Radio Fortune Africa -Na Cantona Joseph
https://zeno.fm/radio/radio-fortune-africa
Mvua kubwa ilisababisha maporomoko ya ardhi siku ya Jumapili, huku sehemu nyingi za kijiji cha Tarasin zikishuhudia “maafa” makubwa, limesema kundi la waasi la Sudan Liberation Movement/Army.

Maporomoko ya ardhi yamesababisha vifo vya takriban watu 1,000 katika milima ya Marra magharibi mwa Sudan, kulingana na kundi la waasi la Sudan Liberation Movement/Army.
Mvua kubwa ilisababisha maporomoko ya ardhi siku ya Jumapili, huku aliyenusurika akiwa mtu mmoja tu wakati sehemu nyingi za kijiji cha Tarasin zikishuhudia “maafa” makubwa, kundi hilo lilisema katika taarifa.
Kundi hilo limeomba msaada wa kibinadamu kutoka kwa Umoja wa Mataifa na mashirika mengine ya kikanda na kimataifa.
Wakazi wengi katika jimbo la Darfur Kaskazini walikuwa wametafuta hifadhi katika eneo la Milima ya Marra, baada ya vita kati ya jeshi la Sudan na Vikosi vya Rapid Support Forces (RSF) kuwalazimisha kuondoka makwao.
Putin asifu uhusiano ‘wa kipekee’ na China wakati wa kuanza kwa mazungumzo ya viongozi hao

Rais Xi Jinping wa China na mwenzake wa Urusi Vladimir Putin wameanza mazungumzo ya pande mbili mjini Beijing, mkesha wa sherehe ya gwaride kubwa la kijeshi katika mji mkuu wa China.
Putin alipongeza uhusiano kati ya nchi hizo, akisema uko katika “kiwango cha kipekee”.
“Rafiki mpendwa, mimi na wajumbe wote wa Urusi tunafurahi kukutana tena na marafiki na wafanyakazi wenzetu wa China,” Putin alimwambia Xi, kulingana na video iliyochapishwa kwenye Telegram katika akaunti rasmi ya Urusi.
“Mawasiliano yetu ya karibu yanaonyesha hali ya kimkakati ya uhusiano wa Urusi na China, ambao uko katika kiwango cha juu sana,” aliongeza.
“Siku zote tulikuwa pamoja wakati huo, na bado tuko pamoja hadi sasa.”
Xi alimwambia Putin kwamba “uhusiano kati ya China na Urusi umestahimili jaribio la mabadiliko ya kimataifa” – akiongeza kuwa Beijing iko tayari kufanya kazi na Moscow “kukuza ujenzi wa mfumo wa utawala wa kimataifa wenye haki na busara”.
Xi anatazamiwa kuwa mwenyeji wa gwaride kubwa zaidi la kijeshi nchini China siku ya Jumatano, ambalo litaadhimisha miaka 80 tangu Wajapani walipojisalimisha nchini China mwishoni mwa Vita vya Pili vya Dunia.
Kiongozi wa Korea Kaskazini yuko China kuhudhuria gwaride la kijeshi

