Kocha wa DRC, Ngoma atafuta suluhisho la haraka baada ya kuanza vibaya

Radio Fortune Africa -Na Cantona Joseph

https://zeno.fm/radio/radio-fortune-africa

Nairobi, Kenya – Kocha Mkuu wa Jamhuri ya Kidemokrasia ya Kongo Otis Ngoma alitaja maandalizi duni na utimamu wa kutosha wa mechi kuwa sababu kuu za timu yake kushindwa 1-0 na Kenya katika mechi ya ufunguzi ya michuano ya Kombe la Mataifa ya Afrika (CHAN) 2024.

Kocha wa DRC Otis Ngoma angali anafukuzia ushindi wake wa kwanza kama kocha wa Leopard
Kocha wa DRC Otis Ngoma angali anafukuzia ushindi wake wa kwanza kama kocha wa Leopard © CAF Media

Leopards, mabingwa mara mbili wa CHAN, walianza kampeni yao ya Kundi A kwa Bahati mbaya kwa kufungwa na Harambee Stars Jumapili katika mechi ambayo kumiliki mpira na juhudi hazikutosha kuepuka kushindwa.

Licha ya kuonesha ari kipindi cha pili, Wakongo walishindwa kubadilisha nafasi zao na sasa wanakabiliwa na mchezo muhimu wa pili kwenye kundi A dhidi ya Zambia siku ya Alhamisi wiki hii.

Uundaji Duni wa DRC

Otis Ngoma, kocha wa DR Congo
Otis Ngoma, kocha wa DR Congo BackpagePix – Djaffar Ladjal/BackpagePix

Mahangaiko ya DR Congo, kulingana na kocha Ngoma, yanatokana na mchanganyiko wa ubutu na kambi duni ya maandalizi kabla ya mechi.

Huku msimu wa ligi ya ndani ukimalizika kabla ya muda wake na wachezaji kutocheza mechi za kirafiki kuelekea CHAN, vijana hao wa Ngoma waliingia kwenye michuano hiyo wakiwa hawajatayarishwa vizuri.

“Tuna wachezaji ambao hawana ushindani. Leo tumepoteza mipira mingi, tulikosa nafasi za mabao labda kutokana na uchovu, kutokuwa makini, kukosa umakini, lakini pia maelezo mengine,” Ngoma alisema kwenye mkutano na waandishi wa habari baada ya mechi.

Ili kuonyesha maudhui haya X (Twitter) maudhui, unahitaji kuidhinisha kipimo cha hadhira na vidakuzi vya matangazo.KubaliDhibiti chaguo langu

Wakongo walikuwa na wiki mbili na nusu tu za maandalizi, kipindi ambacho Ngoma alikiri hakitoshi kujenga muunganiko wa timu na kemia ya wachezaji.

“Kambi ya mazoezi ya kabla ya mashindano haikuwa kama inavyopaswa kuwa.

“Kumalizika kwa mapema kwa ligi yetu kulimaanisha wachezaji hawakucheza vya kutosha. Hili ndilo lililotuumiza usiku wa leo,” alisema.

Kukosa kutumia fursa kadhaa

Jephte Kitambala Bola wa DR Congo akimkabili Sylvester Owino Ahono wa Kenya wakati wa michuano ya Mataifa ya Afrika ya 2024, CHAN, mechi ya kandanda kati ya Kenya na DR Congo kwenye Uwanja wa kasarani jijini Nairobi , Kenya mnamo 03 Agosti 2025
Jephte Kitambala Bola wa DR Congo akimkabili Sylvester Owino Ahono wa Kenya wakati wa michuano ya Mataifa ya Afrika ya 2024, CHAN, mechi ya kandanda kati ya Kenya na DR Congo kwenye Uwanja wa kasarani jijini Nairobi , Kenya mnamo 03 Agosti 2025 BackpagePix – Djaffar Ladjal/BackpagePix

Licha ya kushindwa, mechi dhidi ya Kenya haikuwa ya upande mmoja kabisa. Leopards walifurahia muda mwingi wa kumiliki mpira, haswa katika kipindi cha pili, na kutengeneza nafasi nyingi ambazo zingeweza kubadilisha matokeo.

