“ It wasn’t raining when Noah built the ark”

Radio Fortune Africa -Na Cantona Joseph

https://zeno.fm/radio/radio-fortune-africa

Mwandishi maarufu na mshauri wa mambo ya kifedha Howard Ruff aliwahi kusema kuwa…

It wasn’t raining when Noah built the ark”

(Wakati Nuhu Anajenga Safina Mvua haikuwa inanyesha).

Msemo huu una maana kubwa sana kwa kila anayetaka mafanikio.

Tabia ya watu wengi sana ni kuanza kujiandaa pale wanapoziona fursa ama zinapowakaribia.

Ukiwa wa namna hii utajikuta kila siku unachelewa.

Wakati sahihi wa kujenga safina ni wakati ambako hakuna mvua.

Usisubiri usikie kuna kupandishwa cheo ndio uanze kutafuta kuongeza elimu.

Usisubiri uambiwe kuna mchongo ndio uanze kutafuta ujuzi.

Jiulize sasa hivi unahitaji nini?

Na anza kufanyia kazi ili fursa yako inapokuja ikukute ukiwa tayari.

Kuna watu wanadhani muda ambao hawana kitu cha kufanya basi ni muda wa kulala siku nzima…

.

…kuzurura ama kuangalia movie tu n.k

Ukijigundua uko kwenye kipindi kinachoonekana kama hauna cha kufanya, kumbuka ni muda wa kujiandaa Mungu amekupa.

Usiutumie vibaya, kwa sababu kuna fursa iko njiani itakuja baada ya hapo.

All Rights Reserved © The Cantona Group PLC||2025


Discover more from cantonadigital

Subscribe to get the latest posts sent to your email.

Leave a comment