Radio Fortune Africa -Na Cantona Joseph
https://zeno.fm/radio/radio-fortune-africa

Jeshi la Wanamaji la Iran linasema lilitumia makombora matatu ya baharini, yaliyopewa jina la “Nasir, Ghadir, na Ghader,” katika mazoezi ya kombora ya “Eqtdar Paydar 1404”.
Haya ni mazoezi ya kwanza ya kijeshi kwa Iran tangu vita vya siku 12 na Israel.
Kwa mujibu wa tangazo la Jeshi la Wanamaji la Iran, zoezi hili la kombora lilianza (Alhamisi, Agosti 21) kwa lengo la kuonyesha “nguvu ya ulinzi na kujaribu silaha za hivi karibuni” kaskazini mwa Bahari ya Hindi na Bahari ya Oman, na “vitengo vya ardhini, vitengo vya kuruka, maeneo ya makombora ya ufuo wa Bahari na wengineo”.
Kwa mujibu wa televisheni ya taifa ya Iran, wakati wa mazoezi hayo makombora na ndege zisizo na rubani yalirushwa kwenye shabaha katika maji ya Bahari ya Hindi.
Awali Admiral Abbas Hassani, msemaji wa zoezi hilo, alisema kwamba zoezi hilo litafanyika kwa siku mbili. Hata hivyo, idara ya mahusiano ya umma ya jeshi ilitangaza kuwa zoezi la kombora lilimalizika kwa “kufikia malengo yaliyopangwa mapema”.
Zoezi hili la kombora lilifanyika takriban mwezi mmoja baada ya mazoezi ya pamoja ya Iran na Urusi, ambayo yalifanyika katika maji ya Bahari ya Caspian.
Lil Nas X akamatwa akizurura mitaani akiwa na suruali ya ndani pekee

Rapa aliyeshinda tuzo nyingi Lil Nas X amekamatwa baada ya kuzozana na polisi huko Los Angeles, mamlaka imethibitisha.
Polisi waliitwa huko Ventura Boulevard saa 05:30 saa za eneo siku ya Alhamisi baada ya ripoti za mtu kutembea barabarani akiwa amevaa suruali ya ndani pekee, msemaji wa Idara ya Polisi ya Los Angeles (LAPD) alisema.
Baada ya maafisa kufika katika eneo la tukio, idara ya polisi inadai kwamba mwimbaji huyo “alizozana” nao na kuwekwa chini ya ulinzi kwa tuhuma za kuwashambulia.
Kisha akapelekwa hospitali kwa matibabu kwa uwezekano wa kunywa dawa kupita kiasi. BBC imewafikia wawakilishi wake kwa maoni yao.
Erik Menendez anyimwa kuachiliwa kwa msamaha miaka 30 baada ya kuwaua wazazi wake huko LA

Erik Menendez amenyimwa kuachiliwa kwa msamaha baada ya kutoa ombi lake mbele ya bodi ya msamaha ya California.
Yeye na mdogo wake ambao wote ni mashuhuri, walipatikana na hatia katika mauaji ya 1989 ya wazazi wao matajiri huko Beverly Hills, na alitoa ombi lake la kwanza kwa bodi ya msamaha Alhamisi asubuhi.
Kaka yake, Lyle, ombi lake la kuachiliwa kwa msamaha kumeratibiwa kusikilizwa siku ya Ijumaa.
Ndugu wote wawili walistahiki kuomba kuachiliwa kwa msamaha baada ya kupewa hukumu mpya na hakimu mnamo mwezi Mei.
Erik Menendez anaweza kujaribu kuomba tena kuachiliwa kwa msamaha katika kesi nyingine baada ya miaka mitatu, bodi iliamua.
Israel kuanza mazungumzo ya kuachiliwa huru mateka wote, Netanyahu asema

Waziri Mkuu wa Israel Benjamin Netanyahu amesema ameagiza kuanza kwa mazungumzo ya kuachiliwa kwa mateka wote waliosalia na kukomesha vita huko Gaza kwa masharti “yanayokubalika na Israel”.
Netanyahu aliwaambia wanajeshi wa Israel Alhamisi usiku kwamba baraza lake la mawaziri pia limeidhinisha mipango ya shambulio kubwa katika mji wa Gaza kaskazini mwa eneo hilo, licha ya upinzani mkubwa wa kimataifa na wa ndani.
Hamas ilikubali pendekezo lililotolewa na wapatanishi wa Qatar na Misri kwa ajili ya kusitisha mapigano kwa siku 60 siku ya Jumatatu, ambayo kwa mujibu wa Qatar itashuhudia kuachiliwa kwa nusu ya mateka waliosalia huko Gaza.
Lakini akijibu kwa mara ya kwanza, Netanyahu hajakubali mpango huo uliopo mezani kwa sasa.
Vyombo vya habari vya Israel vimemnukuu afisa wa Israel akisema wapatanishi watatumwa kwa mazungumzo mapya pindi eneo litakapoamuliwa.
Katika taarifa yake ya video alipotembelea makao makuu ya kitengo cha Gaza nchini Israel Alhamisi usiku, Netanyahu alisema “ameagiza kuanza mara moja mazungumzo ya kuachiliwa kwa mateka wetu wote”.
“Nimekuja kuidhinisha mipango ya IDF (Vikosi vya Ulinzi vya Israel) kuchukua udhibiti wa Mji wa Gaza na kuwashinda Hamas,” alisema.
All Rights Reserved © The Cantona Group PLC||2025
Discover more from cantonadigital
Subscribe to get the latest posts sent to your email.