri akiwemo kiongozi mkuu wa zamani wa ACT, Zitto Kabwe ni miongoni mwa waliofika kufuatilia uamuzi wa shauri lililofunguliwa na ACT Wazalendo dhidi ya Ofisi ya Mwanasheria Mkuu wa Serikali na Tume Huru ya Taifa ya Uchaguzi nchini Tanzania.
Shauri hilo ambalo lilifunguliwa na bodi ya wadhamani ya ACT Wazalendo na mgombea mteule wa kiti cha urais kupitia chama hicho lilipinga kuondolewa kwa Mpina kwenye mchakato wa uchaguzi Mkuu kwa kuzuiwa kurejesha fomu ya kuomba uteuzi wa kugombea nafasi ya urais.
Shauri hili ambalo lilifunguliwa kwa hati ya dharura lilisikilizwa na jopo la majaji watatu likiongozwa na Abdi Kagomba, Evaristo Longopa na John Kahyoza.
Ufaransa inashuku ujasusi wa kigeni umehusika na vichwa vya nguruwe vilivyoachwa nje ya misikiti

Polisi wa Ufaransa wanashuku kuwa watu walioweka vichwa vya nguruwe nje ya misikiti ya Paris Jumatatu usiku walikuwa wakifanya kazi chini ya maagizo kutoka kwa idara ya kijasusi ya kigeni, pengine Urusi.
Vichwa hivyo vilipatikana Jumanne asubuhi nje ya misikiti tisa katikati mwa Paris na vitongoji vya jirani, na kusababisha wimbi la hasira na lawama.
Lakini wachunguzi sasa wamesema watu wawili waliohusika waliendesha gari lililosajiliwa na Serb, walitumia simu ya rununu ya Croatia, na kuvuka hadi Ubelgiji saa chache baadaye.
Tukio hilo lina mfanano wa kushangaza na uchochezi mwingine wa hivi majuzi – haswa ule unaojulikana kama Star of David kwenye kuta za Paris mnamo Oktoba 2023, na uchoraji wa mikono rangi nyekundu kwenye ukumbusho wa Maangamizi ya Wayahudi mnamo Mei 2024.
Israeli yatishia kuwaua viongozi wa Hamas waliosalia Qatar

Waziri Mkuu wa Israeli, Benjamin Netanyahu, ametishia kuwaua tena viongozi wa Hamas walioko nchini Qatar iwapo Doha haitawafukuza maafisa hao, na kusababisha majibu makali kutoka kwa serikali ya Qatar.
Pamoja na ukosoaji huo wa kimataifa kuhusu shambulio lililotokea katika mji mkuu wa Qatar inaarifiwa kuwa Netanyahu hajatetereshwa kwa namna yoyote.
Netanyahu amesema siku ya Jumatano kwamba mataifa yanapaswa “kuipongeza” Israel kwa mashambulizi yake ya mabomu na mauaji katika maeneo mbalimbali ya Mashariki ya Kati.
Kauli hizo zilitolewa siku moja baada ya Israel kufanya shambulio lisilo la kawaida ndani ya Qatar, kwa kuwalenga viongozi waandamizi wa Hamas walioko Doha, wakati mazungumzo kuhusu pendekezo la kusitisha mapigano lililoungwa mkono na Marekani yakiendelea.
Katika taarifa yake, Wizara ya Mambo ya Nje ya Qatar imelaani vikali kauli za Waziri Mkuu huyo wa Israeli, ikizitaja kama “jaribio la aibu … la kuhalalisha shambulio la kinyonge dhidi ya ardhi ya Qatar, pamoja na vitisho vya wazi vya kuvunja tena mamlaka ya kitaifa ya nchi.”
“Netanyahu anafahamu vyema kuwa ofisi ya Hamas ilifunguliwa nchini Qatar katika muktadha wa juhudi za upatanishi zilizopigiwa chapuo na Marekani pamoja na Israel,” Taarifa hiyo imeeleza.
“Kauli kama hizi si jambo la kushangaza kutoka kwa mtu anayejiegemeza katika misimamo mikali ili kupata ushindi wa kisiasa, huku akiwa anatafutwa na vyombo vya sheria za kimataifa, akikabiliwa na vikwazo vinavyozidi kuongezeka kila uchao hali inayozidi kumtenga katika jukwaa la kimataifa,” Taarifa hiyo iliongeza.
Wakati hayo yakijiri, ikumbukwe kwamba ndani ya kipindi cha siku tatu pekee, Israel imefanya mashambulizi katika maeneo ya Gaza, Lebanon, Yemen, Syria, Tunisia na Qatar, huku ikiendeleza uvamizi wa kila siku katika Ukingo wa Magharibi unaokaliwa kwa mabavu na siku ya Jumatano, Israeli iliwaua watu 35 katika shambulio nchini Yemen.
Chelsea yakabiliwa na mashtaka 74 kuhusu malipo ya wakala

Chelsea imeshtakiwa na Chama cha Soka kwa madai ya kukiuka sheria 74 zinazohusiana na malipo kwa mawakala kati ya 2009 na 2022.
Gharama hizo kimsingi zinalenga matukio yaliyotokea kati ya misimu ya 2010-11 na 2015-16.
Bwenyenye wa Urusi Roman Abramovich alikuwa akiidhibiti klabu hiyo kuanzia 2003 hadi 2022, kabla ya kuiuza Chelsea kwa muungano ulioongozwa na mwekezaji Mmarekani Todd Boehly na kampuni ya kibinafsi ya Clearlake Capital.
Sheria hiyo inadaiwa kukiuka mawakala, wapatanishi na uwawekezaji wengine kwa wachezaji.
Chelsea, ambao walisema wameripoti ukiukaji wa sheria unaowezekana kwa FA wenyewe, wana hadi Septemba 19 kujibu.
Kuna machaguo mawili ya kuiadhibu Chelsea, ikiwa ni pamoja na faini, vikwazo vya uhamisho na kukatwa pointi. Hata hivyo, ushirikiano wa hali ya juu wa The Blues utazingatiwa.
All Rights Reserved © The Cantona Group PLC||2025
Discover more from cantonadigital
Subscribe to get the latest posts sent to your email.