Marekani yamzuia kiongozi wa Palestina kuhudhuria mkutano wa Umoja wa Mataifa mjini New York

Radio Fortune Africa -Na Cantona Joseph

https://zeno.fm/radio/radio-fortune-africa

Rais wa Palestina Mahmoud Abbas amezuiwa kuhudhuria kikao cha Baraza Kuu la Umoja wa Mataifa mjini New York mwezi ujao baada ya yeye na maafisa wengine 80 wa Palestina kufutiwa viza zao, wizara ya mambo ya nje ya Marekani imethibitisha.

Mahakama ya Marekani yasema ushuru mwingi aliouweka Trump kwa mataifa ni kinyume cha sheria

g

Mahakama ya rufaa nchini Marekani imeamua kuwa ushuru mwingi uliotolewa na Rais wa Marekani Donald Trump ni kinyume cha sheria, hivyo basi kutayarisha mpambano wa kisheria ambao unaweza kuathiri ajenda yake ya sera za kigeni.

Uamuzi huo unaathiri ushuru wa Trump, uliowekwa kwa nchi nyingi ulimwenguni, pamoja na ushuru mwingine uliowekwa kwa nchi za China, Mexico na Canada.

Katika uamuzi wa Mahakama ya Rufaa ya Marekani ya shirikisho ilikataa hoja ya Trump kwamba ushuru huo unaruhusiwa chini ya sheria ya dharura ya nguvu za kiuchumi, ikiziita “batili na kinyume cha sheria”.

Uamuzi huo hautaanza kutekelezwa hadi tarehe 14 Oktoba ili kuwapa muda watawala kuitaka Mahakama ya Juu zaidi kushughulikia kesi hiyo.

Trump aliikosoa mahakama ya rufaa na uamuzi wake akisema: “Ikiwa itaruhusiwa kusimamishwa, uamuzi huu utaangamiza Marekani kihalisi.”

“Leo Mahakama ya Rufaa ya Wanachama wa Juu ilisema kimakosa kwamba ushuru wetu unapaswa kuondolewa, lakini wanajua Marekani itashinda mwishowe,” aliandika.

“Kama ushuru huu utasitishwa, litakuwa janga kubwa kwa nchi. Itatufanya kuwa dhaifu kifedha, na inabidi tuwe na nguvu.”

Kizuizi kinajengwa kuzunguka mji wa Sudan uliozingirwa, picha za satelaiti zinaonyesha

h
Maelezo ya picha,Kushoto: Picha ya setilaiti ya kijiji cha Alsen, magharibi mwa el-Fasher, iliyopigwa tarehe 6 Julai. Kulia: Picha ya tarehe 24 Julai inayoonyesha sehemu ya ukuta iliyojengwa kupitia kwenye makazi

Ukuta mkubwa wa udongo unajengwa kuzunguka mji uliozingirwa wa Sudan wa el-Fasher na unakusudiwa kuwafungia watu ndani, kulingana na utafiti kutoka Chuo Kikuu cha Yale.

Kulingana na picha za satelaiti, Maabara ya Utafiti wa Kibinadamu ya chuo kikuu imetambua zaidi ya kilomita 31 (maili 19) za “berms” – au ardhi zilizoinuliwa – zilizojengwa tangu Mei katika eneo nje ya jiji linalokaliwa na Wanajeshi wa kikosi cha dharura (RSF).

El-Fasher, iliyozingirwa kwa zaidi ya mwaka mmoja, ni kituo kikuu cha mwisho huko Darfur kwa jeshi, ambalo limekuwa likipambana na wapiganaji wa RSF tangu Aprili 2023.

Mtandao wa Madaktari wa Sudan umeiambia BBC kuwa RSF inazidisha mashambulizi yake huko na kuwalenga raia kimakusudi.

Kesi ya talaka ya Jose Chameleone na mkewe Daniella yaibua gumzo Uganda

g

Mahakama mjini Kampala, Uganda, imeahirisha kesi ya talaka kati ya mtunzi na muimbaji maarufu wa muziki nchini humo Jose Chameleone na mkewe Daniella Atim hadi Septemba ijayo kutokana na kutoelewana kati ya pande hizo mbili.

Hii ni moja ya habari zinazogonga vichwa vya habari na kujadiliwa sana nchini Uganda na miongoni mwa wapenzi wa muziki mkoani humo wanaomfahamu msanii Jose Chameleone.

Magazeti ya Uganda yanaripoti kwamba Chameleone – majina halisi Joseph Mayanja, na Daniella, wanatofautiana kuhusu mgawanyo wa mali, ikiwa ni pamoja na nani atapapewa idhini ya malezi ya watoto, na nani atakuwa mlezi pekee.

Chameleone na Daniella wameoana kwa takriban miaka 17, na msanii huyo ameimba kuhusu mapenzi yake kwa Daniella katika baadhi ya nyimbo zake maarufu kwa miaka mingi.

