Radio Fortune Africa -Na Cantona Joseph
https://zeno.fm/radio/radio-fortune-africa

Maafisa wanane wa polisi wamejeruhiwa katika mlipuko uliotokea kwenye gari yao katika barabara ya Banabs-Yumbis huko kaunti ya Garissa, mamlaka ya polisi ilisema.
Kundi hilo lilikuwa likisafiri kwa gari la polisi la Mine Resistant Ambush Protected (MRAP) katika eneo hilo jioni ya Jumanne, Agosti 5, gari hilo lilipokanyaga kilipuzi.
Hii ilikuwa baada ya timu ya Kitengo cha Doria ya Mipakani kuvamiwa na kuhusika katika tukio la kurushiana risasi na watu wenye silaha wanaoaminika kuwa wanachama wa wanamgambo wa al-Shabaab.
Gari aina ya Land Cruiser la pili likiwa na maafisa wa polisi zaidi lilifika eneo la tukio kuwaokoa wenzao waliokuwa wamekwama.
Waliokolewa kutoka kwa gari lililokuwa linaungua na kukimbizwa hospitalini wakiwa na majeraha mabaya huku washambuliaji wakifanikiwa kutoroka eneo la tukio, polisi walisema.
Baadaye walihamishwa hadi hospitali ya eneo hilo kwa uangalizi zaidi kabla ya mpango wa kuhamishwa hadi Nairobi, maafisa walisema.
Wawili kuwania urais ACT, yupo Mpina

Halmashauri Kuu ya Chama cha ACT Wazalendo kwenye kikao maalum kilichofanyika jana tarehe 5 Agosti 2025 kwenye ukumbi wa Hakainde Hichilema pamoja na mambo mengine ilipendekeza majina ya wagombea wa Urais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania na Urais wa Zanzibar.
Kwa mujibu wa Shangwe Ayo, Naibu Katibu wa Habari, Uenezi na Mahusiano na Umma, ACT Wazalendo, kwa upande wa Urais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, majina yaliyopendekezwa ni;
1. Aaron Kalikawe
2. Luhaga Mpina
Kwa upande wa Urais wa Zanzibar Halmashauri Kuu imependekeza jina la Ndugu Othman Masoud Othman ambaye ndiye mwanachama pekee aliyechukua fomu ya kugombea nafasi hiyo.
Ndugu Othman Masoud Othman pia ni Mwenyekiti wa Taifa wa Chama na Makamu wa Kwanza wa Rais wa Zanzibar.
Majina ya wagombea yaliyopendekezwa yatawasilishwa kwa Mkutano Mkuu Taifa kwa ajili ya kupigiwa kura.
Katika hatua nyingine, Halmashauri Kuu ilipokea na kuridhia hatua ya mgombea wa Urais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ndugu Dorothy Jonas Semu kujitoa kugombea nafasi ya Urais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania.

Kwenye maelezo yake mbele ya Halmashauri Kuu Ndugu Dorothy Semu ambaye pia ni Kiongozi wa Chama cha ACT Wazalendo aliieleza Halmashauri Kuu kuwa alichukua hatua hiyo katika kutekeleza wajibu wake wa kiuongozi wa kukiwezesha Chama kutekeleza wajibu wake wa kimapambano wa kuiondosha CCM madarakani kwenye Uchaguzi Mkuu 2025 kwa kuzingatia mazingira ya kisiasa ya sasa nchini.
All Rights Reserved © The Cantona Group PLC||2025
Discover more from cantonadigital
Subscribe to get the latest posts sent to your email.