Kiongozi wa Korea Kaskazini Kim Jong Un amesafiri kwenda China kwa treni kuhudhuria gwaride kubwa la kijeshi, vyombo vya habari vya serikali ya Korea Kaskazini vilisema Jumanne.
Kim Jong Un anatarajiwa kuungana na Rais wa China Xi Jinping, Rais wa Urusi Vladimir Putin na viongozi wengine wa dunia katika tukio hilo la kihistoria.
Gwaride hilo la dakika 70 huenda likaonyesha silaha za hivi karibuni zaidi za China, zikiwemo mamia ya ndege, vifaru na mifumo ya kuzuia ndege zisizo na rubani – mara ya kwanza muundo mpya wa jeshi lake unaonyeshwa kikamilifu katika gwaride.
Kiongozi huyo aliyejitenga husafiri mara chache sana, huku mawasiliano yake ya hivi majuzi na viongozi wa dunia yakimhusisha Putin, ambaye amekutana naye mara mbili tangu uvamizi wa Urusi nchini Ukraine.
Korea Kaskazini Jumatatu ilionyesha kuunga mkono matamshi yaliyotolewa na Xi katika mkutano wa kilele unaotaka utawala mzuri wa ulimwengu, na kuongeza kuwa ushirikiano kati ya Korea Kaskazini na China utakua kwa sababu ya masuala kama hayo, kulingana na Makamu wa Mambo ya nje aliyetoa maoni yake katika tovuti ya wizara ya Wizara ya Mambo ya nje ya Korea Kaskazini.
Makumi kwa maelfu ya wanajeshi watashiriki gwaride hilo maalum litakalofanyika uwanja wa kihistoria wa Tiananmen Square mjini Beijing, kuadhimisha miaka 80 ya Japan kujisalimisha katika Vita vya Pili vya Dunia na kumalizika kwa mzozo huo.
Viongozi wengi wa Magharibi hawatarajiwi kuhudhuria gwaride hilo, kwa sababu ya kupinga kwao uvamizi wa Urusi wa Ukraine, ambao umesababisha vikwazo dhidi ya serikali ya Putin.
Kiongozi wa Korea Kaskazini yuko China kuhudhuria gwaride la kijeshi
Kiongozi wa Korea Kaskazini Kim Jong Un amesafiri kwenda China kwa treni kuhudhuria gwaride kubwa la kijeshi, vyombo vya habari vya serikali ya Korea Kaskazini vilisema Jumanne.
Kim Jong Un anatarajiwa kuungana na Rais wa China Xi Jinping, Rais wa Urusi Vladimir Putin na viongozi wengine wa dunia katika tukio hilo la kihistoria ambapo China itaonesha nguvu zake za kijeshi.
Korea Kaskazini Jumatatu ilionyesha kuunga mkono matamshi yaliyotolewa na Xi katika mkutano wa kilele unaotaka utawala mzuri wa ulimwengu, na kuongeza kuwa ushirikiano kati ya Korea Kaskazini na China utakua kwa sababu ya masuala kama hayo, kulingana na Makamu wa Mambo ya nje aliyetoa maoni yake katika tovuti ya wizara ya Wizara ya Mambo ya nje ya Korea Kaskazini.
Ubelgiji kutambua taifa la Palestina katika Mkutano wa UN, asema waziri wa mambo ya nje

Ubelgiji itatambua taifa la Palestina katika Mkutano Mkuu wa Umoja wa Mataifa mnamo mwezi Septemba, waziri wake wa mambo ya nje amesema.
“Palestina itatambuliwa na Ubelgiji katika kikao cha Umoja wa Mataifa! Na vikwazo vikali vitawekwa dhidi ya serikali ya Israel,” Waziri wa Mambo ya Nje Maxime Prevot ameandika kwenye mtandao wa X.
Mnamo mwezi Julai, Rais wa Ufaransa Emmanuel Macron alisema Ufaransa itatambua taifa la Palestina katika mkutano wa Umoja wa Mataifa, unaotarajiwa kufanyika kuanzia Septemba 9 hadi 23 mjini New York.
Zaidi ya nchi kumi za Magharibi zimetoa wito kwa wengine kufanya hivyo.
Prevot alisema uamuzi huo ulikuja “kutokana na janga la kibinadamu” linalotokea Gaza, ambapo mashambulizi ya Israel yamewafanya watu wengi kuwa wakimbizi angalau mara moja.
“Katika kukabiliana na ghasia zinazofanywa na Israel kwa kukiuka sheria za kimataifa, ikizingatiwa majukumu yake ya kimataifa, ikiwa ni pamoja na wajibu wa kuzuia hatari yoyote ya mauaji ya halaiki, Ubelgiji ilipaswa kuchukua maamuzi magumu ili kuongeza shinikizo kwa serikali ya Israel na Hamas,” Prevot aliandika.
“Hili halihusiani kwa vyovyote na kuwaadhibu watu wa Israel, lakini ni kuhakikisha kuwa serikali yake inaheshimu sheria za kimataifa na za kibinadamu na kuchukua hatua kujaribu kubadilisha hali hiyo,” aliongeza.
Jitihada za uokoaji zinaendelea baada ya tetemeko la ardhi la Afghanistan kuua zaidi ya watu 800

