Urafiki wenye Tija

Radio Fortune Africa -Na Cantona Joseph

https://zeno.fm/radio/radio-fortune-africa

Rafiki yako akiwa na biashara USIWE MSTARI wa mbele kukopa bila kulipa, au kutumia bila kugharamia.

Usigeuze sehemu ya biashara ya rafiki yako kuwa kijiwe hadi unafukuza wateja wengine.

Ukienda basi nunua kitu usisubiri kupewa bure.

Uwe mtu wa kwanza KUMSAPOTI ili ainuke, umchangie ili asimame, aone faida yako kwake ni kuinuka na sio kumzamisha.

Kama hauna sababu ya msingi ya kununua kwa wengine, basi nunua kwake ili azidi kusonga mbele.

Waache wengine wakope ili wewe jitahidi kutoa “cash”, uwe rafiki unayemuinua.

Je, marafiki zako wamekuwa sehemu ya kusapoti unachofanya au…

Wanatumia urafiki kama sehemu ya kukukwamisha?

Kama umependa makala hii tafadhali share na wengine.

All Rights Reserved © The Cantona Group PLC||2025


Discover more from cantonadigital

Subscribe to get the latest posts sent to your email.

Leave a comment