Mali: Jeshi lawakamata washukiwa wa njama ya kutekeleza mapinduzi

Radio Fortune Africa -Na Cantona Joseph

https://zeno.fm/radio/radio-fortune-africa

Mali imewakamata makumi ya wanajeshi wanaoshukiwa kupanga njama ya kupindua serikali ya kijeshi, ambayo yenyewe ilichukua mamlaka katika nchi hiyo ya Afrika Magharibi katika mapinduzi.

Rais wa mpito wa Mali Jenerali Assimi Goita Juni 23, 2025. Pavel Bednyakov/Pool via REUTERS
Rais wa mpito wa Mali Jenerali Assimi Goita Juni 23, 2025. Pavel Bednyakov/Pool via REUTERS via REUTERS – Pavel Bednyakov

Tangu kuchukua madaraka katika mapinduzi ya 2020 na 2021, jeshi limeendeleza ukandamizaji dhidi ya wakosoaji wake licha ya kuenea kwa utovu wa usalama kutokana na mashambulio ya wanajihadi.

Kwa siku tatu sasa, jeshi limeendeleza kamatakamata ambapo hadi sasa watu 20 wamekamatwa kwa mujibu wa vyanzo wa usalama nchini humo, wanajeshi wawili wakiripotiwa kukamatwa usiku wa jumapili kuamkia Jumatatu.

Miongoni mwa waliokamatwa ni jenerali Abass Dembele aliyewahi kuwa gavana katika eneo la Mopti ya kati na afisa wa jeshi anayeheshimika.

Tangu 2021, mali imekumbwa na mashamnbulio ya wanajihadi wanaohusishw a na kundi la al qaeda na Islamic tstae ambao wamekuwa wakiendeleza mashambulio katika   eneo la sahel.

All Rights Reserved © The Cantona Group PLC||2025


Discover more from cantonadigital

Subscribe to get the latest posts sent to your email.

Leave a comment