Juhudi za uokoaji za Afghanistan zikianza tena asubuhi ya leo, takriban watu 800 wakifariki katika mojawapo ya matetemeko mabaya zaidi ya ardhi nchini humo siku ya Jumapili.
Kuna hofu kwamba idadi ya vifo itaongezeka kwa kiasi kikubwa kwani eneo lililoathiriwa zaidi ni la mbali na milima, na kufanya shughuli za uokoaji kuwa ngumu.
Vifo vingi vilitokea katika mkoa wa milima wa Kunar, ambao ulikuwa karibu zaidi na kitovu cha tetemeko la ardhi la ukubwa wa 6.0 lilipotokea Jumapili usiku.
Uingereza imetoa msaada wa dharura wa £1m ($1.35m), huku Ofisi ya Mambo ya Nje ikisisitiza itapitisha msaada huo kupitia washirika wake ili kuhakikisha kwamba hauendi kwa utawala wa Taliban unaotawala nchi hiyo ya Asia Kusini.
Idadi ya mataifa mengine – ikiwa ni pamoja na China, India na Uswizi – yameahidi kutoa misaada.
Umoja wa Mataifa imetoa $5m (£3.7m) kutoka kwa hazina yake ya kimataifa ya kukabiliana na dharura.
Israel inatekeleza mauaji ya halaiki huko Gaza, wataalam wakuu duniani wanasema

Jumuiya kuu duniani ya wataalam imetangaza kuwa Israel inatekeleza mauaji ya kimbari huko Gaza.
Azimio lililopitishwa na Jumuiya ya Kimataifa ya Wanazuoni wa Mauaji ya Kimbari (IAGS) linasema kuwa mwenendo wa Israel unakidhi ufafanuzi wa kisheria kama ilivyoainishwa katika mkataba wa Umoja wa Mataifa kuhusu mauaji ya kimbari.
Katika azimio la kurasa tatu, IAGS inawasilisha orodha ya hatua zilizochukuliwa na Israel katika muda wote wa vita vya miezi 22 ambayo inatambua kuwa ni mauaji ya kimbari, uhalifu wa kivita na uhalifu dhidi ya binadamu.
IAGS ni jumuiya kubwa zaidi ya kitaaluma duniani ya wasomi wa mauaji ya halaiki na inajumuisha idadi ya wataalam wa Holocaust. Kati ya wanachama wake 500, 28% walishiriki katika kura hiyo na 86% ya waliopiga kura waliunga mkono azimio hilo.
Katika muhtasari wa sera na hatua za Israeli, azimio hilo linabainisha mashambulizi yaliyoenea kwa wafanyakazi na sekta muhimu kwa ajili ya kuendelea kuishi, ikiwa ni pamoja na katika sekta ya afya, misaada na elimu.
Miongoni mwa mambo mengine mengi, inabainisha watoto 50,000 waliouawa au kujeruhiwa na Israel, kama ilivyoangaziwa na shirika la Umoja wa Mataifa linalosimamia maslahi ya watoto (Unicef), ambalo linachangia uwezo wa Wapalestina huko Gaza kuishi kama kikundi na kuzaliana.
Azimio hilo pia linaangazia uungwaji mkono kati ya viongozi wa Israel kwa kuwatimua kwa lazima Wapalestina wote kutoka Gaza, pamoja na hatua ya Israel ya kubomoa kabisa makazi katika eneo hilo.
All Rights Reserved © The Cantona Group PLC||2025
Discover more from cantonadigital
Subscribe to get the latest posts sent to your email.