Mwezi Machi mwaka huu, Daniella ambaye sasa anaishi Marekani aliomba mahakama katika mji mkuu wa Kampala kumtenganisha na mumewe.

Nyaraka za mahakama zilizonukuliwa na magazeti ya Uganda zinasema kwamba Daniella anamshutumu Chameleone kwa kutelekeza familia kihisia kwa miaka mingi, kupuuza majukumu yake, na kushindwa kukidhi mahitaji ya kaya.

Daniella mara nyingi huchapisha kwenye mitandao ya kijamii matatizo makubwa aliyoyapata katika ndoa yake, ikiwa ni pamoja na unyanyasaji, ambao anadai uliutoroka na kukimbilia Marekani kutoroka.

Katika taarifa yake kwenye mitandao ya kijamii usiku wa kuamkia leo, Jose Chameleone alisema kuwa Daniella aliwachukua watoto hao na kwenda kuishi Marekani kwa ridhaa yao ya pande zote mbili, na kwamba hakuwatelekeza wala kuacha majukumu yake kama anavyotuhumiwa.

Alisema anataka kuendelea kupata watoto wake na kwamba popote walipo, atawapelekea kile wanachohitaji mara kwa mara.

Huku ikisemekana wapendanao hao wa zamani wako katika hali nzuri na kutaka utengano ulioombwa na mke, suala bado liko kuhusu mali.

Magazeti ya Uganda yanaripoti kwamba Daniella Atim anataka kupewa nyumba huko Seguku, kusini mwa Kampala, ulezi kamili wa watoto wao watano, na kwamba Chameleone aagizwe kugharamia matunzo yao.

Chameleone alisikika akisema alikasirishwa na kitendo cha mkewe kumtaka “aonyeshe mambo yake nikiwa bado hai.” Pia alimshutumu mkewe kwa kuwafanya watoto wake wamchukie.

Akasema: “Tunachopigania sio changu ni cha watoto wetu. Na watoto hao watawaachia watoto wao. Tatizo langu wananilazimisha kurithi mali hizi nikiwa hai na mzima.”

Chameleone anadhani yeye na Daniella wanapaswa kutoa huduma ya watoto kwa sababu wote wanafanya kazi.

Mahakama ilisikiliza pande zote mbili na kuahirisha kesi hiyo hadi mwezi ujao.

Marekani yamzuia kiongozi wa Palestina kuhudhuria mkutano wa Umoja wa Mataifa mjini New York

h

Kiongozi wa Palestina Mahmoud Abbas alikuwa akipanga kusafiri kwenda New York kwa mkutano wa Umoja wa Mataifa

Rais wa Palestina Mahmoud Abbas amezuiwa kuhudhuria kikao cha Baraza Kuu la Umoja wa Mataifa mjini New York mwezi ujao baada ya yeye na maafisa wengine 80 wa Palestina kufutiwa viza zao, Wizara ya Mambo ya Nje ya Marekani imethibitisha.

Waziri wa Mambo ya Nje wa Marekani Marco Rubio aliwalaumu kwa kuhujumu juhudi za amani na kutafuta “kutambuliwa kwa upande mmoja kwa taifa la Palestina la kudhaniwa”.

Uamuzi huo ambao umekaribishwa na Israel si wa kawaida kwani Marekani inatarajiwa kurahisisha usafiri kwa maafisa wa nchi zote zinazotaka kutembelea makao makuu ya Umoja wa Mataifa.

Marufuku hiyo inajiri wakati Ufaransa ikiongoza juhudi za kimataifa za kulitambua taifa la Palestina katika kikao hicho – hatua ambayo utawala wa Donald Trump umeipinga.

Balozi wa Palestina katika Umoja wa Mataifa, Riyad Mansour, alisema hapo awali kwamba kama mkuu wa ujumbe wake, Abbas atahudhuria mkutano wa wakuu wa nchi na serikali huko New York.

Lakini afisa wa Wizara ya Mambo ya Nje baadaye alisema Abbas na Wapalestina wengine wapatao 80 wataathiriwa na uamuzi wa kukataa na kufuta viza kutoka kwa wanachama wa Harakati ya Ukombozi wa Palestina (PLO) na Mamlaka ya Palestina (PA).

Ofisi ya Abbas ilisema ilishangazwa na uamuzi huo wa kumnyima viza, ambao “unapingana waziwazi na sheria za kimataifa na Mkataba wa Makao Makuu ya Umoja wa Mataifa, hasa kwa vile Taifa la Palestina ni mwanachama waangalizi wa Umoja wa Mataifa”. Iliitaka Marekani kubadili hatua hiyo.

All Rights Reserved © The Cantona Group PLC||2025


Discover more from cantonadigital

Subscribe to get the latest posts sent to your email.

Leave a comment