Radio Fortune Africa -Na Cantona Joseph
https://zeno.fm/radio/radio-fortune-africa

Jana mchana Donald Trump alizungumza na vyombo vya habari katika Ikulu ya White House kuhusu mkutano wake na Putin na hiki ndicho alichokisema:
- Trump alisema kwamba, kama asingekuwa rais, Putin “afadhali zaidi… aichukue Ukraine yote”, na kuongeza kuwa: “Lakini mimi ni rais, na hatanisumbua.”
- Trump alisema atajua katika dakika chache za kwanza kama yeye na Putin “watakuwa na mkutano mzuri”, akisema kwamba vinginevyo “utaisha haraka sana”
- Lengo lake la mazungumzo hayo, alisema, ni “kuweka meza” kwa mkutano mwingine na kiongozi wa Urusi na Rais wa Ukraine Zelensky.
- Akiongea na Fox News Radio mapema jana, Trump alisema ikiwa ni “mkutano mzuri” atampigia simu Zelensky kupanga mwingine, lakini akaongeza kuna uwezekano wa “25% mkutano huu hautakuwa na mafanikio”
- Na rais huyo wa Marekani alisema itabidi kuwe na baadhi ya “kutoa na kuchukua ” kwenye mipaka kati ya Urusi na Ukraine
All Rights Reserved © The Cantona Group PLC||2025
Discover more from cantonadigital
Subscribe to get the latest posts sent to your email.