Hata hivyo, safu ya ulinzi ya Kenya ilionyesha uthabiti, na kuzima mashambulizi ya Wakongo kwa utulivu na nidhamu ya kimbinu. Ukosefu wa ubunifu na makali ya mwisho katika kijisanduku cha Kenya ulionekana – taswira nyingine ya kuvurugika kwa maandalizi ya Leopards.

“Hatukuwa wachangamfu wa kutosha. Kulikuwa na mzunguko mzuri wa mpira, lakini uchezaji katika safu ya tatu ya ushambuliaji haukuwa na makali,” alisema mwanachama wa timu ya kiufundi ya Kongo.

Kipigo hicho kimeendelea kutia wasiwasi kwa Ngoma, ambaye bado anasaka ushindi wake wa kwanza katika awamu ya mwisho ya michuano ya CHAN akiwa kocha mkuu. Pia inaiweka DR Congo katika nafasi ya hatari kabla ya mechi muhimu ya pili.

Kuvunjika kwa mwiko si mwisho wa kupika

Mashabiki wa DR Congo katika mechi dhidi ya Kenya
Mashabiki wa DR Congo katika mechi dhidi ya Kenya © BackpagePix – Djaffar Ladjal/BackpagePix

Licha ya kupoteza, Ngoma alipaza sauti ya matumaini huku akitazama mbele kwa sehemu iliyosalia ya hatua ya makundi.

Huku kukiwa na mechi tatu kuchezwa, mwalimu huyo wa Kongo bado ana imani kuwa timu yake inaweza kubadilisha mambo.

“Tutarejea katika hali nzuri kadri mechi zinavyosonga. Tunahitaji pointi sita pekee ili tufuzu, na bado kuna mechi tatu,” alisema.

“Nina imani wachezaji watarejea haraka.”

Kazi inayofuata ya Jamhuri ya Kidemokrasia ya Kongo ni kukutana kwa dau la juu na Zambia mnamo Alhamisi, 7 Agosti 2025. Ushindi sasa unaonekana kuwa jambo la kutojadiliwa iwapo Leopards wangependa kusalia katika kinyang’anyiro cha kufuzu katika awamu ya muondoano.

“Kushindwa kwingine kutatuweka kwenye ukingo wa kuondolewa,” Ngoma alikiri.

“Tunahitaji kurejesha imani katika kundi na kutafuta ushindi wa kwanza.”

Kenya kama Tanzania yafungua kampeni na ushindi

Kenya wakisherehekea baada ya Austin Odhiambo kufunga bao la ushindi
Kenya wakisherehekea baada ya Austin Odhiambo kufunga bao la ushindi © BackpagePix – Djaffar Ladjal/BackpagePix

Kwenye kambi ya wenyeji Kenya, furaha ilighubika kila mchezaji na mwanachama wa benchi la ufundi baada ya ushindi huo ila kocha mkuu Bennie McCarthy alikiri kuwa lazima wamakinike zaidi katika mechi ya pili ya makundi dhidi ya Angola, Alhamisi wiki hii.

Hii ni mara ya kwanza kabisa Kenya kushiriki michuano hii na walianza kwa ushindi kupitia bao la kiungo wa kati wa Gor Mahia, Austine Odhiambo katika dakika za nyongeza kipindi cha kwanza.

“Najivunia sana timu yangu. Wengi wao ni mara ya kwanza kucheza katika jukwaa kubwa kama hili chini ya shinikizo kubwa kama hii.

“DRC ni timu inayojua maana ya kushinda na kucheza hapa sababu ni mabingwa mara mbili,” alibainisha kocha McCarthy.

All Rights Reserved © The Cantona Group PLC||2025


Discover more from cantonadigital

Subscribe to get the latest posts sent to your email.

Leave a comment