15 wafariki katika mlipuko wa bomu la kujitoa mhanga nchini Pakistan

Radio Fortune Africa -Na Cantona Joseph

https://zeno.fm/radio/radio-fortune-africa

Mlipuko huo ulitokea katika eneo la kuegesha magari la uwanja ambapo mkutano wa kisiasa ulikuwa umefanyika
Maelezo ya picha,Mlipuko huo ulitokea katika eneo la kuegesha magari la uwanja ambapo mkutano wa kisiasa ulikuwa umefanyika.

Watu 15 wamefariki na wengine zaidi ya 30 kujeruhiwa katika shambulio la bomu la kujitoa mhanga karibu na mkutano wa kisiasa nchini Pakistan, mamlaka ilisema.

Mamia ya wanachama wa Chama cha Kitaifa cha Balochistan (BNP) walikuwa wakihudhuria mkutano katika uwanja wa michezo wa Quetta, mji mkuu wa jimbo la Balochistan, wakati bomu lilipolipuka katika eneo la kuegesha magari Jumanne usiku.

Mamlaka za mkoa zilisema Jumatano kwamba idadi ya waliofariki imeongezeka hadi 15.

Kundi la wanamgambo wa Islamic State limedai kutekeleza shambulio hilo.

Balochistan, ambayo inapakana na Afghanistan na Iran, ni eneo kubwa na maskini zaidi nchini humo.

Wakaazi wake pia wanakabiliwa na mashambulizi ya mara kwa mara kutoka kwa Islamic State na makundi yanayotaka kujitenga.

Mshambuliaji wa kujitoa mhanga hakuweza kufika eneo la mkutano kutokana na ulinzi mkali, waziri wa afya wa Balochistan Bakht Muhammad Kakar alisema, kulingana na mtandao wa Pakistan wa Geo News.

‘Mwezi wa damu’ kushuhudiwa Afrika wikendi hii

.

‘Mwezi wa damu’ utashuhudiwa angani wikendi hii, kutokana na kupatwa kamili kwa mwezi.

Watakaokuwa na fursa ya kutazama mwezi huo angani wataona mwezi wote ukibadilika kuwa rangi ya wekundu Septemba 7, 2025.

Kupatwa kwa mwezi kutaonekana katika sehemu za Afrika, Asia, Australia na Ulaya.

Tofauti na matukio mengine ya kupatwa kwa mwezi ambako mtazamaji huitaji miwani maalum na vifaa vingine ili kuweza kutazama angani, kupatwa huku kwa mwezi kunaweza kuonekana kwa urahisi: hakuhitaji muda maalum, vifaa, ujuzi au mpangilio.

Mtazamaji atatazama moja kwa moja kwenye Mwezi wakati tukio hilo linatokea.

Tukio hili adimu litaonekana kwa zaidi ya watu bilioni saba duniani kote, huku takriban bilioni 6.2 wakiweza kushuhudia tukio lote kuanzia mwanzo hadi mwisho.

Kupatwa kwa jua siku hiyo itakuwa ndio tukio refu zaidi la kupatwa kwa mwezi tangu 2022, likiwa na jumla ya saa 1 na dakika 22, ambapo Mwezi utakuwa na rangi nyekundu ya wekundu.

Iran iliongeza hifadhi ya urani hadi kiwango cha silaha, shirika la UN linasema

.

Ripoti ya siri ya shirika la Umoja wa Mataifa la kudhibiti nyuklia ilisambazwa kwa nchi wanachama na kuonekana na Shirika la Habari la Associated Press ilisema Jumatano kwamba Iran iliongeza hifadhi yake ya madini ya urani yaliorutubishwa hadi kufikia viwango vya silaha kabla ya Israel kuanzisha mashambulizi yake ya kijeshi Juni 13.

Ripoti ya Shirika la Kimataifa la Nishati ya Atomiki (IAEA) lenye makao yake makuu mjini Vienna imesema hadi kufikia Juni 13, Iran ilikuwa na kilo 440.9 (pauni 972) za uranium iliyorutubishwa hadi asilimia 60, ikiwa ni ongezeko la kilo 32.3 (pauni 71.2) tangu ripoti ya mwisho ya IAEA mwezi Mei.

Ripoti hiyo ilisema kwamba takwimu hii “inatokana na habari iliyotolewa na Iran, shughuli za uhakiki wa shirika hilo kati ya 17 Mei 2025 na 12 Juni 2025 (siku iliyotangulia kuanza kwa mashambulio ya kijeshi), na makadirio kulingana na operesheni ya zamani ya vituo husika.”

Hatua hiyo imesalia kiwango kidogo tu kufikia silaha cha 90%.

Kulingana na IAEA, takriban kilo 42 za 60% ya madini ya urani iliyorutubishwa kinadharia inatosha kuzalisha bomu moja la atomiki, ikiwa itarutubishwa zaidi hadi 90%.

All Rights Reserved © The Cantona Group PLC||2025


Discover more from cantonadigital

Subscribe to get the latest posts sent to your email.

Leave a comment